Kuoa bila sherehe, mtazamo wako.

Kuoa bila sherehe, mtazamo wako.

Wana jamvi habarini,

Nina rafiki yangu mdada, anahitaji kuolewa na mchumba wake waliokuwa nae kwa miaka miwili sasa
tatizo huyo muoaji, hataki habari za sherehe ya ndoa,
madai yake ni kupoteza muda na pia resources.
ambacho anakipinga ni kuanza kuwachangisha watu michango ya harusi
ila jamaa ni a kind of anti-social fulani
hana marafiki wengi
so nadhani anaogopa kuwa haitafanukiwa.

mimi kama rafiki, mtazamo wangu ni kwamba
sherehe sio ya muhimu saaaana kama wanapendana na kuelewana
namuunga mkono jamaa, akatoe mahali kama utaratibu then achukue mkewe kwa ndoa ya kimila au bomani.

rafiki yangu hajanielewa kwa kukubaliana na mtazamo wa mchumba wake!!!

wewe mwana MMU wasemaje?

sure kama mtu salio lake sio kubwa haina maana ya kufanya sherehe kubwa na mwisho wa siku inakuachia makovu tu.. Kwa mwanamke anaweza kuwa anapewa pressure na marafiki wenzake au hata ndugu ya kufanya sherehe kubwa but as long as kipato ni kidogo sioni mantiki ya kufanya kitu kikubwa.....
 
kuna moja ya Bro wangu tuliifungia kwenye ufukwe wa white sands , baada ya hapo ndugu, jamaa na marafiki wa karibu tukapiga party moja ya kishujaa niliipenda mno.........
haikuwa na michango wala vikao!!!!!!!!!!

Utashangaa watu tunapoteza mida kwenye viako vya harusi, maendelea inakuwa longo longo. Kwa haiyo ya kwako unatunywesha juice ya azam na ka-andazi kamoja basi! LOL
 
Mbaya zaidi huu utamu wa sherehe unawafanya mpaka wanawake wengine wanafikia hatuwa ya kuolewa na watu ambao si chaguo lao kisa tu na yeye kaolewa kwa sherehe kubwa.

Nina ushahidi wa hili, kuna mdada nilikuwa na mahusiano naye lakini nikamuona ni wa mujini sana kwahiyo sikuwa na haraka ya kupropose, basi aliponiona mikausho nikapata kasafari ka mamtoni basi wacha bana, ana Dada zake wana pesa chafu wakamshauri atafute Mwanaume yeyote amuowe wao watagharamia kila kitu, basi ndoa ikapigwa fasta.

Then when i come back Bongo nikamuuliza kwa nini umeamuwa kuolewa bila kuniomba ushauri maelezo aliyonipa ndiyo yanaendana na hii thread, then nikala mzigo kama kawa ingawa sijisikii vizuri kutembea na Mwanamke ambaye ameshaolewa, ila nilipofanikiwa kumuona Mume wake na jinsi huyu demu alivyo sister du tena kiwango, nilishangaa sana.

Hili swala la kutoa nuksi au kudhani kuoa au kuolewa ni lazima nadhani tunapaswa kulitazama upya, Mume na mke ni lazima muendane hata mtu akiwaona anapenda mlivyo, haipendezi hata kidogo eti Joti ndio awe mume wa Klyn.
 
Ni Kweli ifike mahali tuangalie upya baadhi ya mapokeo tulio nayo kwenye jammii, mimi nakubaliana na sherehe rahisi inayokubalika na wawili hao. Changamoto ni kwa wapambe na wale walio nje ambao watashinikiza sherehe. Ni tabia fulani ya ulafi (pengine) kwenye jamii nyingi, kwa mfano ni rahisi watu kukuchangia kwenye kufanikisha sherehe ya Harusi lakini siyo kwenye kufanikisha jambo la kimaendeleo kame elimu/ mtaji n.k
 
halafu utasikia
nataka sherehe ya arusi yangu izidi ya fulani
huku akitegemea michango. arghhh
 
Wana jamvi habarini,

Nina rafiki yangu mdada, anahitaji kuolewa na mchumba wake waliokuwa nae kwa miaka miwili sasa
tatizo huyo muoaji, hataki habari za sherehe ya ndoa,
madai yake ni kupoteza muda na pia resources.
ambacho anakipinga ni kuanza kuwachangisha watu michango ya harusi
ila jamaa ni a kind of anti-social fulani
hana marafiki wengi
so nadhani anaogopa kuwa haitafanukiwa.

mimi kama rafiki, mtazamo wangu ni kwamba
sherehe sio ya muhimu saaaana kama wanapendana na kuelewana
namuunga mkono jamaa, akatoe mahali kama utaratibu then achukue mkewe kwa ndoa ya kimila au bomani.

rafiki yangu hajanielewa kwa kukubaliana na mtazamo wa mchumba wake!!!

wewe mwana MMU wasemaje?

mkuu suala la ndoa ni uamuzi wenu watu wawili tu. Sorry, kumbe we unaomba mtazamo kwa niaba ya hawa watu.
Ok.
Sasa kama wao wamekubaliana haina shida na sababu alizotoa huyo jamaa ni za msingi sana kuliko kufurahisha watu na kupata maumivu yake baadae. Anaweza kuiungia kanisani kama kawaida ila awaalike watu wote wa karibu na ndugu ili ndio iwe ufahamu kwao kabisa. Mara nyingi kupunguza gharama anaweza kumuita mtu wa nyama choma hapo hapo kanisani nje watu wakala bites wakasepa shughuli imeisha. Haina gharama sana.
 
Kuna jamaa yetu alikuwa anaoa, kwenye vikao vya maandalizi kulikuwepo na jamaa mmoja mzungu, ikaonekana jamaa hana pesa kwa ajili ya gharama za Honey moon. Kikao kikapendekeza hizo gharama ziingizwe kwenye budget, yule mzungu akang'aka, no no no, kama tunamlipia na sisi tutakwenda kulala huko huko.
Hahahaaaaa... ndo dawa yao hawa omba omba, kama hauna hela unataka mambo makubwa ya nini?-
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom