Kuoa bila sherehe, mtazamo wako.

Kuoa bila sherehe, mtazamo wako.

Ambao bado hamjaoa kazi mnayo huko tuendako
yaani hii tabia yakuombwa michango inakeeera,
unakuta mtu unashindwa kufanya mambo yako ya maendeleo kisa unakadi 7 za michango wote sio chini ya 100,000 embu niambie, kwanini mtuu usijichangishe vihela vyako mwenyewe theni ndio ujipange kuoa.
kuna ndugu yangu alioa akaestimate anataka harusi yake isipungue 20milns tulikomaje? familia nzima ilibidi tupewe kiwango cha kuleta yaani nikufanywa ombaomba sasa baada ya hela kupatika jinsigani ilivyochezewa kadi moja ya mwaliko ilikuwaimegharimu 12,000 waalikwa 300 sio chakula wala kinywaji hapo hizo ni kadi tuu nikajiuliza sasahivi kuoa imekua anasa ama?
sasa hivi sichangi ambaye hajaoa wala kuolewa na anataka achangiwe imekula kwakwe.
 
sherehe sio lazima iwe kubwa saaana, waweza kuandaa hata mbuzi tu ukashirikisha na watu kadhaa wa karibu toka pande zote kwa bwn na bi arusi halafu wakakaa pamoja na kufurahi hata kwa masaa2, ingawa jamii bado haijalikubali sana hili, ila naona muda si mrefu itakuwa staili ya ndoa nyingi. natumia mawazo ya watu wanavyochangia hii hoja kufikia kusema hivyo. pia watu wengi wanachangia bila kupenda, kwa kulalamika sana, wanaogopa kuonekana vibaya kwa jamaa zao
 
hahah tu mandazi tu asakuta halafu tunapanda ka dala dala fasta kuwahi nyumbani kujipongeza! chezeaaaaa


kuna moja ya Bro wangu tuliifungia kwenye ufukwe wa white sands , baada ya hapo ndugu, jamaa na marafiki wa karibu tukapiga party moja ya kishujaa niliipenda mno.........
haikuwa na michango wala vikao!!!!!!!!!!
 
jaman nmefurahishwa sana na hii mada. me nimeoa 2011 kanisa katoliki kigambon niliamka asubuh sana me na mke wangu na wasimamizi wangu na baadh ya ndugu zangu na mke wangu hao tukamaliza mambo tukarudi nyumban nikachukua beg langu nikaenda chuo mwenzangu akaenda kwenye biashara zake.unajua tatizo ni moja unaweza shawishiwa ufanya sherehe ukaanzisha vkao kwenye kuchanga inakua issue watuu wakiona cm yako tuu wanazima au hawataki kupokea. sasa kwann uanze kununiana na rafik zako?
 
Ambao bado hamjaoa kazi mnayo huko tuendako
yaani hii tabia yakuombwa michango inakeeera,
unakuta mtu unashindwa kufanya mambo yako ya maendeleo kisa unakadi 7 za michango wote sio chini ya 100,000 embu niambie, kwanini mtuu usijichangishe vihela vyako mwenyewe theni ndio ujipange kuoa.
kuna ndugu yangu alioa akaestimate anataka harusi yake isipungue 20milns tulikomaje? familia nzima ilibidi tupewe kiwango cha kuleta yaani nikufanywa ombaomba sasa baada ya hela kupatika jinsigani ilivyochezewa kadi moja ya mwaliko ilikuwaimegharimu 12,000 waalikwa 300 sio chakula wala kinywaji hapo hizo ni kadi tuu nikajiuliza sasahivi kuoa imekua anasa ama?
sasa hivi sichangi ambaye hajaoa wala kuolewa na anataka achangiwe imekula kwakwe.


naomba nichangie mimi wa mwisho bana , memba mwenzako wa jf...........
 
Ambao bado hamjaoa kazi mnayo huko tuendako
yaani hii tabia yakuombwa michango inakeeera,
unakuta mtu unashindwa kufanya mambo yako ya maendeleo kisa unakadi 7 za michango wote sio chini ya 100,000 embu niambie, kwanini mtuu usijichangishe vihela vyako mwenyewe theni ndio ujipange kuoa.
kuna ndugu yangu alioa akaestimate anataka harusi yake isipungue 20milns tulikomaje? familia nzima ilibidi tupewe kiwango cha kuleta yaani nikufanywa ombaomba sasa baada ya hela kupatika jinsigani ilivyochezewa kadi moja ya mwaliko ilikuwaimegharimu 12,000 waalikwa 300 sio chakula wala kinywaji hapo hizo ni kadi tuu nikajiuliza sasahivi kuoa imekua anasa ama?
sasa hivi sichangi ambaye hajaoa wala kuolewa na anataka achangiwe imekula kwakwe.

Nimeipenda sana hii

michango utafikiri mtu anahamia sayari ya MARS khaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!
 
Wana jamvi habarini,

Nina rafiki yangu mdada, anahitaji kuolewa na mchumba wake waliokuwa nae kwa miaka miwili sasa
tatizo huyo muoaji, hataki habari za sherehe ya ndoa,
madai yake ni kupoteza muda na pia resources.
ambacho anakipinga ni kuanza kuwachangisha watu michango ya harusi
ila jamaa ni a kind of anti-social fulani
hana marafiki wengi
so nadhani anaogopa kuwa haitafanukiwa.

mimi kama rafiki, mtazamo wangu ni kwamba
sherehe sio ya muhimu saaaana kama wanapendana na kuelewana
namuunga mkono jamaa, akatoe mahali kama utaratibu then achukue mkewe kwa ndoa ya kimila au bomani.

rafiki yangu hajanielewa kwa kukubaliana na mtazamo wa mchumba wake!!!

wewe mwana MMU wasemaje?

Naona Asilimia zote wengi mnasema ni wastage of resources hapa jf lkn kwenye uhalisia ikoje???... msije ishia kuongea hapa na idadi ya waoaji inapungua kwa sababu hizi hizi za gharama za harusi tuanze humu kubadilika hasa akina dada huwa wanafanya kama ligi fulani kama amehudhuria kwenye harusi ya mwenzake yeye atataka sherehe ya kumzidi rafiki yake bila kujua mfuko wa mwenzake ukoje........ naunga mkono hoja....
 
Ndoa ni pembe tatu zenye MUNGU, Wana ndoa na Wazazi

Hayo yakikamilika hiyo ni ndoa tayari, Hayo Mengine hayanaga cha kuijenga ndoa husika

Maana yangu ni Sijawahi kuona ndoa iliyodumu kwa sababu sherehe ilifana sana
 
Mimi kuna mtu namfaham anapelekwa na huyo wife to be mpaka kauza shamba lake lote la zaid ya heka kumi kwa milion kadhaa ili tu harusi ifankiwe wife to be afurahi, kajichokea mwenyew kabla hata ya ndoa
Sidhan kama hii inafaa
Binafsi ni mkatoliki natarajia kufunga ndoa kanisani misa za asubuh ,tunarud nyumban tutapika maandaz special na chai baaas kila mtu kazini baadae (sijui kuhusu honeymoon labda akitaka)
 
yangu nimefunga leo bomani gharama yake hijafika elfu 35,000 mpaka sasa, nakula life,ninyi wa show off leteni mabakuli yenu tuwapige kalenda mpaka ukonde ili suti iwe gauni
 
Naunga mkono hoja mia kwa mia! ndoa co sherehe! kama huna salio bac funga ndoa sherehe baadae ukipata mafanikio katika familia yako na mkeo! mambo ya kuchangishana na kupeana lawama hayana nafasi miaka hii bana! me binafsi nimefulia na taratibu za kufunga ndoa bila sherehe za kuchangisha marafiki zimesha kamilika hivyo mwez wa kwanza tunachoma ubani na maisha yanasonga!
 
kuna michango mizuri huku mm wife nlimwambia ndoa historia waambie wazazi wataje mahari wakizingua ntawazingua zaidi yao....alipopeleka taarifa akaambiwa mmependana hayo yenu mahari ni kadhaa....ndio mchezo ulivyoisha...namshukuru Mungu amenipa prudent wife..hakuna mbwembwe za kishambashamba
 
Kuoa uoe wewe, mie nitoe hela ili ufanye sherehe! Ili iweje, je mke ni wa kwako ama wa kwetu?

Kuna jamaa yetu alikuwa anaoa, kwenye vikao vya maandalizi kulikuwepo na jamaa mmoja mzungu, ikaonekana jamaa hana pesa kwa ajili ya gharama za Honey moon. Kikao kikapendekeza hizo gharama ziingizwe kwenye budget, yule mzungu akang'aka, no no no, kama tunamlipia na sisi tutakwenda kulala huko huko.
 
Wana jamvi habarini,

Nina rafiki yangu mdada, anahitaji kuolewa na mchumba wake waliokuwa nae kwa miaka miwili sasa
tatizo huyo muoaji, hataki habari za sherehe ya ndoa,
madai yake ni kupoteza muda na pia resources.
ambacho anakipinga ni kuanza kuwachangisha watu michango ya harusi
ila jamaa ni a kind of anti-social fulani
hana marafiki wengi
so nadhani anaogopa kuwa haitafanukiwa.

mimi kama rafiki, mtazamo wangu ni kwamba
sherehe sio ya muhimu saaaana kama wanapendana na kuelewana
namuunga mkono jamaa, akatoe mahali kama utaratibu then achukue mkewe kwa ndoa ya kimila au bomani.

rafiki yangu hajanielewa kwa kukubaliana na mtazamo wa mchumba wake!!!

wewe mwana MMU wasemaje?

Mimi nilioa bila sherehe miaka takriban kumi na mbili iliyopita na sababu kubwa ni kuwa sikutaka kutembeza bakuli kwa ndugu jamaa na marafiki ili nifanye sherehe ambayo sikuwa uwezo nayo. Nilikuwa na ndugu, jamaa na marafiki ambao wangeweza kabisa kuichangia gharama za sherehe lakini niliamua kuwa sitawaomba pesa yao. Sikuwa naamini kuwa ni sahihi kuingia kwenye gharama za sherehe ya muda mfupi ambayo mimi binafsi sikuwa na uwezo wa kuikabili isipokuwa kwa kuzungusha bakuli. I do hate begging!!! Bahati nzuri mtani wa jadi alinielewa na wazazi wa pande zote mbili walielewa somo na mpaka leo tunaendeleza libeneke mama kawaida.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom