Kuoa! Ili iweje?

Kuoa! Ili iweje?

TAI DUME

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2014
Posts
10,745
Reaction score
29,219
1. Kama mpenzi wangu kila ijumaa anakuja kwangu na anasipendi nae mpaka jumapili usiku, nioe ili iweje?
2. Kama kila nguo zangu zikichafuka au nyumba ikihitaji usafi sikosi mwanamke wa kunisaidie, nioe ili iweje?
3. Kama mwanamke niliyempa mimba yuko tayari kuzaa, nioe ili iweje?
4. Kama kila nikihitaji tendo la ngono (sio tendo la ndoa) nalipata kwa wakati, nioe ili iweje?
5. Kama kila nikihitaji ushauri au kuliwazwa na mwanamke napata, nioe ili iweje?

Bado nipo nipo sana

Mkuu kawoli ndoa ni taasisi ambayo ni muhimu sana katika jamii na bila kwayo mambo mengi yangeyumba kwenye kiwango cha jamii kwa ujumla wake ikiwemo kuiongezea mzigo serikali. Kwa nini mtu anaoa inategemea na mtazamo, kuwa wengine anaoa kwa sababu za imani yake, kuna watu wanaoa kwa ajili tu jamii iko hivyo na kadhalika, ntajaribu kukupa sababu za jumla ambazo nahisi zitakuwa zinagusa wengi bila kujali mitazamo binafsi.

Dhamira(commitment)
Tofauti na kimada, kwenye ndoa watu wanakuwa wameungana kupitia mchakato bila mategemeo ya kuachana japo huwa yanajitokeza kwa baadhi. Ni rahisi kupanga maisha yenu ya mbeleni ikiwemo kujiendeleza kiuchumi na mke tofauti na kimada ambae mkataba wenu unaweza kuwa wa siku pekee na kesho yuko na mwingine, utamtafuta tena ukiwa na haja nae.

Mshirika wako uzeeni
Kadri umri unavyoenda ndivyo utaona umuhimu wa mshirika wako wako wa maisha, watu wengi ikiwemo vimada wako hawapendelei maisha ya kuruka miaka yote hivyo kadri siku zinavyosonga utaona wanavyopungua kutokana na kuwa na majukumu katika ndoa zao au maisha yao(hata kama ndoa haijapita).

Watoto
Japo umesema kuna mtu yuko tayari kukuzalia mtoto lakini sidhani kama utaweza kumlea kwa staili ya weekend na atakuwa mtoto mwenye malezi ya mzazi mmoja na kwa aina ya maisha yako uliyoyachagua sidhani kama utakuwa wewe, anaweza kulelewa na mama kimada ambao tunawajua staili yao ya maisha, tena usipoangalia utakuwa unashindishwa ustawi wa jamii kudaiwa fedha za mtoto, atakuwa kitega uchumi kwa mama(kimada) kuendeshea maisha yake. Maisha, malezi na tabia ya mtoto itavyokua malizia mwenyewe.

Tendo salama
Ukilinganisha maisha ya vimada na maisha ya ndoa, bado kwenye ndoa ngono ni salama zaidi na hatuwezi kuhukumu kwa baadhi ya matukio hasi yaliyopo kwenye baadhi ya ndoa kwa watu kusaliti ndoa zao. Maisha ya vimada yamejengwa juu ya dhana ya usaliti hivyo mtandao wa kusambaza magonjwa ya zinaa kwao kawaida na ngumu kutokea uaminifu baina yenu.

Faida ya kiuchumi
Wewe unakaa kwako na kimada anakaa kwake na kila mtu ana maisha yake, kila mtu anaingia gharama ambazo mngekua pamoja labda mngeweza kushea au kuziepuka. Kodi ya nyumba, gharama za take away, kuendesha uhusiano wa kimada ambao ni tofauti kidogo na mke na gharama nyingi nyinginezo. Inawezekana sana ukawa unaendesha gharama za maisha yako na kimada wako kitu ambacho ni tofauti sana ingekua mke.

Heshima na kukubalika kwenye jamii
Kadri umri unavyokatika watu wataanza kukushangaa kwanini huoi na kujituliza kwenye ndoa badala yake unaendesha maisha ya uvimada, kama una wazazi naamini utawasononesha, rika la watu wako mtaani linaweza likawa tofauti na ulilopaswa kuwepo. Maisha yenye furaha na upendo, kuwepo mtu wa kukusikiliza kila siku tofauti na kimada wa weekend, kuwepo mtu wa kutatua nae matatizo kwa hali na mali(scenario chache za watu kukimbia haziwezi kujumuisha vinginevyo) na mengineyo mengi.
 
naona unahalisha nyeupe kuwa nyekundu
maisha ya ndoa ni zaidi za kugegedana
ndio maana kwenye ndoa kuna tendo la ndoa ni sehemu ya ndoa
kuna kuumwa na kuuguzwa sitaki kuamini hiko kimada kisichokula kiapo kitadumu kwenye ups and downs
 
kawoli

1: utakuja Kuzikwa na dhambi ya uzinzi ..

2: hutapata heshima kama mwanaume alieoa anapaswa kupata .

3: Hakuna legacy yeyote utakayo acha kwa mtoto Wako kwakua hatapata mapenzi halisi ya familia
 
Last edited by a moderator:
Hela zitakapokuishia, hizo positives zako zote zitageuka negatives. ZINGATIA HILO.
 
1: utakuja Kuzikwa na dhambi ya uzinzi ..

2: hutapata heshima kama mwanaume alieoa anapaswa kupata .

3: Hakuna legacy yeyote utakayo acha kwa mtoto Wako kwakua hatapata mapenzi halisi ya familia

  • ambae hajawahi kuzini na awe wa kwanza kunyoosha kidole juu
  • Ndoa peke yake haileti heshima, heshima anapata yule ambae anasimamia maadili ya ndoa na jamii inayomzunguka. wangapi wanafanya madudu ktk jamii zao na hawaheshimiki japo wapo ktk ndoa
  • Anachohitaji mwanangu ni kutengenezewa mazingira mazuri ya ili aje aishi maisha bora
 
naona unahalisha nyeupe kuwa nyekundu
maisha ya ndoa ni zaidi za kugegedana
ndio maana kwenye ndoa kuna tendo la ndoa ni sehemu ya ndoa
kuna kuumwa na kuuguzwa sitaki kuamini hiko kimada kisichokula kiapo kitadumu kwenye ups and downs
umenena vema lakini hapo kwenye red, huwezi kuweka guarantee kwa mwanamke/binadamu as tumekuwa tukishuhudia au kusikia baadhi ya wanandoa wakiwakimbia wenzi wao kwenye matatizo sambamba na hilo
 
umenena vema lakini hapo kwenye red, huwezi kuweka guarantee kwa mwanamke/binadamu as tumekuwa tukishuhudia au kusikia baadhi ya wanandoa wakiwakimbia wenzi wao kwenye matatizo sambamba na hilo

kwa hiyo kwa kuwa baadhi ya binadamu ni wezi je watu wote ni wezi ??
usichukue udhaifu wa wachache ukawahukumu watu wote waliouguzana ni wengi kuliko waliokimbiana
muda ukifika utaoa
uzeeni kuishi peke yako haipendezi watu wange wanaoishi pamoja wanaishi kama mtu na mkewe
hiyo kampani uliyonayo sasa itafika kipindi itapotea faraja itapotea kila mtu atakua kivyake akifanya yake na familia yake
ukipata nafasi oa kijana
 
dizain kama aujiamini kuoa na bila shaka huyo mwanamke wako wote hamna malengo ya kuja kuishi kama mume na mke ndyo maana kila kitu kinaishia kwa shot time
 
Halafu Mwanamke akae tu kiuaminifu kwa mwanaume kama huyu??
Dawa yake moja tu huyu....
 
kabisa isitose co kosa lake huenda ni under 18 sooooo msameheni bure.....
Sio under 18 litakuwa lijitu lizima ila sema ubongo wake uli-stuck akiwa na miaka 10, litakuwa lijitu la 30's au 40's lakini ubongo wake unafikiri kama mtoto wa miaka 10. Mtu gani huna akili ya kufikiri wazazi wake walioana linakazaliwa lenyewe na sasa limekuwa linaogopa kuoa kubwa zima
 
Sio under 18 litakuwa lijitu lizima ila sema ubongo wake uli-stuck akiwa na miaka 10, litakuwa lijitu la 30's au 40's lakini ubongo wake unafikiri kama mtoto wa miaka 10. Mtu gani huna akili ya kufikiri wazazi wake walioana linakazaliwa lenyewe na sasa limekuwa linaogopa kuoa kubwa zima

ama ndo kukwep majuku maan wanaume wengi cku hizi hovyoo kbs
 
Halafu Mwanamke akae tu kiuaminifu kwa mwanaume kama huyu??
Dawa yake moja tu huyu....

naomba iyo dawa usiwaambie na wengine maana itakuwa balaa, iwe siri yako tafadhali
 
Back
Top Bottom