Waswahili mna maneno ya shombo sana. Unadhani kulima siku hizi ni rahisi sana kama zamani wakati mvua ni ya uhakika na hakuwa na pembejeo za gharama kama saizi.Arudi Kijiji akalime kama unaweza mtafutie kibarua ila usikutupuke. Usimuonee sana mtu huruma katika hali aliyonayo hujui alipotokea jipe muda kujua sababu za kuwa na hali hiyo.
Pia wengi mnajua kulima ni adhabu na kwa vile mko Mjini mnajua maisha mmeyamaliza ila kwa taarifa yenu nawaomba mjaribu kutembea muone watu wanalima na wana miliki vitu vikubwa kuliko hata sisi tuliobanana hapa Dar hata hewa nzuri shida.
Bado hali ya maisha ni ngumu popote pale sio mjini wala Kijijini na hii hali ya kukalili maisha kuwa ni Mjini hasa Dar es Salaam ni anguko kubwa sana kwa vijana wengi.