Kuolewa

Ongelea upande wa pili wa majukumu ya mume (in the same african marriage) ili usiwe biased. Chakula kinapokosekana nyumbani, ada ya shule wa watoto ikikosekana, makazi bora etc ni nani anawajibika? au wanawake hayo hawayaoni?

hahahahaaa! hata unachokiandika ni matokeo ya mfumo dume wenye mizizi mirefu sana. kwa sababu hujengwa toka tukiwa watoto, wala hatuoni kuwa ni tatizo. we take it for granted.
ndo maana hata wanawake wenye kipato kikubwa kuliko waume zao, bado hudai matumizi na mahitaji yao binafsi kutoka kwa waume zao wakiamini kuwa wao(wanawake) ni watu wa kutunzwa. pia wanaume wengine huamua kuwachisha kazi wake zao kwa sababu wao(waume) wana "wajibu" wa kuitunza familia. mwanaume amefanywa aone kwamba ana wajbu wa kuhakikisha familia yake inapata mahitaji yote ikiwa ni pamoja na uliyoyataja. kwa upande mwingine, mwanamke amefanywa ajione ni wa kutunzwa, kudekezwa, n.k hivyo, mume akishindwa kutimiza majukumu ya " kichwa cha nyumba," yafuatayo yanamhusu:

1. mkwewe atamwita mwanaume suruali, hivyo dharau kwa kwenda mbele kutoka kwa mkewe, ndugu wa mke na hata watoto wake na majirani

2. hata mwanaume mwenyewe hawezi kujisikia vizuri kwani anaona "kashindwa" kutimiza wajibu wake. hali hii hutokea hata kama mke ana hela, anaprovide for the whole family na wala hamnyanyasi mume wake.

sikwenda upande huu kwa sababu ningekuwa out of the topic mkuu
 
Hapo kwenye red; ina maana mwanaume akikuoa yeye hawi mtumwa kwako? Mi nadhani kila mtu anakuwa mtumwa wa mwenzake ila hujajushughulisha kufikiri ni kwa jinsi gani mwanaume naye anawajibika kwenye ndoa kwa nafasi yake kama mume. Ukiainisha majukumu ya mume na mke utakuta kila mtu ni mtumwa wa mwenzake ila kwa namna tofauti. Kama umelelewa kwenye familia ya wazazi wawili kumbuka majukumu gani Baba yako alikuwa anastruggle nayo na hata Mama yako alikuwa anasema ngoja tumwambie baba yako.

bold: haya majukumu hujengwa na jamii, wazazi au wanafamilia wanakuwa walimu tu. that's why majukumu ya wanawake na wanaume hutofautiana kati ya jamii moja na nyingine. mfano vijijini, ktk baadhi ya jamii, ujenzi wa nyumba ni jukumu la wanawake, tofauti na jamii zingine ambako jukumu hilo ni la wanaume

patriarchal system has caught us and we're like little flies in a web. we're all victims of the system
 
Hizi mila hizi zioneni hivi hivi...

kuna dada wa Bangladesh alitupa maelezo ya mila zao nikabaki kushangaa...

Kule bana mwanamke ndiye anayetoa mahari; kumbe maana ya kutoa mahari ni kulipia matunzo utakayo pewa na mumeo pindi atakapo kuoa. Hivyo wanawake hawafanyi kazi; wanaume ndio wanaotunza familia...

Kuna kaka wa Ki Sri Lanka naye alishawahi kunambia mahari inategemea na muoaji ana potential kiasi gani; the most expensive man kwao ni medical doctor...sasa ana dada yake alijipatia mchumba daktari, familia ilikuwa inahangaikaje kuzichanga ili mahari itimie....

Isije kuwa kiafrika tuna chimbuko la haya tunayoona ila hatuko explicit; ya kuwa kwa kuwa mume ndie mtunza familia basi mwanamke lazima umtumikie....na kama hiyo ndio sababu then haiwezi ku apply kwa wamama wanaotafuta kama wanaume...kwa kifupi ukitaka uwe treated kiafrika zaidi mkeo akae ndani atiii
 
hapa ndipo ninashindwa kuelewa kwanini niwe chini ya himaya yake???ni kwanini sote tusiwe chini ya kila mwenza?kwamba yeye yuko juu nad mwenye final says???
ukitaka iwe hivyo hata mahari nyumbani kwenu wasipokee au mtoleane mahari,lakini mwanaume akitoa mahari kwa mwanamke hiyo tayari mwanamke anakuwa chini ya mwanaume na ndo maana mwanamke hubadili hata jina kuanza kutumia la mumewe
 
hapa ndipo ninashindwa kuelewa kwanini niwe chini ya himaya yake???ni kwanini sote tusiwe chini ya kila mwenza?kwamba yeye yuko juu nad mwenye final says???

Katika mifumo yote mahali popote lazima kuwe na kiongozi...hata ndoa nayo ni hivyo hivyo...

Mkitaka kuishi pasipo kuwa na kichwa basi hapo ujue ndoa itageuka kuwa ndoana maana hakutakuwa na mtu mwenye final say...
 
Kuolewa kuna maana gani?
Mwanaume anaposema 'siwez kupika (mfano) kwani mi ndo nimeolewa?'
Does it mean kuolewa haina tofauti na kua mtumwa wa mwanaume?
Does it mean wanaume wanaoongea hayo hawajui maana ya kuoa?
What does kuolewa mean?

Kuna wakati nilikuwa nazungumza na Mr Rocky hapa na nilimuambia kuwa kwenye ndoa kunahitajika kila mtu ajue majukumu yake,hapo ndoa itakwenda angalau salama kidogo

Siku hizi watu hawajui hata ni kwanini wanaolewa na haya maswali yako yanadhihirisha hilo na sijui kama ukiolewa na mtazamo wako huu hiyo ndoa itakuwaje

Masuala ya kindoa ni magumu hasa kwenye ulimwengu huu usiokuwa na kiasi wala mipaka
Wakati Mungu alipomaliza kuwaumba hawa viume aliwapa majukumu na aliwaambia namna ya kuishi,najua na nye alijua kuwa hakuna maisha ambayo yataweza kwenda hivi tu bila kugawana majukumu miongoni mwa wale wanaoishi pamoja

Pia hakuna pahala popote ambapo watu wanakwenda tu bila kuwa na mtu mwenye kauli ya mwisho,yaani hakuna mahali ambapo watu wanaishi pamoja halafu kila mtu anaamua jambo kama vile atakavyo,haipo na haitakuja kuwepo milele

Kwenye suala la ndoa nalo ni hivyo pia
Mwanamke na mwanaume wapo tofauti kimaumbile,kimaumbile mwanamke ndie huishi na mtoto kuanzia anapozaliwa na hata kabla ya kuzaliwa yeye ndie hubeba ujauzito,hivyo kwa sababu hizi za kimaumbile mwanamke ndie hulazimika kuishi na watoto kwa ukaribu kwa muda mrefu atake asitake ndivyo ilivyo,sasa kuishi na watoto ni pamija na yale yanayowahusu hao watoto

Majukumu yanayomuhusu huyu anaetakiwa kuishi na wtoto muda mrefu nimengi lakini kwa uchache ni haya yafuatayo,huwezi kuishi na mtoto halafu asile.asivae huko kuvaa kunaendana na kufua pia,kuoga n.k

Mtu mwenye majukumu hayo analazimika awe yupo nyumbani muda wote ili aweze kuyatimiza hayo majukumu itakiwavyo,sasa kama huyo anatakiwa awepo nyumbani muda wpte ili atimize majukumu hayo ipasavyo kunatakiwa awepo wa kutafuta hela kwaajili ya manunuzi ya hayo mahitaji ya hiyo familia,hapo ndipo yule asiehitajika kimaumbile kukaa na watoto muda wote anapotakiwa kwenda muyatafuta hayo mahitaji

Hapo ndipo unapouja mgawanyo wa majukumu na ndipo iipokuja kuonekana kuwa kuna kazi za kike na kazi za kiume chimbuko lake hi hayo,suala la wewe kutaka mumeo akuoshee vyombo au akupikie sijui wewe utakuwa unafanya nini,sidhani kama kuna mwanamke mwadilifu ambae atataka mumewe apike halafu yeye akae tu

Jukumu la kutafuta mahitaji ni la mume kimaumbile na kiasili,leo kuna wajinga tu wanataka kulibadili hili ndio maana kuna matatizo mengi sana ya kimalezi kwa watu leo hii

Kama wewe utakuwa unafanya kazi bado sio kigezo cha kutokuyafanya majukumu yako kama mke na wala huo sio utumwa na haijawahi kuwa hivyo!
 
Last edited by a moderator:
Mimi huwa nasema 'mapenzi ' ni utumwa wa hiari
as long as unampenda mtu,tayari uko kwenye utumwa wa aina fulani
uwe mume au mke,
sasa wewe unaweza tu kuwa uko sensitive au umeolewa na usiempenda
mwanamke akianza kuhoji hoji kwa nini mwanaume anamwambia fanya hivi na fanya vile
mostly inakuwa hampendi yule mwanaume,aliolewa ili aolewe
wenzio walio in love na wanaume wao...wanarudi home wamechoka na still wanapika
na mume sometimes hata hiko chakula hajatoa pesa...na ukiwaambia waombe talaka wanakuchukia ...

Ukiamua kulichukulia kwa mtazamo huu ndoa inaweza kwenda japokuwa utakuwa unafanya kitu sahihi kwa mtazamo usio sahihi!
 
Kuolewa kuna maana gani?
Mwanaume anaposema 'siwez kupika (mfano) kwani mi ndo nimeolewa?'
Does it mean kuolewa haina tofauti na kua mtumwa wa mwanaume?
Does it mean wanaume wanaoongea hayo hawajui maana ya kuoa?
What does kuolewa mean?

Kiswahili chetu nadhani ndo kinatofautisha sana haya mambo. Wenzetu wazungu wana neno moja tu "get married" haijalishi mwanamke wala mwanamme. Kiswahili chetu kina mambo ya "w" kwa wanawake. Mfano ni maneno hapa chini

MME
1: oa
2: t..mba
3: lala
4: tumia
5: Piga mfano: wamempiga mtungo
6: Baka

MKE
1: ole"w"a
2: t..mb"w"a
3: lal"w"a
4: tumi"w"a
5: Pig'w"a mfano:amepigwa mtungo
6: bak"w"a
 
hapa ndipo ninashindwa kuelewa kwanini niwe chini ya himaya yake???ni kwanini sote tusiwe chini ya kila mwenza?kwamba yeye yuko juu nad mwenye final says???

Maisha ya kufikirika yatawaumizeni sana mabinti

Hakuna mahali maisha yameweza kwenda bila kuwa na mtu wa kauli ya mwisho
Ni bora ungedai wewe uwe na kauli yamwisho ungeeleweka
Lakini kudai mue sawa,haiwezekani

Hebu fikiria tu kama kuna aina hiyo ya maisha,kutakuwa na maamuzi kweli?
Wewe unakuja na kusema salary zote za mwezi huu tunakwenda kumalizia nyumba ya mama kule kijijini
Mumeo anakuja na kusema salary zote za mwaka huu tutazitumia kwaajili ya kufungua kampuni ya usafirishaji
Si vurugu tu hizo?

Au wewe unadhani mtaweza kwenda kwa style hiyo?
I doubt it!
 
Nakubaliana na wewe mfumo dume ndio tatizo na unawaathiri wote wanaume na wanawake.
ni mtazamo wangu tu jamani.....kiafrika, kuolewa ni sawa na kuikana nafsi yako na kuwa chini ya "kichwa cha nyumba". mfumo dume uko hata miongoni mwa wanawake wengi tu. baadhi ya wanawake hawapendi kuwaona waume zao wakifanya "kazi za wanawake" including cooking, washing, etc. na ikionekana mume anafanya hayo kwa ridhaa yake, watu husema kapigwa kipapai/limbwata.

mfumo dume is deep rooted and it can't be easily uprooted.

omba Mungu akuongoze upate mume aliyekombolewa ,kifikira ili asikufanye mtumwa wake.
 
hapa ndipo ninashindwa kuelewa kwanini niwe chini ya himaya yake???ni kwanini sote tusiwe chini ya kila mwenza?kwamba yeye yuko juu nad mwenye final says???

Huwezi kubadili mfumo!

Imagine: i. Kwa nini mwanaume ndo apeleke posa na kutoa mahari? Kwa nini na mwanamke naye asifanye hivyo?

ii. Kwa nini mwanamke ndo anaenda mahali anapokaa mwanaume? Kwa nini isiwe mwanaume kwenda kuishi kwa mwanamke? (Achana na case za Marios).

iii. Kwa nini ni mwanamke ndiye anayefanyiwa send-off? Na kwa Waislamu kuna sherehe ya Reception, kwa nini mwanaume ndiye anayefanya hii reception?

Ukiweza kuona hili, utaona zaidi ya hili kwenye ndoa. Ni mfumo tu!
 
Hayo mambo ndio yanatufanya wengine tuogope kuolewa unamtii mumeo na kumsikiliza kila anachosema hata kama amekosea anakuonea wewe unakuwa passive mh! ni kazi kwelikweli
swali lako inategemeana

waswahili au waafrika kuna kuoa na kuolewa

but wazungu hakuna hiyo,wanaoana

sasa wewe kama unataka usawa wa kizungu nayo ni tabu...
kiafrika ukiolewa unamsikiliza mumeo,unamtii....sio na wewe ulete amri zako
 
Back
Top Bottom