sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,044
Ushirikina sio kutumia uchawi pekee, hata unapomshirikisha Mwenyezi Mungu na majini huo nao ni ushirikina.
Mkasa huu niliweza kuushuhudia live kwa macho yangu 2019, Mgonjwa alipona maradhi yake lakini hadi leo najiuliza ilikuwa sahihi kwa Sheikh / Ustadh kuyatumia majini sambamba na kuitumia Quran takatifu ?
Tumefika nyumbani kwa Shehe na mgonjwa, haya anamwambia akae chini kwenye mkeka, ghafla Ushtadh anapandisha majini, anaanza kucheka kama mtu alierukwa na akili eh heh ehe (kama ni mara yako ya kwanza utaogopa) anaanza kubeua na kucheua, kwa macho legevu mithiri ya kulewa anamtazama mgonjwa kwa makini katika namna ya kumchunguza. Mke wake yupo pembeni wanaangaliana na Ustadh machoni, hujui kinachoendelea kumbe kuna mawasiliano hapo, mke wake ndie anamwambia mgonjwa kwa lugha ya kibinadamu "kasema ufungue kinywa", "kasema usogee karibu usiogope", n.k. Ustadh anamaliza upelelezi, anazinduka akiwa amechoka, jasho linamtoka, anahema kama kakimbizwa umbali mrefu.
Shehe anaanza kuongea na mke wake lugha ambayo nadhani ni ya kikabila ama kiarabu, Shehe anamwambia mgonjwa afungue kinywa amgeukie mke wake, mkewe ghafla ni kama anapitiwa na usingizi akiwa amekaa kumbe nae kashapandisha hapo, anamchunguza mgonjwa kwa dakika 3 hivi, ili kujirudi Ustadh anamwite binti mdogo nadhani ni house girl anakuja kumtikisa anavyojua yeye ndio anazinduka.
baada ya hapo Shehe anaanza kusoma vifungu vya quran kama nusu saa hivi kwa sauti kubwa. Tiba zingine za ziada za mizizi, asali na mabaki ya miti yaliyosagwa ya kuogea mgonjwa anapewa awe anatumia, Shehe anamsisitiza mgonjwa awe anasali kila akiamka na kila akienda kulala, wawili tuliemsindikiza mgonjwa tunapewa jukumu la kuhakikisha anasali na kutumia hizo dawa.
Kwa siku 3 mfululizo mgonjwa tunampeleka mara mbili kusomewa visomo huku akiendelea na dozi.
Mgonjwa anaapona ila bado swali kuu linabaki kwamba kwanini majini hutumika ?
Mkasa huu niliweza kuushuhudia live kwa macho yangu 2019, Mgonjwa alipona maradhi yake lakini hadi leo najiuliza ilikuwa sahihi kwa Sheikh / Ustadh kuyatumia majini sambamba na kuitumia Quran takatifu ?
Tumefika nyumbani kwa Shehe na mgonjwa, haya anamwambia akae chini kwenye mkeka, ghafla Ushtadh anapandisha majini, anaanza kucheka kama mtu alierukwa na akili eh heh ehe (kama ni mara yako ya kwanza utaogopa) anaanza kubeua na kucheua, kwa macho legevu mithiri ya kulewa anamtazama mgonjwa kwa makini katika namna ya kumchunguza. Mke wake yupo pembeni wanaangaliana na Ustadh machoni, hujui kinachoendelea kumbe kuna mawasiliano hapo, mke wake ndie anamwambia mgonjwa kwa lugha ya kibinadamu "kasema ufungue kinywa", "kasema usogee karibu usiogope", n.k. Ustadh anamaliza upelelezi, anazinduka akiwa amechoka, jasho linamtoka, anahema kama kakimbizwa umbali mrefu.
Shehe anaanza kuongea na mke wake lugha ambayo nadhani ni ya kikabila ama kiarabu, Shehe anamwambia mgonjwa afungue kinywa amgeukie mke wake, mkewe ghafla ni kama anapitiwa na usingizi akiwa amekaa kumbe nae kashapandisha hapo, anamchunguza mgonjwa kwa dakika 3 hivi, ili kujirudi Ustadh anamwite binti mdogo nadhani ni house girl anakuja kumtikisa anavyojua yeye ndio anazinduka.
baada ya hapo Shehe anaanza kusoma vifungu vya quran kama nusu saa hivi kwa sauti kubwa. Tiba zingine za ziada za mizizi, asali na mabaki ya miti yaliyosagwa ya kuogea mgonjwa anapewa awe anatumia, Shehe anamsisitiza mgonjwa awe anasali kila akiamka na kila akienda kulala, wawili tuliemsindikiza mgonjwa tunapewa jukumu la kuhakikisha anasali na kutumia hizo dawa.
Kwa siku 3 mfululizo mgonjwa tunampeleka mara mbili kusomewa visomo huku akiendelea na dozi.
Mgonjwa anaapona ila bado swali kuu linabaki kwamba kwanini majini hutumika ?