Kuoa bila sherehe, mtazamo wako.

Kuoa bila sherehe, mtazamo wako.

Snowball umezungumza vyema
ni kautamaduni ambako hakafai
na kanadhalilisha sana
mtu anapanga kuoa kwa bajeti ya kuchangisha watu!!
ili tuu aonekane duniani ameoa!!!
i hate michango ya harusi
Bora tuanze kuchangia elimu kwa wasiojiweza.

Binafsi sikubaliani na dhana ya kuchangishana fedha kwa ajili ya harusi..na kama tusipolisemea hili sasa...kesho tu watu watakuja kuomba wachangiwe na mahari kabisa...Tatizo kubwa letu watz ni kuwa huwa tunapenda sana show offs...kusema ni rahisi but kutekeleza naona ndio mzigo....tubadilike bana!...i wish ningekuwa kijana nionyeshe mfano....
 
Mshauri hivi, afanye bonge la send-off la kufa mtu yeye mwenyewe maana send-off iko upande wake huyo rafiki yako. Kwa upande wa huyo mumewe mtarajiwa, amruhusu ajifanyie kisherehe kilicho ndani ya uwezo wake. Sioni mantiki ya kumlazimisha mtu kufanya misherehe mikubwa wakati hana uwezo au kama ulivyosema ni anti-social, atachangiwa na nani? Au ndo yale mnamaliza kufunga ndoa mnaishia kulipa madeni?

kweli kabisa mkuu
nimemwambia hivyo pia
kama ni sherehe basi amalizie hasira zake kwa end off
ila wadada wa mjini wana kazi jamani!!
 
pole yao! wafanye sherehe inayomatch uwezo wao, sherehe kupendeza siyo ukubwa au gharama mnayotumia rather ubunifu na kinacho matter mwisho wa siku ni nyie wenyewe mme enjoy kias gani, au kama dada ana uwezo wagawane gharama za harusi, ila huyo kaka asimnyime dada wa watu sherehe.... jaman wafanye ya gharama ndogo as I said, ni dream ya most women kuwa na harusi nzuri, SO SHE SHOULD NOT BE DENIED THAT.
 
Unanifaa sana wewe, hasara za kuwajaza watu waje kula na kunywa ni heri hiyo pesa nikutwange na ka GX 110.
kuna harusi nilihudhuria ambayo gharama yake ilikuwa Tsh. 25mil lakini kiukweli ilikuwa haifanani na gharama hizo which means baadhi ya wajumbe wa kamati walichakachua michango.....
 
Kweli mkuu..ni kutiana umaskini tu!

Snowball umezungumza vyema
ni kautamaduni ambako hakafai
na kanadhalilisha sana
mtu anapanga kuoa kwa bajeti ya kuchangisha watu!!
ili tuu aonekane duniani ameoa!!!
i hate michango ya harusi
Bora tuanze kuchangia elimu kwa wasiojiweza.
 
what an idea,atafute uwazi mzuri,eg butani iliyopangika vzuri,anakodisha viti na mapambo machache aite wanafamilia within thirty minutes tayari husband and wife na sherehe imeisha,cost very low.
 
Mfanyakzi wa halmashauri wa mji flani alioa around 43 age mchango wa harussi alipata more than 69milioni kamati ilimpa 30milioni cash,na tena mfanyakazi mwingine akaozesha binti yake kwenye ofice hiyo2 akapata mchango wa more than 95miloni yule binti alipewa kazawadi ka gari ya 15m
 
pole yao! wafanye sherehe inayomatch uwezo wao, sherehe kupendeza siyo ukubwa au gharama mnayotumia rather ubunifu na kinacho matter mwisho wa siku ni nyie wenyewe mme enjoy kias gani, au kama dada ana uwezo wagawane gharama za harusi, ila huyo kaka asimnyime dada wa watu sherehe.... jaman wafanye ya gharama ndogo as I said, ni dream ya most women kuwa na harusi nzuri, SO SHE SHOULD NOT BE DENIED THAT.

Kwani kusipokuwa na sherehe baada ya ndoa haitokuwa harusi nzuri.?
 
nipo na jamaa yangu hapa, yeye aliamua kutofanya sherehe kabisa, kilichotokea upande wa mwanamke wamevunja send off, na ile 12m walioikusanya kwa ajili ya send off itumike kwenye harusi, basi jamaa yupo hapa hajielewi elewi!
 
Hata mie naenda kufunga kesho. Nitakuwa mimi na wasimazi tu baada ya hapo tutarudi nyumbani kuendelea na shughuli zetu za kawaida.
 
nipo na jamaa yangu hapa, yeye aliamua kutofanya sherehe kabisa, kilichotokea upande wa mwanamke wamevunja send off, na ile 12m walioikusanya kwa ajili ya send off itumike kwenye harusi, basi jamaa yupo hapa hajielewi elewi!

Upande wa mwanamke wamevunja sendoff kwa sababu gani.?
 
Maisha yashapinda kitambo, wengine unao kwa sherehe kuuubwa wakati bado unaishi nyumba ya kupanga ,
Tunapotezeana muda na resouces kama huamini kaa chini fanya CBA ( COST BENEFIT ANALYSIS) kisha utapata jawabu.
 
kama mtu ana mtazamo/anaamini kuwa lazima sherehe iwepo then haitakua nzuri definetly!

Si kila mtazamo unaokuwa nao ni sahihi kuutumia, unaweza ukawa na mtazamo ambao si mbaya ukiutekeleza lakini hapohapo uwezo wa kuutekeleza hauna. Watu wengi michango ya harusi huwa hawatoi kwa moyo mmoja kuwa kwamba tunamchangia ndugu/jirani/rafiki/jamaa yetu ili afanye sherehe baada ya ndoa. Wengi huchangia kuondoa lawama kuwa nitaonekanaje nisipomchangia jamaa.

Na huku wafunga ndoa wengine hugeuza mchango kama deni na kero, mtu unakuta amekupatia kadi kwenye kukumbushia mchango anakutumia texts za kukukumbushia mchango mara 3 kwa siku zote zikidai mchango. Wengine hufikia hata kukulaumu na kukusema vibaya kisa tuu hujachangia harusi yake.

Mtu unakuta ana plan ya kufunga harusi ya million 15, lakini yeye yupo tayari kuchangia pesa isiyozidi laki 5 ili kufanikisha na kutegemea michango kiasi kilichobaki. Sidhani kama hili ni sahihi.
 
Upande wa mwanamke wamevunja sendoff kwa sababu gani.?


tumebaki na maswali yasiyokuwa na majibu, ila ni kwamba huyo binti mtarajiwa ndo kaamua iwe hivyo, yaani badala ya kusanya sedoff yeye kaamua hiyo pesa itumike kwa ajili ya harusi, sasa upande wa mwanaume haukujiandaa na hilo, na upande wa mke unauliza pesa ya upande wa muoaji, ili ijumlishwe, na harusi ni wiki mbili zijazo
 
Suala sio kuwa social au anti-social suala ni resource, nilifunga ndoa na kulikua na sherehe lakini maumivu yanayobaki baada ya hapo ni mimi ninayejua. sema niliona mke wambae sio complicated, sasa imebaki story. Kuna kipindi wakati niko chuo pale Mlimani niliona watu siku ya jumatano I think walienda pale CCT kanisani wakafungishwa ndoa wakaondoka zao na mashahidi wao, mwengine ni classmate wangu,alifunga kimya kimya alipomaliza ndugu yake akawachukua wakaenda baharini wakatafuta mahali wakala wakanywa kiasi hao nduki...life goes on
Hii ndiyo staili ya kisasa hata ulaya. Unakwenda kwa City mayor... mnafunga ndoa.... unatoka nje ya ukumbi... mnapiga picha mnakunywa vinywaji (cock tail)..... marafiki wanatoa zawadi ... mnatawanyika, maharusi wanakwenda honeymoon. Suala hapa si kuokoa resources in terms of money tu, bali in terms of time pia. Sherehe kubwa na mbwembwe siyo guarantee kwamba ndoa yenu itadumu. Tuzinduke.
 
tumebaki na maswali yasiyokuwa na majibu, ila ni kwamba huyo binti mtarajiwa ndo kaamua iwe hivyo, yaani badala ya kusanya sedoff yeye kaamua hiyo pesa itumike kwa ajili ya harusi, sasa upande wa mwanaume haukujiandaa na hilo, na upande wa mke unauliza pesa ya upande wa muoaji, ili ijumlishwe, na harusi ni wiki mbili zijazo

Hahahaa......! Hapo majanga, jamaa angewaeleza ya kuwa hayupo tayari kufanya sherehe kubwa baada ya ndoa, fullstop. Maana hapo inaonekana upande wa mwanamke wanachukulia ya kuwa jamaa hataki sherehe basi itakuwa tatizo la pesa. Mshaurini jamaa ya kuwa kama suala la kutokuwa na sherehe ameridhia toka moyoni aende ukweni akawaambie kuwa hayupo tayari na harusi. Wao kama wanataka kumuona binti yao anaagwa wamuandalie sendoff kama walivyopanga. Na ndoa iwe simple kama walivyopanga.

Though nashindwa kuelewa imekuwaje mpaka dakika za mwisho mambo haya yanaibuka. Inamaana hakukaa na mwenza wake wakakubaliana juu ya plan zake.? Maana hapo kinachoonekana ni kukosekana kwa taarifa baina ya waolewa na muoaji.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom