Dingswayo
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 4,019
- 2,923
Kwa mara nyingi sasa nimekuwa nikiona watu wanaandika neno hili 'kuonesha'. Wakati mimi nasoma, na nimekuwa nikiandika pia kwa muda mrefu kwa lugha ya Kiswahili, nimekuwa nikitumia ' kuonyesha'. Nataka kuuliza hivi kuliandika neno hilo bila y ni kwa sababu ya lafudhi (dialect) tu, au limekubalika katika jamii? Ninavyoelewa mimi ni kuwa ukuandika, au kutanka 'kuonesha', unatumia lafudhi ya Zanzibar au Pemba. Sasa hili neno nalo limesambaa mpaka bara?