life is Short
JF-Expert Member
- Apr 1, 2013
- 4,741
- 3,037
Kwani Estimation ni ngapi?
yani me nishatoa tangazo la la siku 21 pale bomani ,bado siku nane..naenda kufunga ndoa kimya kimya na mashahidi ...naenda kwetu kwa wazaz wangu,tunapata chakula na wakwe na rafiki zetu wachache...siku inayofuata me na wife zenjiiiiii...tukirudi likizo ya week 2 zimeisha mke job me job...kwisha habari yake....life goos on!,
nakuelewa unachosema n i agree,mi nilichokua nasema wafanye sherehe kwa uwezo wao kama wana hela ndogo wawe wabunifu sherehe ndogo ila nzuri au kama dada aana uwezo, ila wasiache kufanya shereheSi kila mtazamo unaokuwa nao ni sahihi kuutumia, unaweza ukawa na mtazamo ambao si mbaya ukiutekeleza lakini hapohapo uwezo wa kuutekeleza hauna. Watu wengi michango ya harusi huwa hawatoi kwa moyo mmoja kuwa kwamba tunamchangia ndugu/jirani/rafiki/jamaa yetu ili afanye sherehe baada ya ndoa. Wengi huchangia kuondoa lawama kuwa nitaonekanaje nisipomchangia jamaa.
Na huku wafunga ndoa wengine hugeuza mchango kama deni na kero, mtu unakuta amekupatia kadi kwenye kukumbushia mchango anakutumia texts za kukukumbushia mchango mara 3 kwa siku zote zikidai mchango. Wengine hufikia hata kukulaumu na kukusema vibaya kisa tuu hujachangia harusi yake.
Mtu unakuta ana plan ya kufunga harusi ya million 15, lakini yeye yupo tayari kuchangia pesa isiyozidi laki 5 ili kufanikisha na kutegemea michango kiasi kilichobaki. Sidhani kama hili ni sahihi.
Naunga mkono, sherehe ni kupoteza muda wakati ndoa ni between the 2.
Mfanyakzi wa halmashauri wa mji flani alioa around 43 age mchango wa harussi alipata more than 69milioni kamati ilimpa 30milioni cash,na tena mfanyakazi mwingine akaozesha binti yake kwenye ofice hiyo2 akapata mchango wa more than 95miloni yule binti alipewa kazawadi ka gari ya 15m
ofisi gani hiyo mkuu ? tukachangishe na sisi hiyo michango tupige bingo hapa mjini.
Mimi ukishanivisha pete nikasaini na kale kacheti ka ndoa baaaaaas! Sherehe tupa kuleeee!!
Mi nilioa bila sherehe na mwaka wa tatu huu sasa nadunda na wife. Watu wanataka makubwa kwa kutegemea KUKAMUA watu. Pesa nyingi hupotea kwenye sherehe alafu maharusi wanasuffer baada ya ndoa.
Mi nilioa bila sherehe na mwaka wa tatu huu sasa nadunda na wife. Watu wanataka makubwa kwa kutegemea KUKAMUA watu. Pesa nyingi hupotea kwenye sherehe alafu maharusi wanasuffer baada ya ndoa.
bestiiiiiiiii!!!!!!!!!!!!! nitakuwowa bila sherehe ya harusi.................