Niataeleza Kwa upana wa uelewa wangu:-
1.Ki Baiyolojia.
-wanaume tunazalisha Hadi uzeeni yaani tunaendelea kuwa na hamu ya kufanya ngono Hadi uzeeni ndio maana tunaoa hadi wajukuu,lakini kina mama Wana menopause ambayo huwasaidia kutunza virutubisho vyao hadi Hadi ubibi kizee!!kadiri mwanaume anavyofanya ngono ndivyo anavyokaribia kifo,IPO Siri katika kutofanya ngono ndio maana watawa wengi au jamii nyingi za siri hujitenga na ngono !!
2.Kiuchumi.
-Bado Sana sekta ya uzalishaji inaaminika ni ya wanaume yaani shughuli au kazi zote za nguvu na risky tunafanya sisi wanaume kwahiyo ajali,ulemavu,kupata sumu zinazoathiri mapafu,moyo,figo n.k hii inasababisha lifespan ya mwanamme kuwa fupi!
3.kijamii
Majukumu makubwa kenye familia,ukoo na jamii kapewa mwanamme ndio mtatuzi was changamoto za mahitaji ya wote,huu msalaba wanawake wamewatubebesha sisi hasta kama uwezo wanao,Hilo huleta sonona kwasababu ni ngumu kutimiza mahitaji ya wazazi,familia Yako na wazazi was mke wako Kwa pamoja,Bado presha ya kutotimiza hayo inamuandama Kila siku!!
4.kisiasa
Bado sisi ndio tuna tazamiwa kupigania uongozi kufa na kupona na hio huleta maadui ndani na nje ya familia,kifo hakiepikiki Kwa style hiyo!!
5.Ulozi,maagano na laana
Kila mwanamme Hadi anafikisha miaka 50 ameshajaribu mengi Santa katika utafutaji,ulozi na uganga hadi maagano mabaya keshajaribu ambayo Yana matokeo.chanya au hasi huko mbeleni!!
Laana za watoto,wapenzi wazazi kutokana na kutotimiza matarajio Yao pia zinatuandama kila kukicha!
Kurogwa au kuchezewa shere pale unapopata unafuu.wa maisha pia hufanya maisha yetu kuwanmafupi!
Ukufuatilia sana kwenye ukoo au familia wanaume tuliofanikiwa ndio hufa mapema.sana.wakiacha mali ambazo.wakati mwingine hazidumu!
Ni kuwindwa na.kuwindana Hadi siku.unaenda!!Hilo nimeona sana!!
Wengine wanaweza ongezea!!