Kuna sababu gani mimi kuoa?

Kuna sababu gani mimi kuoa?

Kama maziwa yanapatikana mitaani na nyama mabuchani, kuna haja gani ya kufuga ng'ombe???
Hakuna haja hapo..Cha msingi ni kununua nyama na kuila utakavyo huku ukishushia na maziwa fresh. Kufuga ng'ombe kupotezeana mda tu
 
Salaam wanajukwa,

Ijumaaa hiyo kwa wale wenzangu na mimi ambao Magufuli hajatuathiri sana tukutane.

Niende kwenye mada moja kwa moja.

Nimekua nikisoma story za watu nimekua nikishudia mwenyewe. Hata wewe unaesoma hapa na mpenzi wa jukwaa hili jaribu kupitia Thread za huku. Nyingi ni kuumizana, usaliti, kuzaa nje ya ndoa, kula mashemeji na mambo chungu nzima ya kuudhi na kuumiza.

Nimetafakari sana nikajiuliza kuna sababu gani mimi KUOA?

Nimekua nikiona rafiki zangu waliooa wakiwacheat wake zao, wadada rafiki zangu wakiwacheat waume zao marafiki zangu ambao hawajaoa wana wapenzi zaidi ya watatu na wanawapanga si mchezo.

Mimi mwenyewe nina wapenzi zaidi ya wawili na hawajuani na nikiwafatilia nao hao wapenzi wangu nao wana wapenzi wengine.

Binafsi nina mtoto nimezaa na mdada mmoja ila sijapanga kumuoa. Kila nikipata wazo la kuoa aisee nikikumbuka mambo ninayosoma na kushuhudia nakufa moyo sitamani kabisa ndoa.

Marafiki zangu karibia wote wameoa, wadogo zangu nao wanataka kuoa ila mimi bado najiuliza naoa kutafuta nini? Si niongeze mtoto mwingine na mwanamke mwingine halafu nilee tu watoto? Kwanini kuleta maumivu ndani ya nyumba?

BADO NAWAZA



wewe ni dini gani????
 
Salaam wanajukwa,

Ijumaaa hiyo kwa wale wenzangu na mimi ambao Magufuli hajatuathiri sana tukutane.

Niende kwenye mada moja kwa moja.

Nimekua nikisoma story za watu nimekua nikishudia mwenyewe. Hata wewe unaesoma hapa na mpenzi wa jukwaa hili jaribu kupitia Thread za huku. Nyingi ni kuumizana, usaliti, kuzaa nje ya ndoa, kula mashemeji na mambo chungu nzima ya kuudhi na kuumiza.

Nimetafakari sana nikajiuliza kuna sababu gani mimi KUOA?

Nimekua nikiona rafiki zangu waliooa wakiwacheat wake zao, wadada rafiki zangu wakiwacheat waume zao marafiki zangu ambao hawajaoa wana wapenzi zaidi ya watatu na wanawapanga si mchezo.

Mimi mwenyewe nina wapenzi zaidi ya wawili na hawajuani na nikiwafatilia nao hao wapenzi wangu nao wana wapenzi wengine.

Binafsi nina mtoto nimezaa na mdada mmoja ila sijapanga kumuoa. Kila nikipata wazo la kuoa aisee nikikumbuka mambo ninayosoma na kushuhudia nakufa moyo sitamani kabisa ndoa.

Marafiki zangu karibia wote wameoa, wadogo zangu nao wanataka kuoa ila mimi bado najiuliza naoa kutafuta nini? Si niongeze mtoto mwingine na mwanamke mwingine halafu nilee tu watoto? Kwanini kuleta maumivu ndani ya nyumba?

BADO NAWAZA
Huo ni uoga wako tu. Mbona ajali barabarani ziko kibao ila watu bado wanasafiri na wengi hufika salama huko waendako! Ndoa ni kama safari. Jua dhumuni lako la kuoa... Usifanye kuiga au kushinikizwa. Wewe mwenyewe jitambue kua unahitaji kuoa. Tafuta mwenza mtakaeweza ishi pamoja bila mvurugano. Hapa ndo ambapo Mungu anahitajika zaidi... Muombe akuletee mke wako. Watu wengi huchanganywa na feelings tu. Eti unamuoa mtu kwa sababu unampenda tu. Upendo unaatengenezwa, unakua na unaweza kufa pia... Unaingia kwenye ndoa kwa sababu unapenda tu sijui utafanya nini upendo ukianza kupungua! Angalia sababu zingine na sio upendo tu.
Kingine, swala la kua na michepuko mi naona wanaume ndo kabisa hawawezi jizuia. Ila kama mume husimfanye mkeo akahisi kabisa kua kuna mtu mwingine pembeni. Jali familia yako na muoneshe upendo. Mfanye mkeo awe kama wanawake unaowapenda huko nnje. Kama unapenda wanaovaa vimini, mvalishe mkeo.
Ukimjua mwenza wako wala hakutakua na ugomvi kati yenu.
 
Baba zetu wangekuwa wana fikra za hivi sijui ingekuwaje????nadhani wote humu tungekuwa watoto wa mwendokasi
Heshima sana Baba yangu kwa kumuoa mama yangu laiti ungefikiria kama huyu Leo hii ningekuwa mtoto wa single mother
 
Kama maziwa yanapatikana mitaani na nyama mabuchani, kuna haja gani ya kufuga ng'ombe???
Mwanaune alieoa anaheshimiwa zaidi ya kapela. Yaani unaonesha jinsi gani ulivo responsible. Ata maofisini... Mtu alie na mke anaaminiwa kupewa majukumu fulani.
 
Mwanaune alieoa anaheshimiwa zaidi ya kapela. Yaani unaonesha jinsi gani ulivo responsible. Ata maofisini... Mtu alie na mke anaaminiwa kupewa majukumu fulani.
Bila shaka we ni KE nimehisi.Hivi kama una mke anayechepuka na vitoto vidogo, utaheshimiwa kiaje??? inamaana hujawahi kuona mabachelor wanaojituma ktk kazi, wenye mafanikio??? hiyo siyo alama ya mtu aliye responsible???
 
Humu duniani kuna kuumwa mara magonjwa mbali mbali, mara kuna ajali zinatokea kila siku, mara kuna kukosa hela sometimes, mara kuna kugombana na watu Saa ingine huna kosa, kuna kusingiziwa kesi Saa zingine polisi, mara kuna kukosa hela yaani tabu tupu!

Kuna marafiki zako wengi wamepitia hayo, wengine kuumwa, wengine kukosa hela, wengine ajali nk

Sasa niambie kuna faida gani wewe kuishi? Kwwnn usighaili kuishi ukajiua zako tu
 
Bila shaka we ni KE nimehisi.Hivi kama una mke anayechepuka na vitoto vidogo, utaheshimiwa kiaje??? inamaana hujawahi kuona mabachelor wanaojituma ktk kazi, wenye mafanikio??? hiyo siyo alama ya mtu aliye responsible???
Ni mawazo yangu tu na jamii niliokulia.
 
kama unapata maziwa haiana haja ya kufuga ng'ombe
kweli kabisa,ifike wakati tuache kuishi kwa mazoea,hizi pingu za maisha,zilishapitwa na wakati,at least watu waishi kwa mikataba,mkichokana au mwisho wa mkataba kila mtu aende kivyake
 
Yule rais wa Taiwan sijui mwanamke aliulizwa hujaolewa akasema hawezi nunua nguruwe nzima kwa ajili ya sausage. Acha usioe kama Hitaji lako kwa mwanamke Ni Hilo tu utamtesa mkeo
 
Back
Top Bottom