Kunatokota sana huku mtaani

Kunatokota sana huku mtaani

JF

Sijui kuhusu mitaa yenu, ila mitaa mingi nliyopita kunatokota sana. Watu wana machungu na hasira sana.

Kama wanadhani watu wameanza kusahau, wajue ardhi bado ni ya moto sana.

Haki huinua taifa.
Haya matokeo yameonyesha kuna uzuzu wa kufikiri wa hali ya juu mno kwa viongozi wa Tanzania, ni nani anaweza kupata 98% ! Hata Mwenyezi Mungu akipigiwa kura, kuna binadamu watamkataa tu......Kwanza waliojitokeza walikuwa wachache kushinda chaguzi nyingi zilizopita. Akili za kawaida tu hata wangetaka kuzipika wengeweka hata angalau range ya 69% to 82%. Wengine wanasema Mama aligoma kabisa kupata chini ya 98%! Alitaka awe juu kuliko viongozi wote waliomtangulia! The highest form of inferiority complex.

Katika mengi ambayo nimejifunza katika Uchaguzi huu, ni kuwa uwezo wa viongozi wa CCM kufikiri, kuisoma jamii uko nyuma mno! Kwa wao (wana CCM) Tanzania badi iko miaka 70! Utategemea nini kama kina Mzee Wasira ndio ndio wapanga mikakati (strategist) wa CCM! Namshangaa sana hata Kikwete ambaye anaonekana anazijua siasa za ndani, kweli amekuwa kipofu na kushindwa kuiona jamii inabadilika.

Matokeo haya yametufanya Watanzania kuwa vituko mno! Hata kama Mama kama atakuwa na roho ya paka na kuendelea kutawala, brand yake imeshuka mno! Na bahati mbaya mno media za nje zimelibebea bango, sioni kama tutakuwa na Waziri wa Mambo ya nje wa kuweza kumuosha Mh Samia, huyu Thabit Kombo ni mtupu mno kuwa Waziri wa Mambo ya Nje.......Maana mojawapo ya kazi kubwa sasa hivi katika serikali itakayoundwa ni kujaribu Kumsafisha Samia na Tanzania kwa Ujumla!

Ukweli ni kwamba damu iliyomwagika itakuwa ngumu mno kusafishika, na hizi kesi za uhaini ndio zinaifanya serikali ya Tanzania kuonekana kituko mbele ya kadamnasi ya Kitaifa!
 

Attachments

  • Screenshot_20251024_134912_Chrome.jpg
    Screenshot_20251024_134912_Chrome.jpg
    26.5 KB · Views: 13
Nyie roho waovu roho wachafu mapepo watoto wa shetani wafu mnaotembea (stakehigh King Nkondo Lucha Abou Shaymaa etc) mnaofurahia mauaji kwakuwa mali zenu ziliibiwa / haribiwa:

1. Huyu mtoto aliwaibia nini? Aliwachomea nini? Mna uthibitisho kuonyesha ni yeye aliwaharibia?





2. Huyu dada / mama je? Uthibitisho mnao?




3. Kwenye huu umati uliofyatuliwa risasi mwizi ni yupi, mchomaji ni yupi, muandamaji wa amani ni yupi, mpita njia ni yupi? Uthibitisho unao?




4) Tukichanga, tukauza mali zetu na kuomba misaada nje tuwarudishie mali zenu, kwenye maelfu mlioua mtafufua wangapi?
 
Nyie roho waovu roho wachafu mapepo watoto wa shetani wafu mnaotembea (stakehigh King Nkondo Lucha Abou Shaymaa etc) mnaofurahia mauaji kwakuwa mali zenu ziliibiwa / haribiwa:

1. Huyu mtoto aliwaibia nini? Aliwachomea nini? Mna uthibitisho kuonyesha ni yeye aliwaharibia?


View attachment 3499420


2. Huyu dada / mama je? Uthibitisho mnao?

View attachment 3499423


3. Kwenye huu umati uliofyatuliwa risasi mwizi ni yupi, mchomaji ni yupi, muandamaji wa amani ni yupi? Uthibitisho unao?


View attachment 3499427

4) Tukichanga, tukauza mali zetu na kuomba misaada nje tuwarudishie mali zenu, kwenye maelfu mlioua mtafufua wangapi?
Im sorry for kid and the lady viashiria vya fujo vilifanywa na waharifu wachache wapuuzi vimegharimu maisha ya innocent wengi like the kid and girl, Mungu awalaze pema peponi.
 
Nyie roho waovu roho wachafu mapepo watoto wa shetani wafu mnaotembea (stakehigh King Nkondo Lucha Abou Shaymaa etc) mnaofurahia mauaji kwakuwa mali zenu ziliibiwa / haribiwa:

1. Huyu mtoto aliwaibia nini? Aliwachomea nini? Mna uthibitisho kuonyesha ni yeye aliwaharibia?


View attachment 3499420


2. Huyu dada / mama je? Uthibitisho mnao?

View attachment 3499423


3. Kwenye huu umati uliofyatuliwa risasi mwizi ni yupi, mchomaji ni yupi, muandamaji wa amani ni yupi? Uthibitisho unao?


View attachment 3499427

4) Tukichanga, tukauza mali zetu na kuomba misaada nje tuwarudishie mali zenu, kwenye maelfu mlioua mtafufua wangapi?
wakati tunahamisha amani wewe uliona vurugu ndo znafaaa
 
Im sorry for kid and the lady viashiria vya fujo vilifanywa na waharifu wachache wapuuzi vimegharimu maisha ya innocent wengi like the kid and girl, Mungu awalaze pema peponi.
mngekua wise haya yote yasingetokea, si far Sir God atahukumu chanzo cha kifo
 
Maisha ya binadamu hayawezi kulinganishwa na mali au biashara yeyote.
Leo mtaani kwetu waliofiwa wamewasomea dua marehemu bila kupewa miili ya marehemu.
Kifupi wameuwa, wameteketeza maiti au wamezika Kama wanyama makaburi ya halaiki.
Hata kisasi cha mauwaji ya Pemba 2001 hii imepitiliza.
Ukatili huu hauvumiliki.
Mimi pia tarehe 9/12 nitaingia road.
Leo kwa wale kesho inaweza kuwa kwangu hata nisipo shiriki maandamano.
Kijana jirani yetu aliuwawa siku ya tarehe 30 asubuhi alipoenda kununua mboga akiwa na mdogo wake wote bila silaha au chochote zaidi ya pesa.
kama hakuhusika na maandamano, na mm Maombi yangu yapo kwake apumzike kwa amani, kama alikua kwenye maadamano huo mwili usirudishwe
 
JF

Sijui kuhusu mitaa yenu, ila mitaa mingi nliyopita kunatokota sana. Watu wana machungu na hasira sana.

Kama wanadhani watu wameanza kusahau, wajue ardhi bado ni ya moto sana.

Haki huinua taifa.
Waambie wakiingia Tena barabaran kufanya wizi na uvunjifu wa amani mwendo ni ule ule,ulivyokuja ndivyo utavyopokelewa
 
Back
Top Bottom