Kuna Viboko kumfanya mtoto aelewe na Kuna Viboko kumpa mtoto Nidhamu!

Adhabu ya viboko kwa watoto ni barbaric na mojawapo ya adhabu za hovyo sana katika karne ya 21.
Ww mtoto wako huwa akikosea huwa unampa hadhabu gani akosea nje ya viboko au bado hujazaa?
 
Hao hao walio sema kuwa kupiga mtoto ni ukatiri ndo hao hao walio sema kufanya ushoga na kutoa mimba ni halali.

Kufananisha mfumo wa maisha wa mnyama na binadamu ni upumbavu maana ni mifumo miwili tofauti kabisa.
Kwani mnyama akiuwa au akijeruhi huwa nafungwa jera kama binadamu anavyo fungwa?
Binadamu ameubwa katika mfumo ambao ili haache makosa ni lazima ayajutie na ili ayajutie ni lazima haadhibiwe pale anapo fanya makosa.

Kwahiyo ww mtoto wako akikosea huwa unamuita na kufanyia sherehe na kumpongeza?

Kama ulishawahi kupendwa katika maisha yako na Wazazi/Mlezi huwezi kuthubutu kumfanyia ukatili mtoto wako mwenyewe damu yako, ni sawa na Mwanamke ambaye ameolewa anapigwa kila na Mume wake lkn bado anarudi na kumtetea mtesi wake, hiyo ni psychological problem, kama ulipendwa na kukulia maisha ya amani na furaha utajua upendo ni nini lkn kama ulikosa upendo ni ngumu kujua na ndio maana kwako unaona ni kawaida kutesa mtoto wako damu yako mwenyewe!
 
Mi naona mwalimu ashughulikie taaluma ya mtoto, maswala ya nidhamu amwachie mzazi.

Kama mikono inawasha akachape watoto wake
 
Matokeo ya viboko ni tumepata taifa la hovyo. Taifa la watu waoga ambao hawawajibiki mpaka kuwe na adhabu. Watu ambao kwao hakuna jambo baya, ila ubaya ni kukamatwa na kuadhibiwa.
 
Viboko Ni muhimu Sana kwa wanafunzi jitu zima liko lasaba halijui horoza hata Kwanza Hadi ya hata tano

Bila fimbo huu Ni mwanafunzi kweli

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Hao hao walio sema kuwa kupiga mtoto ni ukatiri ndo hao hao walio sema kufanya ushoga na kutoa mimba ni halali.

Kufananisha mfumo wa maisha wa mnyama na binadamu ni upumbavu maana ni mifumo miwili tofauti kabisa.
Kwani mnyama akiuwa au akijeruhi huwa nafungwa jera kama binadamu anavyo fungwa?
Binadamu ameubwa katika mfumo ambao ili haache makosa ni lazima ayajutie na ili ayajutie ni lazima haadhibiwe pale anapo fanya makosa.

Kwahiyo ww mtoto wako akikosea huwa unamuita na kufanyia sherehe na kumpongeza?
Umeonges Busara Sanaa

Inawezekana yeye watoto wake, wakikosa anawafanyia sherehe
 
Nakumbuka wakati nasoma ,Kuna wanafunzi walikua Wana Uwezo wa kawaida , wengine kupuuza tu mambo Kwa kiburi n.k, Walimu walisimama kidete, Umepewa Kazi hujafanya Makusudi ,Bakoraa !! umepewa Kazi umekosa zaidi ya Nusu ,bakoraaa .. Mimi mwenyewe niliwah Chapwa bakora Kwa sababu ya Mwandiko mbovu !!.
Ndio, Wakati Mwingine Bakora humuogopesha Mwanafunzi ,na kumwondelea Uwezo na wengine Kugeuza Fimbo kama sababu ya Kuacha Shule.

Tukimchukulia yule Dogo wa Mtwara, yeye aliamua kuandika Barua mwenyewe Kwa Mkuu wa Shule, kwamba Bwana eeehh Mimi Kwa hiyari yangu sitaki shule tena, na anahojiwa anasema, Hata Wakimfunga Baba yangu, wao wamfunge lakini Shule siendiiiiiii siendiiii!!.

Je huyu kaacha shule sababu ya Fimbo?.

Kuna Wale Vijana walochoma Bweni kipindi fulan, nakumbuka Hayati JPM alisema, wachapweee Viboko, Wazazi wao waitwe wajenge Bweni, kama hawawez wafukuzwe shule !!.

Je wanafunzi kama Hawa , uharifu Huu ni sababu ya Uwepo wa Fimbo Shuleni?.

Ufaulu Kwa shule za Serikali kua mbaya, Je ni matokeo ya kuwepo Kwa Fimbo mashuleni ?.

Katika kanuni ya KIROHO na kimbingu, ,maandiko yasema

Mithali 13:24. Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; Bali yeye ampendaye humrudi mapema.

He that spareth his rod hateth his son: but he that loveth him chasteneth him betimes.....

Hamna Uponyaji wa Akili na Tabia Kwa mtoto awaye yoyote yule hapa chini ya Jua ambaye Wazazi na jamii yake inayomzunguka itaamua kutougusa mwili wake Kwa Fimbo !!.

Leo hiii Bunge Linajadili Et na nyumbani pia kuwekwe Sheria za utoaji adhabu?.

Leo hii Bunge Linajadili Et, Tuondoe Fimbo mashuleni !?.

Kwamba Tuondoe Fimbo katika kizazi ambacho, Wazazi wamekua wahovyoo, wanazaa watoto wanaolelewa hovyo, Leo hii watoto wapo Shuleni Kwa Waalimu ambao nao ni Wazazi, huko Walimu wanahitajika kutumia Fimbo katika kurekebisha tabia fulan fulan za mtoto , Nako mnataka Fimbo zisitumike?.

Ni SHETANI pekee anayejificha nyuma ya Haki za Binadam ndiye aendaye kinyume na maelekezo ya Mwenyezi Mungu , Siku zote SHETANI yupo kinyume na Mungu, SHETANI anapambana Dunia iwe na kizazi Cha hovyooo kisicho na maadili ,kizazi kisichoogopa dhambi !!.

Badala ya Kujadili jinsi ya kulinda watoto dhidi ya Ushoga, mnajadili Fimbo?.

Filamu zinazochochea Ushoga, tamthiliya zinazochochea Ushoga, Jamii kua na lugha chafu mbele ya watoto, kiasi kwamba watoto Leo hii wanafirana Kwa Kasi ya ajabu, watoto wanakua wakiwa hawana Uanaume, badala ya Kujadili namna ya kumlinda huyu mtoto wa kiume, mnajadili kuondoka bakora ??.

ustaharabu gani huuu ?? Unaiga ustaharabu wa Magharibi?. Mataifa ambayo yamejichokea kabisa kinidhamu, Et Nawewe Muafrika, Sasa umuache mtoto wako aseme na atende apendavyo kwakua Kuna haki za Binadam?.

Kizazi Bora kinaandaliwa, Kama lengo ni kuondoka Fimbo kama sehem ya adhabu, Je ni watoto wa aina gani mnawapeleka Shuleni ili Waalimu wetu wanaoishi Kwa shida sana , wasitumie Bakora ?.

Wajibu wa Wazazi katika kurekebisha Tabia za wanao kabla hamjawapeleka shule ni upi? Ili Walimu wetu wabaki na kazi ya kufundisha tu nasio kudeal na Nidhamu ya Mwanafunzi ?.

Kama Lengo ni kuondoa Fimbo ili wafaulu, ni kweli kabisa utafiti mmefanya mkagundua mkiondoa Fimbo watoto watafulu?.


Serikali na Bunge .....

Kwa Ajili ya Taaluma ...

1- Ufaulu ni matokeo ya Uwezo mzuri wa akili , Nchi Ina njaaa hii watoto hawali , amekula saa 10 jion, keshoa ende shule, Sukari imemshuka mwilin, ataelewa??.. HAKIKISHENI MTANZANIA ANAKULA MILO MITATU, HAKIKISHENI WATOTO WANAKULA ILI KUUJENGA UBONGO!!.

2.. Wekezeni Kwa dhati kwenye Elimu .
Mtoto ambaye tayari amekula, ubongo umetulia, anahitaji Mwalimu Bora wa Hesabu, anahitaji Mwalimu Bora wa kingereza ... Unataka Mwanafunzi afaulu hesabu alafu Mwalimu mwenyewe sio mjuzi wa Hesabu niile tu ni Mwalimu kwamba anaweza fundisha lolote Somo???

3-Toeni Motisha Kwa Walimu, Sisi Walimu tuna msemo wetu tunasema "uzuri mwisho wa mwezi mshahara unaingia" .....Hawa Walimu wanahitaji Motisha, mbona Afya tunakula hela mpaka unasema iiihhii Serikali Ina Hela ya kuchezeaa, kwann Walimu msiwakumbuke Kwa Motisha, msiwafanye wakajihisi kunipenda kazi .... Hivi mnajua, Mwalimu wa Tanzania ndio kiumbe mwenye stress za Maisha kuliko hata Mama Ntilie??. Mwalimu anastress za Maisha, anaingia kazin anakutana na Juma macho makubwa haadiki notice Kwa mwezi mzima, mnataka afanyeje ??? Mbona mahela mengi mnayapiga Kwa ufisadi Kila kukicha ?.

4-Wapeni Waalimu Uhuru wa Utumiaji Bakora Ndani ya Darasa kama sehem ya kufundishiaa , Mwalim anafundisha Kuna mtoto anapiga kelele chapa Fimbo , katoa H/Work hujafanya, chapa fimbooo !!.

na Mwalimu atapima Saikolojia ya mtoto Mmoja dhidi ya mwingine IKIWA huyu anaweza elewa Kwa Fimbo, au huyu anahitaji kuelewa Kwa ushauri .... TUSIMUONDOLEE MWALIMU UHURU WA KUTUMIA FIMBO !!.

5-Tuwaboreshee mazingira ya utendaji kazi Hawa Walimu wetu, Madarasa , maabara, michezo pia tuguse.

KWA AJILI YA NIDHAMU

1-Wazazi waache ujinga, Wazazi waache kusukumia nafasi zao Kwa watu wengine, Wazazi ndio Walimu wakwanza wa watoto, Wazazi wawajibike, na WAWACHAPE WATOTO WAO FIMBO, FIMBO HAIUI, CHAPENI WATOTO, MSIWALEE KIMAANDAZI MAANDAZI .

2-WALIMU WASIONDOLEWE NAFASI YAO YA UTUMIAJI WA FIMBO KUREKEBISHA TABIA ., ACHENI WATOTO WACHAPWE MAKALION ILA UWEKWE UTARATIBU MZURI TU NA WALIMU WAUFATE.

3-VIONGOZI WA DINII, MMELALA SANAA,. VIONGOZI WA DINI WAMELALA, NA KUSHUKA KWA NIDHAM ZA WATOTO KWA UJUMLA ,KWA NAMNA MOJA NI MATOKEO YA DINI ZETU KUJIKITA KWENYE MAFUTA YA UPAKO , CHUMVI, UTAJIRI, FEDHA, MAGARI, WANASAHAU KUNA KIZAZI KINACHOHITANI MALEZI, VIONGOZI WA DINI WANAKULA MUDA WA WAZAZI MPAKA WAZAZI WANASHINDWA TIMIZA WAJIBU WAO HOME, HAO HAO VIONGOZI WA DINI , HUWEZ KUTA WANAFUNDISHA JUU YA MALEZI YA WATOTO, KUWAFUNZA WATOTO N.K!!.

4-MTOTO WA MWENZIO NI WA KWAKO, JAMII USIMPUUZE KUMREKEBISHA MTOTO WA MWENZIO.

5-TUMTANGULIZE MUNGU MBELE , KWA SASA PAMBANO KUU NI BAINA YA SHETANI BABA WA MAOVU ,DHIDI YA UUNGU UTAKATIFU... TUMTANGULIZE MUNGU MBEKE., TUOMBEE WATOTO WETU!!.
Laiti watunga Sera na Viongozi wote (Serikali +Dini zote + Wanasiasa) wangezingatia hayo uliyoshauri hapa, tungefanikiwa pakubwa sana. Ubarikiwe sana kwa andiko hili.
 
Kama ulishawahi kupendwa katika maisha yako na Wazazi/Mlezi huwezi kuthubutu kumfanyia ukatili mtoto wako mwenyewe damu yako, ni sawa na Mwanamke ambaye ameolewa anapigwa kila na Mume wake lkn bado anarudi na kumtetea mtesi wake, hiyo ni psychological problem, kama ulipendwa na kukulia maisha ya amani na furaha utajua upendo ni nini lkn kama ulikosa upendo ni ngumu kujua na ndio maana kwako unaona ni kawaida kutesa mtoto wako damu yako mwenyewe!
Kwa hiyo ww ukikosea serikali ikakufunga inakuwa imekufanyia ukatiri na sio kulipia makosa uliyo yafanya?

Adhabu na ukatiri vina husiana nn? Ukatiri kwa mtoto utafisirika pale utakapo mpa adhabu kubwa na isiyo endana na umri wake na kosa lake.
Kwani mtoto akikosea ukachukua kafimbo kadogo ukamcharaza tuviboko tutatu huyo mtoto atapungukiwa na nn?


Huwezi kusema una upendo kwa mtoto alafu awe anafanya mambo ya kumpoteza alafu unamuacha kwa kigezo cha eti kupiga mtoto ni ukatiri.

Nimekuuliza swali hujanijibu ww mtoto wako huwa akikosea huwa unamuita na kumpongeza na kufanyia sherehe?
 
Hao hao walio sema kuwa kupiga mtoto ni ukatiri ndo hao hao walio sema kufanya ushoga na kutoa mimba ni halali.

Kufananisha mfumo wa maisha wa mnyama na binadamu ni upumbavu maana ni mifumo miwili tofauti kabisa.
Kwani mnyama akiuwa au akijeruhi huwa nafungwa jera kama binadamu anavyo fungwa?
Binadamu ameubwa katika mfumo ambao ili haache makosa ni lazima ayajutie na ili ayajutie ni lazima haadhibiwe pale anapo fanya makosa.

Kwahiyo ww mtoto wako akikosea huwa unamuita na kufanyia sherehe na kumpongeza?
Hii nimeipenda na ndio ukweli. "Hao hao walio sema kuwa kupiga mtoto ni ukatiri ndo hao hao walio sema kufanya ushoga na kutoa mimba ni halali."
Na wapo wanaotumia msemo wa vijiweni........"Hapendwi mtu hapa........"
 
Kwa hiyo ww ukikosea serikali ikakufunga inakuwa imekufanyia ukatiri na sio kulipia makosa uliyo yafanya?

Adhabu na ukatiri vina husiana nn? Ukatiri kwa mtoto utafisirika pale utakapo mpa adhabu kubwa na isiyo endana na umri wake na kosa lake.
Kwani mtoto akikosea ukachukua kafimbo kadogo ukamcharaza tuviboko tutatu huyo mtoto atapungukiwa na nn?


Huwezi kusema una upendo kwa mtoto alafu awe anafanya mambo ya kumpoteza alafu unamuacha kwa kigezo cha eti kupiga mtoto ni ukatiri.

Nimekuuliza swali hujanijibu ww mtoto wako huwa akikosea huwa unamuita na kumpongeza na kufanyia sherehe?

Kwa nini umpe mtoto adhabu? Hiyo ni psychopathy, hilo la Serikali kutoa adhabu ni kwa criminals sidhani kama unataka kumfananisha mtoto wako damu yako na criminals ambao wanafungwa na Serikali ili kuprotect jamii.

Kama umelelewa kwa upendo na amani huwezi mpa adhabu mtoto damu yako, hiyo wording peke yake kwamba adhabu inaonyesho ukosekano wa upendo!
 
Kwa nini umpe mtoto adhabu? Hiyo ni psychopathy, hilo la Serikali kutoa adhabu ni kwa criminals sidhani kama unataka kumfananisha mtoto wako damu yako na criminals ambao wanafungwa na Serikali ili kuprotect jamii.

Kama umelelewa kwa upendo na amani huwezi mpa adhabu mtoto damu yako, hiyo wording peke yake kwamba adhabu inaonyesho ukosekano wa upendo!
Sidhani uko sahihi sana mkuu. Mwanao unamleaje?Unamlea peke yako? Mtoto unayempenda kwa kawaida mzazi huwa unatamani kwamba hapo baadaye ajekuwa ni mtu wa namna fulani ndani ya Jamii. Upendo ni pamoja na kumrudi (kumpa adhabu) ili ajitambue kwamba alichofanya sio kitu chema au kizuri. Zipo njia nyingi za kumfundisha atambue mambo mema na mabaya. Wewe kama mzazi utatamani aache na kuepuka yale mabaya na azingatie kutenda yale mema siku zote na mwishowe hiyo ijijenge kwake na iwe ndio tabia yake.
Je, labda mwanao anaanza mazoea ambayo baadaye inaweza kuja kuwa ni tabia kwa kuanza kidogo-kidogo kuiba sukari nyumbani au kwenda kwa majirani na kujichukulia bila kuomba e.g. maembe au chochote anachokitamani. Kweli ww utambembeleza? Ukimkataza hasikii anarudia na wakati mwingine ukimwita ili kumuonya anakimbia. Utamchekea tuu?
Kwa kufanya hivyo ww ndo utakuwa unaonesha una tatizo la Psychopathy kwani hata jamii unamoishi hawatakuelewa yaani huendani na mfumo uliopo wa kijamii (ww uko kinyume) ambapo watoto wanalelewa kwa kila aina ya mbinu inayokubalika. Kumbuka mtoto ni wako kwa kuzaa lakini kijamii ni mtoto atakayelelewa na Jamii nzima ili hatimaye aweze kukubalika ndani ya jamii mahalia. Mtoto mtukutu, mtundu, mwizi, mjeuri na asiye na adabu huwa ni aibu na fedheha kwa wazazi wake na huwa ni chukizo/kero ndani ya jamii na lawama huenda kwa wazazi kwamba wazazi wameshindwa kumlea. Je, utauficha wapi uso wako ikiwa Jamii nzima inakunyoshea kidole? Usidhani kwamba utadumu daima na mwanao huyo unayempeti-peti.
 
Hoja zako ni nzuri,,but bado fimbo haiwezi kuwa solution kwa karne hii.
Ni kweli fimbo haiwezi kuwa solution kwa karne hii bali ni mojawapo kati ya mbinu nyingi zinazoweza kutumika ili kufikia lengo.
 
Kwa hiyo ww ukikosea serikali ikakufunga inakuwa imekufanyia ukatiri na sio kulipia makosa uliyo yafanya?

Adhabu na ukatiri vina husiana nn? Ukatiri kwa mtoto utafisirika pale utakapo mpa adhabu kubwa na isiyo endana na umri wake na kosa lake.
Kwani mtoto akikosea ukachukua kafimbo kadogo ukamcharaza tuviboko tutatu huyo mtoto atapungukiwa na nn?


Huwezi kusema una upendo kwa mtoto alafu awe anafanya mambo ya kumpoteza alafu unamuacha kwa kigezo cha eti kupiga mtoto ni ukatiri.

Nimekuuliza swali hujanijibu ww mtoto wako huwa akikosea huwa unamuita na kumpongeza na kufanyia sherehe?
Hoja hii "Adhabu na ukatiri vina husiana nn? Ukatiri kwa mtoto utafisirika pale utakapo mpa adhabu kubwa na isiyo endana na umri wake na kosa lake.
Kwani mtoto akikosea ukachukua kafimbo kadogo ukamcharaza tuviboko tutatu huyo mtoto atapungukiwa na nn?"
Ni hoja yenye mashiko
Hiyo ndo Hekima na Busara ya Mzazi anayempenda mwanaye. Hongera mkuu.
 
Mi naona mwalimu ashughulikie taaluma ya mtoto, maswala ya nidhamu amwachie mzazi.

Kama mikono inawasha akachape watoto wake
Hapo hapo kwenye kushughulikia Taaluma, Kuna wanafunzi bila kutumia Viboko, hawaelewi kabisa .

Wangapi Leo hii tunawakumbuka wale Walimu walikua wakali enzi zetu tunasoma naleo tunawakumbuka Kwa kutufanya tuwe Bora na wenye Thaman?.
 
Hoja hii "Adhabu na ukatiri vina husiana nn? Ukatiri kwa mtoto utafisirika pale utakapo mpa adhabu kubwa na isiyo endana na umri wake na kosa lake.
Kwani mtoto akikosea ukachukua kafimbo kadogo ukamcharaza tuviboko tutatu huyo mtoto atapungukiwa na nn?"
Ni hoja yenye mashiko
Hiyo ndo Hekima na Busara ya Mzazi anayempenda mwanaye. Hongera mkuu.
Alafu Ukatili na Utoaji adhabu ni vitu viwili tofauti.


Mwanadam anapokosea nilazima ajutishwe kupitia Adhabu
 
Back
Top Bottom