Kuongeza kodi ni kuongeza umasikini...

I was just watching how Obama lifted USA out of bad state... kwakweli bado tuna safari ndefu...

Mkubwa alifacilitate circulation ya pesa na commodities, sisi naona tumechagua the opposite route ya kubana

Risk ya kubana na kulimbikiza everything centrally ni pale kwenye disaster zozote zile

Umeona Magufuli anataka Serikali iagize sukari
mifuko ya jamii iwekeze kwenye viwanda
serikali ifanye hiki na kile...

hii ni disaster in the making.....
hakuna facilitation ya watu kufanya chochote
hata kuhoji tu hairuhusiwi.....
 
Tangu serikali hii ya tano iingie umekuwepo na msisitizo wa kukusanya kodi mkubwa
lakini hata hivyo imekuwepo na tabia za kupandisha kodi maeneo mbalimbali kiholela

na hata hii bajeti ya sasa inaonesha wazi serikali hii ya awamu ya tano wanachotaka
wao ni kodi tu hata kama kodi hiyo 'itaua' baadhi ya biashara za watu....

Ukweli ni kwamba wanachokifanya ni 'kumkamua maradufu ng'ombe maziwa' huku ng'ombe mwenyewe
hana afya ya kutosha na chakula chake kinazidi kupungua......

Kwa mwendo huu umasikini utaongezeka......biashara zitakufa na hayo mapato yatapungua

Ilikuwa busara zaidi ng'ombe akaongezewa kwanza chakula na matunzo na hata kupunguza
kumkamua kwanza ili anawiri ndo ukamuaji ufuatie......

Mentality kuwa watanzania wengi wana pesa na hawalipi kodi ni hatari sana...
Ukweli ni kuwa watanzania wengi ni masikni na wanaishi kwa kubangaiza zaidi
biashara rasmi ni chache sana na gharama za umeme,kodi na nyinginezo ni kuubwa sana...

Serikali ilipaswa kutumia nguvu kubwa kwenye 'new economy' na Utalii...ambako hakuna
mafanikio ya kuridhisha......kuliko kukazania kuongeza kodi kwa mwananchi....

kodi zinavyo zidi na umasikini unazidi

.
Ahsante sana mkuu nakuunga mikono na miguu ni watanzania wachache sana wana uelewa wa mambo haya ya ongezeko la kodi na ndo mana kuna wengine wanadiriki kufurahi kitu fulani kikiongezewa kodi ambapo hasara ni kwetu lakini najua its a matter of time wote tutainamisha vichwa kwa ugumu wa maisha kwa mwendo huu.
 
Umeona Magufuli anataka Serikali iagize sukari
mifuko ya jamii iwekeze kwenye viwanda
serikali ifanye hiki na kile...

hii ni disaster in the making.....
hakuna facilitation ya watu kufanya chochote
hata kuhoji tu hairuhusiwi.....
yani hapo kwenye mifuko ya jamii usinikumbushe machungu mkuu Iknow god is watching hata mfalme nebukdnz Mungu aliingilia kati utawala wake si kwa kunyonywa huku kusiko na hatia na utu.
 
Wachunguzi wengi wanasema ni vema watanzania wakamuliwe hadi damu na ikiwezekana wengine wafe kwa njaa ili wajue umuhimu wa kung'oa ccm madarakani , binafsi nimefurahishwa sana kwa masikini kukomeshwa .
hahahahaha nimecheka ana ingawa si cha kucheka ni kuonea huruma
 
Afrika ni masikini kwa sababu hatutozi kodi. Ulaya kodi ndo maendeleo.

Ndo maana wanaona wanatupa hela za walipa kodo wao harafu sisi tunazifuja. Mwisho wanatudharau.

Kwetu huku, Rwanda inaongoza kwa kulipa kodi na hakuna anayesema na mwisho tunasema inapiga hatua.

Sijui sisi tutakuwa lini kiuchumi kwa kauli kama hizi.
huwezi kujilinganisha na ulaya at all sisi ni dunia ya tatu ,kwa Tabia zetu za ubiunafsi ndo yametufika haya hata hicho kidogo kinachokusanywa kinatumika vibaya why then kuongeza?kwanza asilimia kubwa ni maskini sasa sijui unawasaidiaje kwa kuchukua hata kile kidogo.
 
Maduka ya wakwepa kodi yafungwe tu. Watajitokeza wafanyabiashara halali na kufanya biashara hizo. Kutakuwa na kipindi cha mpito chenye matatizo lakini mwishowe mambo yatakaa sawa.
Tanzania haitakuwa ya kwanza kupitia mchakato huo. Afterall, hao "wafanyabiashara" wataishi vipi? Hili linauma sehemu zote. Wengine watafilisika kimoja!
Hahahahaha huo mpito si wa leo hata kesho utasubiri sana kufika promised land mana matatizo yaliyoko si ya mpito wa leo hata kesho kama miaka hamsini yalishindikana sembuse kumi utakaa sana ndugu .kila kitu lazima kiwe na kiasi si kukamuana mpk damu.ni sawa na wewe ulaze familia njaa kisa unajenga nyumba .Kila kitu lazima kiendelee kistrategic sio kiforce .Note: usije ukakimbia mpk ukapitiliza kwenu.
 
Ukawa walitoka nje ya bunge kupinga sheria ya makosa ya mtandaoni kwamba ni sheria mbaya sana na kandamizi kwa wananchi, ! Leo ni miezi 9 tokea sheria ianze kufanya kazi ,sasa nyinyi nyumbu tuwaulize mpaka sasa sheria ya mtandaoni imeshamkandamiza nani??
Siasa za kupotosha watu kiasi hiki hazitawafikisha popote nyinyi UKIWA.
 
Afrika ni masikini kwa sababu hatutozi kodi. Ulaya kodi ndo maendeleo.

Ndo maana wanaona wanatupa hela za walipa kodo wao harafu sisi tunazifuja. Mwisho wanatudharau.

Kwetu huku, Rwanda inaongoza kwa kulipa kodi na hakuna anayesema na mwisho tunasema inapiga hatua.

Sijui sisi tutakuwa lini kiuchumi kwa kauli kama hizi.
Ni kwel lkn je kiwango cha kodi rwanda kikoje ndugu makato na ukiangalia unachobakia nacho akitoshi unataka tena kusomesha mtt wako vizur mpk bei elekezi itoke mtt amekua mtu mzima makampuni ya cm tz yalikua na makato makubwa kwa mteja kwenye maongezi matokeo yake hasara kila uchwao wanakufa kibiashara nw days wameshusha ona ndo makampuni yanayopiga hela hili mtu alipe kodi vizur mpe gharama ndo ili aepuke usumbufu na kulipa kodi tena wote watalipa serikal aiangalii kama biashara nayofanya cpati faida ndo mana aikui wao lipa kodi ukifa atakuja mwingine fanya hiyo biashara
 
Usilalamike basi kuwa tuna maisha magumu kwa vile hutaki mabadiliko. Subiri wazungu aje kwa vile hatutaji kujisahihisha.

Kaulize wanaoendelea kama wanawaangalia wafanyabiashara usoni.
huwezi kujilinganisha na ulaya at all sisi ni dunia ya tatu ,kwa Tabia zetu za ubiunafsi ndo yametufika haya hata hicho kidogo kinachokusanywa kinatumika vibaya why then kuongeza?kwanza asilimia kubwa ni maskini sasa sijui unawasaidiaje kwa kuchukua hata kile kidogo.
 
Tuliambiwa huyu D Mpango ni genius mwenye mipango kibao lakini awamu ya nne hawakumsikiliza
now huyu huyu leo anaonyesha upungufu wa waziwazi wa kuongoza na kuja na mbinu mpya za kiuchumi
hii bajeti tunaweza sema 'the worst ever'....
Many people are Afraid of Changes.. Whoever resist to change will extinct. Wacha Serikali ifanye jambo linalofaa kwa hii nchi.... Tatizo wabongo kelele nyiingi and we know & achieve NOTHING.
 
Kwa kadiri ya mawazo yangu....
Ni ujinga kuwaza kuwa kukopa na kuongeza kodi kwa watanzania ama katika huduma z a kijamii na kibiashara ndiyo njia pekee ya kuendesha shughuli za kimaendeleo nchini huku nchi ikiruhusu kupokea 4% ya mapato ya madini yake kwa wawekezaji wa nje. 50% peke yake ya makanikia tuliyokamata ilitosha kuinua uwekezaji wa ndani na nje ya nchi kusababisha ukuaji kiuchumi na kupunguza upungufu wa ajira kwa vijana kwa kuwawezesha katika kilimo na usindikaji wa mazao. Fedha zilizowekezwa katika miradi ya kifisadi kama kule Chato na Dar es salaam zingewekezwa pia kuinua kilimo na viwanda leo hii tungeshuhudia kuimarika kwa shilingi ya Tanzania hadi kuwa $1 = Sh 1800 badala ya ilivyo sasa kuwa ni sh 2250! Vipaumbele vibovu na ufisadi wa uwekezaji kwenye mirdi isyozalisha haraka kama hii ya flyovers, pangaboi na treni ya mwendokasi ndivyo visababishi vikubwa kwa vichaa kuona njia pekee ya kupata pesa ni kuongeza kodi na gharama za huduma za jamii nchini
 
Kwa kadiri ya mawazo yangu....
Ni ujinga kuwaza kuwa kukopa na kuongeza kodi kwa watanzania ama katika huduma z a kijamii na kibiashara ndiyo njia pekee ya kuendesha shughuli za kimaendeleo nchini huku nchi ikiruhusu kupokea 4% ya mapato ya madini yake kwa wawekezaji wa nje. 50% peke yake ya makanikia tuliyokamata ilitosha kuinua uwekezaji wa ndani na nje ya nchi kusababisha ukuaji kiuchumi na kupunguza upungufu wa ajira kwa vijana kwa kuwawezesha katika kilimo na usindikaji wa mazao. Fedha zilizowekezwa katika miradi ya kifisadi kama kule Chato na Dar es salaam zingewekezwa pia kuinua kilimo na viwanda leo hii tungeshuhudia kuimarika kwa shilingi ya Tanzania hadi kuwa $1 = Sh 1800 badala ya ilivyo sasa kuwa ni sh 2250! Vipaumbele vibovu na ufisadi wa uwekezaji kwenye mirdi isyozalisha haraka kama hii ya flyovers, pangaboi na treni ya mwendokasi ndivyo visababishi vikubwa kwa vichaa kuona njia pekee ya kupata pesa ni kuongeza kodi na gharama za huduma za jamii nchini
Niwie radhi na mimi nitoe maoni yangu kwa mawazo yangu! Kama kumbukumbu zetu zitakuwa sahihi, kulikuwa na mjadala mpana bungeni na nje ya bunge juu ya athari za kiuchumi zilizokuwa zinaisibu nchi kutokana na msongamano wa magari Jijini Dar es Salaam. Mabilioni ya shilingi yamekuwa yakipotea kwa wafanyakazi na wadau wengineo wa maendeleo kupoteza muda mwingi kwenye foleni. Hivyo kuwekeza kwenye barabara za juu (flyovers) kama mmoja ya mbinu za kukabiliana na changamoto hiyo (ambayo pia naamini imetoa ajira kwa vijana) haijawa ni mipango ya kifisadi kama utaona umuhimu wake. Uharibifu wa barabara kutokana na magari ya mizigo, nadhani ni sababu tosha ya kujenga reli mpya (ambayo pia imetoa ajira kwa vijana). Tunaweza tusione matokeo chanya sasa hivi, lakini naamini kitambo si kirefu, tutaona manufaa yake!
Kuhusu uwanja wa ndege Chato, kama tutakuwa na uelewa wa jiografia ya Ziwa Magharibi, na kuelewa makusudio ya kimkakati, naamini tutaondokana na tuhuma zisizokuwa na msingi za kuuona mradi huu kama wa kifisadi.
Aidha ni ukweli usiopingika kwamba ukopaji na nyongeza ya kodi sio njia pekee ya pato la taifa. Lakini pia si sahihi kuiona kodi kama balaa (sio kwa tafsiri yako). Tunapaswa kuchukulia ulipaji kodi kama mmoja wa wajibu wa kila anayestahiki kulipa kodi. Nchi zingine ni wakali zaidi kwenye masuala ya ukwepaji kodi. Ni vyema basi nasi tukajenga utamaduni wa kulipa kodi pasi shuruti.
Kuhusu mrabaha wa madini, ni kweli serikali (kupitia mikataba mibovu) iliingia kwenye mfumo wa utandawazi na uwekezaji kwenye madini bila kuandaa sera na sheria za ukusanyaji wa mapato kutokana na madini. Haiwezekani kutumia sheria ya madini juu ya mrabaha kwa kutumia kiwango kile kile ujichokuwa unawatoza wachimbaji wadogo wadogo ambao pia ulikuwa unakusanya / unanunua dhahabu yao (STAMICO) na kuweka akiba Benki Kuu na huyu mwekezaji mkuu anakulipa 3% na anakwenda na dhahabu yote kwao. Haiwezekani kuwapa likizo ya kodi (Holiday Tax) wakati wachimbaji wadogo wadogo / wachimbaji wazawa wanaminywa kodi! Haiwezekani!
Kwa kuwa tuko kwenye kipindi cha mabadiliko (transition period), na kwa kuwa kila enzi na kitabu chake, ni vyema tukavuta subira na kuishauri serikali (kupitia majukwaa mbali mbali) juu ya njia mwafaka na yenye mtizamo chanya ya kutupeleka mbele. Tuikosoe kirafiki na kuipongeza pale inapofanya vizuri!
Tujitafakari!
 
Niwie radhi na mimi nitoe maoni yangu kwa mawazo yangu! Kama kumbukumbu zetu zitakuwa sahihi, kulikuwa na mjadala mpana bungeni na nje ya bunge juu ya athari za kiuchumi zilizokuwa zinaisibu nchi kutokana na msongamano wa magari Jijini Dar es Salaam. Mabilioni ya shilingi yamekuwa yakipotea kwa wafanyakazi na wadau wengineo wa maendeleo kupoteza muda mwingi kwenye foleni. Hivyo kuwekeza kwenye barabara za juu (flyovers) kama mmoja ya mbinu za kukabiliana na changamoto hiyo (ambayo pia naamini imetoa ajira kwa vijana) haijawa ni mipango ya kifisadi kama utaona umuhimu wake. Uharibifu wa barabara kutokana na magari ya mizigo, nadhani ni sababu tosha ya kujenga reli mpya (ambayo pia imetoa ajira kwa vijana). Tunaweza tusione matokeo chanya sasa hivi, lakini naamini kitambo si kirefu, tutaona manufaa yake!
Kuhusu uwanja wa ndege Chato, kama tutakuwa na uelewa wa jiografia ya Ziwa Magharibi, na kuelewa makusudio ya kimkakati, naamini tutaondokana na tuhuma zisizokuwa na msingi za kuuona mradi huu kama wa kifisadi.
Aidha ni ukweli usiopingika kwamba ukopaji na nyongeza ya kodi sio njia pekee ya pato la taifa. Lakini pia si sahihi kuiona kodi kama balaa (sio kwa tafsiri yako). Tunapaswa kuchukulia ulipaji kodi kama mmoja wa wajibu wa kila anayestahiki kulipa kodi. Nchi zingine ni wakali zaidi kwenye masuala ya ukwepaji kodi. Ni vyema basi nasi tukajenga utamaduni wa kulipa kodi pasi shuruti.
Kuhusu mrabaha wa madini, ni kweli serikali (kupitia mikataba mibovu) iliingia kwenye mfumo wa utandawazi na uwekezaji kwenye madini bila kuandaa sera na sheria za ukusanyaji wa mapato kutokana na madini. Haiwezekani kutumia sheria ya madini juu ya mrabaha kwa kutumia kiwango kile kile ujichokuwa unawatoza wachimbaji wadogo wadogo ambao pia ulikuwa unakusanya / unanunua dhahabu yao (STAMICO) na kuweka akiba Benki Kuu na huyu mwekezaji mkuu anakulipa 3% na anakwenda na dhahabu yote kwao. Haiwezekani kuwapa likizo ya kodi (Holiday Tax) wakati wachimbaji wadogo wadogo / wachimbaji wazawa wanaminywa kodi! Haiwezekani!
Kwa kuwa tuko kwenye kipindi cha mabadiliko (transition period), na kwa kuwa kila enzi na kitabu chake, ni vyema tukavuta subira na kuishauri serikali (kupitia majukwaa mbali mbali) juu ya njia mwafaka na yenye mtizamo chanya ya kutupeleka mbele. Tuikosoe kirafiki na kuipongeza pale inapofanya vizuri!
Tujitafakari!
Nikujibu tu kifupi!!... Suala la Uchumi wa wenye magari na waishio Dar lisingechukuliwa kuwa kigezo pekee cha kusababisha kila mtanzania kuingia gharama kuchangia kuondolewa kwa madhila yao. Mipango mibovu ya uchumi kwa sehemu husika ndiyo sababu ya yote hayo na kujibidiisha kuwaneemisha watu wa Dar kwa kuwalazimisha watanzia wote kuwa watumwa wa mikopo isiyowapa tija ni udhalimu kiuchumi kwa mwananchi wa pembezoni!
 
Nikujibu tu kifupi!!... Suala la Uchumi wa wenye magari na waishio Dar lisingechukuliwa kuwa kigezo pekee cha kusababisha kila mtanzania kuingia gharama kuchangia kuondolewa kwa madhila yao. Mipango mibovu ya uchumi kwa sehemu husika ndiyo sababu ya yote hayo na kujibidiisha kuwaneemisha watu wa Dar kwa kuwalazimisha watanzia wote kuwa watumwa wa mikopo isiyowapa tija ni udhalimu kiuchumi kwa mwananchi wa pembezoni!
Taifa likikopa, kwa mfano, kwa ajili ya kujenga uwanja wa ndege Musoma, je, deni hilo haliwahusu watanzania wengine? Na je, utakuwa ni ufisadi?
Kila senti inayotumiwa, iwe kwa mkopo au bila mkopo (bila kujali mahali ilipotumika) ni mali ya Watanzania wote na kwa manufaa ya wote. Dar si ya wenye kuishi Dar tu. Na magari yaliyoko Dar si ya wanaoishi Dar tu.
Tujitafakari!
 
Kwa kadiri ya mawazo yangu....
Ni ujinga kuwaza kuwa kukopa na kuongeza kodi kwa watanzania ama katika huduma z a kijamii na kibiashara ndiyo njia pekee ya kuendesha shughuli za kimaendeleo nchini huku nchi ikiruhusu kupokea 4% ya mapato ya madini yake kwa wawekezaji wa nje. 50% peke yake ya makanikia tuliyokamata ilitosha kuinua uwekezaji wa ndani na nje ya nchi kusababisha ukuaji kiuchumi na kupunguza upungufu wa ajira kwa vijana kwa kuwawezesha katika kilimo na usindikaji wa mazao. Fedha zilizowekezwa katika miradi ya kifisadi kama kule Chato na Dar es salaam zingewekezwa pia kuinua kilimo na viwanda leo hii tungeshuhudia kuimarika kwa shilingi ya Tanzania hadi kuwa $1 = Sh 1800 badala ya ilivyo sasa kuwa ni sh 2250! Vipaumbele vibovu na ufisadi wa uwekezaji kwenye mirdi isyozalisha haraka kama hii ya flyovers, pangaboi na treni ya mwendokasi ndivyo visababishi vikubwa kwa vichaa kuona njia pekee ya kupata pesa ni kuongeza kodi na gharama za huduma za jamii nchini
Nini mbadala wa ulilolipinga?, vinginevyo ni wehu au kichaa kilichokomaa, pumbavu kuhani mkuu wewe.
 
Back
Top Bottom