Kuna watu wanamaisha magumu sana

Kuna watu wanamaisha magumu sana

Mimi nilitoka Club na mipombe kibao nikasema nikirudi home na harufu hii wale maustadhi hawatanielewa kabisa.

Nikamcheki chali anakaa ilala pale mtaa wa Manyoni st na Bungoni st karibu na Don hotel pale. Sasa nikataka kuingia choo kilikuwa na harufu flani mbaya hatari. Halafu vile vyoo kuchutama nilitoka mbio mpaka leo nikenda naishia nje tu.
 
Endelea ....
Huyo rafiki angu alikuwa akifanyakazi za saidia fundi kubeba zege, kuchimba mitaro, gardening, kubeba mawe na kazi nyingine kibao ila chakushangaza hata nguo zake ni mbovu hanunui nguo mpya ni zilezile tu.

Nilijiuliza shida labda itakuwa kodi lkn nikitathimini anapoishi kodi haivuki 20000 kwa mwezi.
nilihitaji kumuuliza pesa anapeleka wapi lkn nikaingiwa na wazo nikifny hivyo itaonekn km namchunguza ikabidi niache ila nakaamua nitumie njia nyingine.

Kuna siku nilimuomba aje tuonane pahala nikamwambia naomba niazime simu yako kidogo rfk angu maana yangu imezima akanipatia sasa nikaanza kupekuwa asee nilikutana na majina ya ajabu sana mara Aisha utamu , Mshangazi, My Heart, lingine Wife mbeya asee moja kwa moja nikajua pesa anawapa wanawake na kwao hua hatumii pesa kabisa.

Hio siku ilipita siku nyingine majira ya jioni bado nilikuwa nae tunapiga story za hapa na pale mara simu yake ikaanza kuita nikamwambie mpokelee simu akapokea nilisikia sauti ya kike inafoka hata bila salamu et ivi wewe unajitoa akili nimekwambia nitumie pesa kama kweli unataka niwe mkeo nilisikitika sana.
hio sauti ya kike ikaendelea kufoka kama hutumi hio pesa mimi na wewe basi tuachane, jamaa yangu alianza kulia kama mtoto mdogo nilimuonea huruma sana lkn sikua na jinsi issue za mapenzi hua siziingilii.

Lkn nilimshauri kitu arudi om akajipange kama shida ni mwanamke basi aoe nikatoka zangu dar .

Angalizo,Unapoenda sehemu kijitafuta achana kabisa na mambo ya wanawake, Wanawake wanarudisha sana nyuma maendeleo ya kijana anaejitafuta mjini.
Achana na kina asha utamu, mara zuuuh , Kina cutee😁 utaisha hawezi kukushauri chochote yeye ni leta tule akupe kipapa basi, unabeba zege afu ela unaipeleka huko ungemtumia ata maza nyumbani ungebarikiwa
 
Ni mwaka fulani nipita apo Dar, nikaamua nipite kwa mshikaji wangu wa kitambo tulisoma wote huko kanda ya ziwa.

Nilimtafuta akanambia yeye yupo kulagwa akanambia hana ela ya usafiri kunifata nilipo nikaona isiwe shida nikamfuata.

Nilipofika asee sikuamini maisha yamemponda sana ile sana nikamuuliza vitu mzee akanambia kama ninavomuona nilimhurumia sana nikampatia 50000 ya kumsaidiasaidia.

Tukaenda adi alipopanga tulipofika akanambia ndio hapa binapoishi asee nje kuchafu choo hakuna, bafu hakuna, maji hakuna, umeme hakuna nikaamua nimuulize unaishije sasa ndugu yangu akasema ni kawaida ameshazoea maisha hayo.

Tukaongozana kuelekea ndani mlango ulikuwa umefungwa tulipokaribia mlangoni kwake akainama akaokota jiwe nikamuuliza vipi tena mbona jiwe tena akacheka akasema hili sio jiwe ni funguo yangu mara akapiga jiwe juu ya kufuri, kufuri likafunguka nilisitajabu sana.

Alipofungua mlango tu ivi asee chumba hakina sakafu nzuri madirisha hakuna nilipowasha kitochi cha simu hakun godoro analala kwenye mkeka tu

Chumba kichafu sana harufu kali sana ya nguo chafu vyombo kama vinamiaka havijaona maji.
nilishindwa kukaa pale nilimpa pesa kidogo nikaenda zangu kulala lodge

Dar anamiaka karibia kumi lakini hata godoro hana
FUNZO,UNAPOPATA MAISHA MAZURI MSHUKURU MUNGU SANA MAANA KUNA WATU WANAISHI KAMA WANYAMA .
Namshukuru Mwenyezi mungu
 
Naona wengi mnashindwa kuelewa utofauti kati ya Maisha magumu, Mali na Hali.

Mtu anaweza kuwa hana kipato[Mali] lakini ana hali ya usafi, afya njema iliyotunzwa na ana furaha tu kwasababu anaamini anaelekea pazuri.

Uchafu, Ulevi na Kupenda ngono ni tabia ambazo hata watu matajiri wanazo.
Kuna watu hawana mali ila wana hali nzuri kiusafi na kitabia.
 
Ni bora maana haishi kwa ndugu au shemeji ila kung'ang'ania kuishi dar 10yrs na bado life haliko poa mwambie abadili location
 
Ni mwaka fulani nipita apo Dar, nikaamua nipite kwa mshikaji wangu wa kitambo tulisoma wote huko kanda ya ziwa.

Nilimtafuta akanambia yeye yupo kulagwa akanambia hana ela ya usafiri kunifata nilipo nikaona isiwe shida nikamfuata.

Nilipofika asee sikuamini maisha yamemponda sana ile sana nikamuuliza vitu mzee akanambia kama ninavomuona nilimhurumia sana nikampatia 50000 ya kumsaidiasaidia.

Tukaenda adi alipopanga tulipofika akanambia ndio hapa binapoishi asee nje kuchafu choo hakuna, bafu hakuna, maji hakuna, umeme hakuna nikaamua nimuulize unaishije sasa ndugu yangu akasema ni kawaida ameshazoea maisha hayo.

Tukaongozana kuelekea ndani mlango ulikuwa umefungwa tulipokaribia mlangoni kwake akainama akaokota jiwe nikamuuliza vipi tena mbona jiwe tena akacheka akasema hili sio jiwe ni funguo yangu mara akapiga jiwe juu ya kufuri, kufuri likafunguka nilisitajabu sana.

Alipofungua mlango tu ivi asee chumba hakina sakafu nzuri madirisha hakuna nilipowasha kitochi cha simu hakun godoro analala kwenye mkeka tu

Chumba kichafu sana harufu kali sana ya nguo chafu vyombo kama vinamiaka havijaona maji.
nilishindwa kukaa pale nilimpa pesa kidogo nikaenda zangu kulala lodge

Dar anamiaka karibia kumi lakini hata godoro hana
FUNZO,UNAPOPATA MAISHA MAZURI MSHUKURU MUNGU SANA MAANA KUNA WATU WANAISHI KAMA WANYAMA .
Jiji la Dar limechelewesha na kuua ndoto za vijana wengi sana.
 
Ni bora maana haishi kwa ndugu au shemeji ila kung'ang'ania kuishi dar 10yrs na bado life haliko poa mwambie abadili location
Sawa
Jiji la Dar limechelewesha na kuua ndoto za vijana wengi sana.
Kweli kabisa maana maendeleo yake hamna kbs , muda mwingine anapiga si.u mkoani anaomba kodi asee
 
At least ulimpa fedha kidogo,safi sana,
Kama una uwezo kiasi,muulize ana fanya issue gani ili umsapoti kwenye hizo issue zake,au ajaribu maisha kwingine na sio kuendelea kupoteza time yake Dar tu,

Kitendo cha wewe kumtafuta mtu mliyesoma nae,kinaonyesha una moyo wa upendo na una jali,

Pia kitendo cha huyo rafiki yako kukuonyesha maisha yake halisi bila kukuficha,kina ashiria kua nae ni mtu mwema japo bado hajajipata.
Mleta mada hana huo wema, angekuwa mwema asingekuja kumuanika rafiki yake humu. Kama kaweza kuandika uzi basi jua mitaani ameshamchafua sana. Waogope ssna watu uliokuwa nao mtaani, uliosoma nao utotoni na uliomaliza nao chuoni.
 
Back
Top Bottom