Kunyonyesha mtoto

Kunyonyesha mtoto

ngoja niihifadhi, itanifaa nikianza kunyonyesha. senkyu lizzy.
 
miezi 6 maziwa ya mama tu...hayatoshi!!!

yanatosha sana, mie dadangu wanae wote wanne wamenyonya 6 months bila kulishwa chakula kingine na walikuwa na afya na uzito mzuri tu
 
Yanatosha kwa wanaokaa nyumbani..
Lakini kwa wafanyakazi wengi hiyo ni ngumu...
Maana production ya maziwa inategemea pia na frequency ya unyonyeshaji...

Labda ndio maana nchi nyingi za ulimwengu wa kwanza likizo ya uzazi ni miezi 6...
(japo wanawake huko hawapendi kunyonyesha muda mrefu; na si issue kwao maana maziwa ya kopo kwa ni safe as maji yao ni safe, na vyakula vinapimwa ubora...si huku mchina; issue ya maziwa ya kopo kuwa si mazuri inalennga nchi masikini sababu ya hygiene na umasikini)

yanatosha sana, mie dadangu wanae wote wanne wamenyonya 6 months bila kulishwa chakula kingine na walikuwa na afya na uzito mzuri tu
 
yanatosha sana, mie dadangu wanae wote wanne wamenyonya 6 months bila kulishwa chakula kingine na walikuwa na afya na uzito mzuri tu

kuna wengine wakifika miezi 3 au4 huwa wanalia sana kama anapewa maziwa pekeee ndo mana naonaga wengi wanaanzishiwa uji mwepesi uliochujwa
 
Mimi kwa kweli mke wangu nampa bonasi ya 30,000/= kila mwezi kwa kumngonyesha mwanangu. Pia kifurushi cha muda wa maongezi cha cha 2,000.00 tigo kila wiki kama motisha amnyonyeshe mwanangu. Na bahati nzuri mwanangu anafahamu kama anaponyonya kua motisha kwa hiyo ye ni kunyonya mwanzo mwisho. Mama yake naye kwa kutambua hilo anajitabidi kula vizuri kwa ajili yake na mwanetu.
 
Hahahaa eti utakamua nini.
Maziwa yapo bana, ni kiasi cha kula na kunywa vizuri. Alafu huonagi wengine wanaenda kazini blouse zinalowa maziwa wakati mtoto hapati, siyakamuliwe hayo ili hata mama nae awe confortable?!

Mtama kwa watoto hongera mwaya. Watoto wa kiume wanakamua haswa, wangu kafikisha miaka miwili ila ndo kwanza utamu wa nyonyo umekolea vizuri. Siwezi ku-imagine wangekuwa wawiwili.

Anyway, uzito gani umekataa kuondoka?! Wa mwili?! Kama ndo huo na umeshaacha kunyonyesha anza kupunguza chakula unachokula taratibu na mazoezi kidogo hata ya kutembea tu utapungua.

Nimewachisha Miaka miwili lakini ilikua shida duh, wanavuta nyonyo Mpaka unasikia kama mtu anakomba sufuria, mie nilikua sikamui nikawachiaa wananyonya asubuhi na nivile wawili wana maliza Saa 6 wanaletwa kazini kunyonya Mimi Saa 9 nakua home....
 
Last edited by a moderator:
Nimeona niandike hii makala baada ya kushuhudia watoto kadha wa kadha wakidhoofika kwa kulazimishwa kula vitu ambavyo umri wao hauruhusu. Wako ambao miili yao inakuwa sawasawa au hata zaidi (overweight) ila bado hawaendelei vizuri kwenye mambo mengine mf. Kuwa wazito kutembea, kuongea, kufikiri n.k.

Kabla ya kwenda mbali, tukumbushane kwamba faida za kumnyonyesha mtoto kwa miezi sita bila kumpa chochote na kuendelea kumyonyesha kidogo kidogo hata baada ya hapo ni nyingi na ni muhimu sana kwa afya ya mtoto. Baadhi ni....
1. Kumsaidia mtoto kuepuka magonjwa, mtoto haugui hovyo.
2. Inampa mtoto nafasi kubwa kuepuka kuwa na mizio (allergies) kuliko anaepewa maziwa.
3. Maziwa ya mama yanaongeza ufahamu wa mtoto.
4.Ukaribu kati ya mama na mtoto unaongezeka na hiyo 'bond' inamsaidia mtoto kukua vizuri kwa furaha.
5. Speed ya ukuaji wa mtoto kiakili, kimwili, kisaikolojia na kihisia inakuwa juu. N.k

PS.
KWA WAMAMA, KUNYONYESHA EXCLUSIVELY KWA MIEZI 6 NI NJIA NZURI SANA YA UZAZI WA MPANGO. Wengine hata period wanasahau kwa zaidi ya mwaka mmoja (hii nimeifaidi..lol)

Tukirudi kwenye mada, wadada/wamama wengine huwa wanawalazimisha watoto kunywa uji/mtori/mziwa ya ng'ombe kwa kutopenda kunyonyesha, kudai hawana maziwa ya kutosha na kuwa busy na kazi kwa wale walioajiriwa ama kujiajiri.
1. Wasiopenda kunyonyesha.
..Huo ni ubinafsi uliotukuka.
Ikiwa hauko tayari kumtimizia mtoto mahitaji yake ya msingi kwanini ubebe mimba?! Kula ujana ukimaliza ndio uzae. Kwanza unataka manyonyo yakae juu juu maisha yako yote yamekuwa mawingu?!-😉
2.Wanaoamini hawana maziwa ya kutosha/mepesi kwasababu mtoto ananyonya non-stop bila kuonyesha dalili ya kushiba Nakushauri KULA VIZURI.

Nna rafiki yangu ana mtoto wa miezi minne tu na ana kilo 5,kadogoooo lakini anakunywa uji na maziwa huku maziwa ya mama yakiwa kama nyongeza tu kwa kisingizio cha "hashibi". Ila kwa kushinda na rafiki yangu niligundua tatizo lake, anaweza kunywa chai asubuhi na asile tena mpaka saa tisa mchana. Kwa maana hiyo mtoto ananyonya breakfast (Kipande cha mkate labda na mayai mawili) kwa masaa zaidi ya sita. Baada ya hapo anaweza akakaa tena mpaka saa mbili/tatu ndo ale tena. Hapo kitatoka kitu cha maana kweli?! Obviously not. Na sio yeye tu, kuna binti jirani yetu mtoto wangu na wake walipishana wiki tu kuzaliwa lakini kwenye ukuaji wamepishana kama vile wamezidiana mwaka mzima.

Binafsi siamini kwenye kula sana na kula vyakula vyenye mafuta mengi wakati wa uzazi. Na ile imani ya kwamba ugali,wali,maharage,cabbage,dagaa na vyakula vingine kama hivyo sio chakula cha mzazi sio kweli. Kila kitu kinalika na kila kimoja kina faida yake.

Ujanja ni kula portion ndogo ndogo kila baada ya masaa machache. Mf. Saa 1 CHAI na mayai mawili au na vipande viwili vya mkate, saa 3-4 kabakuli kadogo ka uji, saa 6 supu kidogo, saa 8 lunch (wali, ugali,ndizi,viazi, spaghetti, chapati za maji n.k), saa 11 matunda yoyote yale yanayopatikana kwa kipindi hicho au salad, saa 2 chakula cha usiku alafu basi. Katikati ya usiku ukisikia njaa kunywa chai/kikombe cha maziwa au juice labda na kipande cha mkate. Hapo hata ukimaliza uzazi hutoki umenenepa kama tembo na mtoto atakuwa mwenye afya tele.
3. Waajiriwa/waliojiajiri.
Mkamulie mtoto maziwa yahifadhiwe ili apewe kwa muda ule ambao haupo. Maziwa ya mama yanaweza kuhifadhiwa kwenye friji na mtoto akapashiwa kidogo muda wake wa kula ukifika. Pia, panga ratiba zako vizuri, kama uwezekano wa kurudi nyumbani mchana upo basi rudi unyonyeshe pia kuhakikisha mtoto wako yuko salama.

Kwa kuongezea tu, Maziwa ya ng'ombe ni mazuri kwa afya lakini sio kwa mtoto chini ya mwaka mmoja. Na sababu ni kwamba yana protein na madini zaidi ya ambavyo mwili wa mtoto mchanga unavyoweza kusaga. Pia minerals na vitamin zilizopo kwenye maziwa ya ng'ombe sio kiasi kile ambacho mtoto anahitaji. Ndo unakuta mtoto anakuwa na upungufu wa madini ya chuma ambayo inaweza kupelekea mtoto kupata anemia which is serious.

So, kuweni wazazi wazuri, kuleni vizuri (vyakula, matunda na mboga za kila aina) mnyonyeshe. Wababa wasaidieni wake/wazazi wenzeni kutimiza wajibu huu kwa kuwajali muwafaidishe watoto wenu.

Kwa kuongezea tuu kunyonyesha kunasaidia pia kupunguza uzito kwa Mama, kupunguza risks za kupata Cancer na magonjwa ya Moyo . Thanks!
 
bora uwakumbushe maana siku hizi wanajifanya usasa umewatawala,hawanyonyeshi tena,wanaogopa ziwa kulala wakati liliwekwa kwa matumizi ya mtoto na sio baba(baba wanadandia tu chakula cha watoto)

Alafu wanakuaga wanaboa ukiwaambia wanajidai vichwa vigumu eti dokta kasema tuanze kumnywesha uji apate nguvu, uji mtoto wa miezi minne akili ya wapi hiyo 😬😐😐😐😡😡😡😡😡
 
Yanatosha kwa wanaokaa nyumbani..
Lakini kwa wafanyakazi wengi hiyo ni ngumu...
Maana production ya maziwa inategemea pia na frequency ya unyonyeshaji...

Labda ndio maana nchi nyingi za ulimwengu wa kwanza likizo ya uzazi ni miezi 6...
(japo wanawake huko hawapendi kunyonyesha muda mrefu; na si issue kwao maana maziwa ya kopo kwa ni safe as maji yao ni safe, na vyakula vinapimwa ubora...si huku mchina; issue ya maziwa ya kopo kuwa si mazuri inalennga nchi masikini sababu ya hygiene na umasikini)

sio mama wa nyumbani, ni mfanyakazi na alimanage
 
Honestly Mimi nilinyonyesha mpaka mwanangu aliacha mwenyewe. Na nilikuwa nafanya kazi na kwenda shule full time . Nikiwa kazini au shule , huwa napump usiku wake kabla sijalala na kuyaweka kwenye fridge. Asubuhi nikimdrop mwa mwanangu kwa sitter nadrop na maziwa yake niliyokaamua ,ilienda hivi kwa muda . My dear inahitaji moyo, willing na commitment kunyonyesha. Kazini tunawashauri sana sana breastfeeding kwa Mtoto angalau miezi sita ya mwanzo., ili Mtoto asipate na allergies, or maradhi mengineyo kwa kuwa immune system zao haziko strong ,so breastfeeding inawasaidia sana sana watoto wetu ,. Jamani tukishakuwa wamama inabidi tuu tujisahau kuhusu wenyewe na kuwaza benefits za watoto wetu. Sisemi usijutuze hapana , kwa wale mnaohofia miili yetu mbona breastfeeding inasaidia kupunguza ,na hata gym pia mbona ziko za kumwaga tuu ni kuweka muda Wa kwenda huko na kututumka. Inauma , kuna wazazi kibao wanaokuja kazini kwangu nikiwauliza unanyinyesha anasema hapana kisa hataki maziwa yake yaanguke sasa najiuliza walizalia nini kama Bado usichana haujaisha. Au analalamika eti maziwa hayatoshi ,na akipewa suggestion ya food nutrition za kutumia ili apate lishe ya mtoto anakuambia vitamfanya anenepe, kazi Kweli Kweli Mungu atusaidie tuu . Thanks.
 
Kama kawaida yangu naangalia kitu kwa jicho la tatu...
Muwe mnapima afya zenu mara kwa mara...
Maana ung'ang'anie kunyonyesha huku mumeo mzinzi mtoto apate maambukizi toka kwa mama...

Na ukiona mtu hataki kunyonyesha mtoto wake mumuwache...
Wengine wameathirika...kuuliza uliza na kuwashangaa shangaa kunawafanya wajisikie vibaya...
Haya mambo ni very private...

Kuna rafiki yangu huko Mghana...alijifungua kipindi huko kwao kuna kampeni ya mama kunyonyesha mtoto...
Anasimulia ilikuwa worst experience kwake...
Alikuwa analetewa mtoto amnyonyeshe huku maziwa yana vidonda (alilazwa baada ya kujifungua)...sikilizia maumivu yake na usalama wa afya ya mtoto...

Mwili wangu...mtoto wangu...nani aniamulie...

Kwa ufahamu mdogo nilionao ni kwamba mama hata kama ameathirika ananyonyesha miezi sita ya kwanza ila kwake yeye agizo la kutompa kitu kingine chochote linatakiwa lizingatiwe sana.....mama akizingatia hili huku anaendelea na dawa mtoto anakuwa salama kabisa
 
Kwa ufahamu mdogo nilionao ni kwamba mama hata kama ameathirika ananyonyesha miezi sita ya kwanza ila kwake yeye agizo la kutompa kitu kingine chochote linatakiwa lizingatiwe sana.....mama akizingatia hili huku anaendelea na dawa mtoto anakuwa salama kabisa

Hii ni very rare kushauriwa kufanya hivi . kwa maana wengine wanaweza kujisahau kufuata masharti matokeo yake Mtoto ndio anakuwa victim . Kuna dawa/ kinga Yes wamama wanapata ili waweze kuwanyonyesha watoto kwa muda Fulani. Ila inategemea na muathirika yuko katika stage gani, mashambulizi yako too strong or. So kuna precautions za kuchukua pamoja na vipimo zaidi. Ila for sure doctors wengi wanajitahidi sana sana kusave maisha akiwa tumboni asipate maradhi kama Mama, kwa kutumia dawa na masharti ,wengi wao wana succeed hilo lengo kutimia . Thanks.
 
Hii ni very rare kushauriwa kufanya hivi . kwa maana wengine wanaweza kujisahau kufuata masharti matokeo yake Mtoto ndio anakuwa victim . Kuna dawa/ kinga Yes wamama wanapata ili waweze kuwanyonyesha watoto kwa muda Fulani. Ila inategemea na muathirika yuko katika stage gani, mashambulizi yako too strong or. So kuna precautions za kuchukua pamoja na vipimo zaidi. Ila for sure doctors wengi wanajitahidi sana sana kusave maisha akiwa tumboni asipate maradhi kama Mama, kwa kutumia dawa na masharti ,wengi wao wana succeed hilo lengo kutimia . Thanks.

Mmmmh suala la kuvunja masharti ni uzembe wake yeye mama. Ila kama mama ana hali nzuri anashauriwa kunyonyesha. Nimekaa PMTCT kwa miezi miwili na nimeona kabisa wamama wanaonyonyesha na watoto wana afya nzuri kabisa
 
Nauliza tu koh koh koh mtoto anakaaje 6mnths bila kunywa maji? baby wangu nmekaa nae wiki 2 akaanza kutoka mate mazito afu mengi, anasweat sana na lips zake znakauka mi nkahisi ana kiu ikabidi nianze kumpa maji kijiko kidogo 1, mate yakaisha na lipsi hazijakauka tena!!!
 
Mmmmh suala la kuvunja masharti ni uzembe wake yeye mama. Ila kama mama ana hali nzuri anashauriwa kunyonyesha. Nimekaa PMTCT kwa miezi miwili na nimeona kabisa wamama wanaonyonyesha na watoto wana afya nzuri kabisa

Ni Kweli kwa masharti kuzingatiwa, my dear sio Wa Mama wote ni wazembe wengine hujisahau kwa schedules especially nnchi za nnje , na ndio wanaafya Wa hapa tunawaeleza kabisa benefits na risks kama wakifuata masharti na wasipofuata masharti, in that case wengi wao hawataki kuweka Mtoto kwenye risks na kuwa victim so wanaamua kutofanya hivyo . Nnchi nyingi za nnje mtoto huwa anawekwa wa kwanza na sio wa mama . Na ndio maana hata kwenye kujifungua tuko tayari kusave maisha ya mtoto kwanza ya mama ndio yanafuata .Thanks.
 
Back
Top Bottom