Kuna mwana JF amesoma ''The Urantia Book"?

Kuna mwana JF amesoma ''The Urantia Book"?

Kuna kosa la msingi huwa unalifanya.

Kitendo Cha kuthibitisha au kutothibitisha uwepo wa Mungu haifanyi hiko kitu kuwepo au kutokuwepo.

Mfano;

Mimi nimeua Kisha nikapelekwa mahakamani kusomewa mashtka, kabla ya hukumu nikapewa nafasi ya kujitetea "nithibitishe" kwamba sijaua. Hapo mahakamani nikatoa maelezo yangu ya utetezi Kisha wakati wa hukumu Sheria ikaona Sina kosa na hivyo kuikwepa hukumu ya kifungo au kunyongwa kwa kosa la mauaji. Nimekuwa huru kwa mujibu wa Sheria.

Kwa lugha nyepesi ni kwamba, Sheria imeshindwa kuthibitisha kwamba Mimi ni muuaji(nimeua).

Ila ukweli ulio wazi ni kwamba niliua/nimeua. Ila Sheria imeshindwa kuthibitisha hivyo ikashindwa kunihukumu.

Nahitimisha kwa kusema kuwa MUNGU ANASIMAMA KAMA KWELI.MUNGU NI KWELI. Kweli inasimama Kama moja. Kweli haithibitishiki. Either unishinde kwa hoja au nikushinde,hiyo haifanyi kutokuwepo kwa Mungu.

Ni Kama uchawi tu, either uuthibitishe au usiuthibitishe haifanyi uchawi usiwepo. Uchawi upo na kupitia nguvuna matokeo ambayo binafsi nimezishuhudia kwa macho Kama mtu aliyekufa kisha kuwekwa msukule kisha kumuona akiwa mzima miaka mingi baadae ikiwa imeenda. Kama tusivyoweza kuona uchawi ila tunauona kupitia matokeo ndivyo ambavyo hatuwezi kumwona Mungu na kumthibitisha katika namna ambayo wasioamini wanataka tuthibitishe ila tunaona nguvu zake zinavyooperate.

Mungu yupo.

NB: Hili la uchawi nimechomekea tu,tusifanye kuwa mjadala.
Sawa.

1.Kuna vitu vipo, na vinathibitishika kuwa vipo. Hivi tunapata uhakika kwamba vipo, havina tabu.
2. Kuna vitu havipo, kimakosa vinathibitishika kuwa vipo. Hivi tunapata uhakika wa uongo kwamba vipo.
3. Kuna vitu vipo, na havithibitishiki kwamba vipo. Hivi tunataka kuvichunguza na kuvihakikisha kwamba vipo tupate uhakika kwamba vipo.
4.Kuna vitu havipo, na havithibitishiki kwamba vipo au havipo, kwa sababu havipo, na kama havipo, havithibitishiki kuwa vipo au havipo, kwa sababu falsafa ya kuthibitisha kiuhalisia (other than logical proofs such as proof by contradiction) ni kwa vilivyopo, visivyopo havithibitishiki, kwa sababu havipo.

Sasa, umetoa hoja nzuri, kwamba kushindwa kuthibitisha kitu hakumaanishi kitu hakipo. Inawezekana kitu kipo, lakini hakithibitishiki tu. Hili nalielewa na nimelielezea mara kadhaa hapa.

Lakini je, utajuaje kitu kipo, na hakithibitishiki tu, na si kwamba hakithibitishiki kuwa kipo kwa sababu hakipo?

Kabla ya uthibitisho, utajuaje tofauti?

Hatutakiwi kukubali tu kwamba kitu kipo ila hakithibitishiki tu, kwa msingi huo, mimi naweza kukuambia kwamba mimi ndiye Mungu, ila wewe kwa akili zako za kibinadamu huwezi kuthibitisha hilo, utakubali?

Zaidi ya hilo, pingamizi langu kuhusu uwepo wa Mungu si tu kwa sababu wewe huwezi kuthibitisha Mungu yupo.

Pingamizi langu kuhusu uwepo wa Mungu, hususan huyu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote ni kwamba, hoja ya uwepo wake ina internal contradiction. Uwepo wa Mungu huyu ni sawa na mtu akwambie katika Euclidean planes, kuna pembetatu ambayo hapohapo ni duara, wakati unajua pembetatu na duara ni vitu tofauti, na haiwezekani kuwapo pembetatu ambayo hapohapo ni duara.

Kwa hivyo, ninapokupa mtihani wa kuthibitisha uwepo wa Mungu, tayari najua huwezi kuthibitisha Mungu yupo.

Mungu huyu hayupo, si kwa sababu wewe huwezi kuthibitisha yupo (tushaona kuna vingine hatuwezi kuvithibitisha lakini vipo, inatuchukua miaka mingi kuvithibitisha), lakini, Mungu huyu hayupo kwa sababu dhana ya kuwepo kwake ina internal contradiction.

You can either have an omnipotent, omniscient and omni benevolent God, or have a universe in which evil is possible.You can't have both logically. The two are mutually exclusive.

And since we have a world in which evil is possible, by using the very definition of people who believe God exists, then that God does not exist.

1. Ni muhimu kuweza kuthibitisha kitu kipo, hata kama kutoweza kuthibitisha kitu kipo hakumaanishi kitu hakipo.

2. Namba 1 hapo juu ni muhimu ili tujue kwamba hatuamini kitu kipo wakati hakipo. Kwa sababu, tukisema tu kitu kipo ila hatuwezi kukithibitisha, inawezekana ikawa hatuwezi kukithibitisha kwa sababu hakipo, tukaamini kipo, wakati hakipo.

3.Muhimu zaidi, sitegemei wewe kushindwa kwako kuthibitisha kwamba Mungu yupo kama uthibitisho wangu kwamba Mungu hayupo. Uthibitisho wangu kwamba Mungu hayupo unatokana na problem of evil/ Epicurean Paradox.Wewe kushindwa kuthibitisha Mungu yupo nakuonesha umeshindwa kuthibitisha Mungu yupo kwa sababu hayupo, si kwa sababu nyingine.

Sijui kama umenielewa.
 
Kiranga ni kama Ferguson enzi zake. Ukiingia tu kwenye mfumo wake umeisha.

Ukijichanganya anakugaragaza kwa hoja ila jamaa ni mwepesi tu ukimsoma saikolojia yake ukawa mbele ya kile anachotaka kukuuliza au kukujibu. Ana misamiati mingi ila ni wa kawaida Sana kwenye hoja ihusuyo Mungu,sijui kwa nini Kuna ambao wanamgwaya Sana.
I will let Eli Walach talk for me.

"When you have to shoot, shoot. Don't talk."

 
Ulichokifanya hapa, ndicho wanachotakiwa kukifanya watu wote wanaojadiliana na Kiranga kuhusu uwepo wa Mungu. Na pengine ungekifanya mapema zaidi, na huu mjadala usingekua mrefu!

Mimi ni mmoja kati ya wanaoamini uwepo wa Mungu. Ila ni wazi, kuna cracks nyingi sana kwenye msingi uliotumika kuijenga imani ya uwepo wa Mungu. Kuna vitu vingi sana ambavyo kwa logic ya kawaida ya kibinadamu, vinapingana na ukweli kuhusu Mungu muweza wa yote na mjuzi wa yote.

Hata huko kwenye maandiko, kuna sarakasi nyingi ambazo zikijadiliwa in a logical way, zinaleta ukakasi. Ndio maana mimi nilifikia muafaka, ninaamini uwepo wa Mungu, but i can't prove it.

Ni kama ambavyo naamini kuwa kesho nitaamka salama, japo siwezi kuthibitisha. I simply can't prove my faith. Na ndio maana hata sitaki kujadili na watu wasioamini, ni kwakua wanazo sababu za muhimu kutokuamini.

Sio lazima kila mtu aamini kile ninachokiamini mimi!
Huyo Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, kuumba ulimwengu ambao watu kumjua ni shida sana, wanabishana, wanapigana vita, wanauana, kwa sababu za dini na kushindwa kukubaliana kuhusu uwepo wake, huoni kwamba ni contradiction?

Huoni kwamba huyo Mungu angekuwepo, kwa jinsi alivyo mwema, alivyo mjuzi na muweza wa yote, angejiweka wazi kwa kila mtu, kila mtu amjue bila utata, tusihitaji mtume wala msahafu, kila mtu amjue tangu anazaliwa kwa kuwekewa habari zake zote kwenye DNA isiyoharibika, kiasi kwamba watu wote wa dunia wamjue Mungu wa kweli, atuepushe na mizozo isiyoisha kuhusu uwepo wa Mungu?

Hivi, huoni kuwa that is the logical thing kwa Mungu huyo kufanya, instead of kujificha asijulikane vizuri, watu wakauana mamilioni kwa mamilioni, kutokana na vita za kidini?

Huoni kwamba, logically tu, kuwapo kwa dini tofauti, migogoro ya kidini, sintofahamu nyingi, na hata hii mijadala ya kujadili uwepo wa Mungu, ni ushahidi kwamba huyo Mungu hayupo, kwa sababu angekuwepo, mjadala kuhusu uwepo wake usingewezekana kuwepo, kwa kuwa kila mtu angejua Mungu yupo bila utata?
 
Asante mkuu.

Kiukweli binafsi sijawahi kuingia kwenye majibizano na Kiranga yahusuyo Mungu na maswala ya imani. Ila nafuatilia mijadala hii Sana miaka na miaka na Mara nyingi jamaa anawatoa Sana kamasi. Kuna mwingine wa rafiki yangu wa kuitwa Scars nae ni mtata Sana katika hizi mambo Kama kiranga tu.

Yes, majibizano ya namna hii hata Mimi siyapendi Kama wewe usivyopenda maana Mara nyingi hayafiki muafaka,kila mmoja anabaki na kuamini anachoamini. Siyo muumini wa majibizano
Majibizano hayawezi kufika muafaka kama mnajadiliana kwa imani.

Kwa sababu imani haina kanuni, mtu anaamini anachoamini tu, halazimiki kufuata kanuni.

Lakini kama tunaamua kufuata logic na facts, tunaweza kufikia makubaliano kwamba Mungu- kwa kuanzia mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote- hayupo.

Kwa sababu tunaweza kuonesha logically, kwa proof by contradiction, kwamba Mungu huyo hawezi kuwepo, by using the problem of evil and the Epicurean Paradox.
 
Gifted people ni watu ambao wamepata bahati ya Kuzaliwa kama Binadamu lakini wako AWARE NA LIFE PURPOSE YAO.

Hawa watu wako very powerful...kwa Sababu SPIRIT ZAO ZINAWALETEA MESSAGE KAMA ZINAVYOTAKIWA KUWA!

SPIRIT za watu kama hao zinapokea Communique kutoka kwa fellow beings kwa Sababu wanaweza kuzipokea.

Hawa wanaitwa Spiritual Enlightened people!

Na wanaweza kuwasiliana na Other Beings ambao huitwa A Highly Evolved Beings-Hawa wako wengi sana na wanatuzidi sana uwezo..!

So it good to read the Book!
Akina nicola tesla hawa
 
Za Biblia, Quran, vitabu vingi vya dini, zako wewe.

Ndiyo maana mpaka sasa hujathibitisha Mungu yupo.

Ukibisha, thibitisha Mungu yupo nje ya hizo stories.
Huwezi kuthibitisha uwepo wa Mungu kwa kutumia Logical Mind mkuu,since it is very LIMITED,maana utapaswa kutumia only five senses.

Je unajua kuwa kuna more than five senses? Then you have to go beyond the mind via yoga ama Meditation to explore the presence of God ama higher mystical spiritual consciousness which is UNLIMITED.
 
Huwezi kuthibitisha uwepo wa Mungu kwa kutumia Logical Mind mkuu,since it is very limited,maana utapaswa kutumia only five senses.

Je unajua kuwa kuna more than five senses? Then you have to go beyond the mind via yoga ama Meditation to explore the presence of God ama higher mystical spiritual consciousness.
Ukikataa logic, umekubali chaos.

Yani, umekubali ulimwengu ambao:-
1. Mungu yupo.
2. Mungu hayupo.
3.Mungu yupo na hayupo kwa wakati huohuo.
4. Mungu yupo na hayupo kwa wakati huo huo, lakini hilo linamaanisha yupo.
5. Mungu yupo na hayupo kwa wakati huohuo, lakini hilo linamaanisha hayupo.
6. Hayupo ni yupo, Mungu hayupo, na hilo linamaanisha yupo.
7. Yupo ni hayupo, Mungu yupo, na hilo linamaanisha hayupo
8. Mungu yupo kama hayupo.
9.Mungu hayupo kama yupo.
10.Yote hayo ya juu kwa pamoja.
 
Kama unanipinga na kusema Mungu yupo, thibitisha Mungu yupo.

Mimi reference yangu ya kwanza kuhusu kutokuwepo kwa Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote ni Epicurean Paradox.
I gat you ngoja nikuitie sipana Leo hadi akili ikukae sawa naomba twende nukta after nukta sitaki urukeuruke, wewe mzee wa epicurus philosophy kumbe unatumia Epicurean paradox ntakupangulia moja baada ya nyingine na Leo ndio utakua mwisho wako kuwasumbua watu humu
 
I gat you ngoja nikuitie sipana Leo hadi akili ikukae sawa naomba twende nukta after nukta sitaki urukeuruke, wewe mzee wa epicurus philosophy kumbe unatumia Epicurean paradox ntakupangulia moja baada ya nyingine na Leo ndio utakua mwisho wako kuwasumbua watu humu
Umeielewa kwanza?

"When you have to shoot, shoot. Don't talk"

 
Kiranga ni kama Ferguson enzi zake. Ukiingia tu kwenye mfumo wake umeisha.

Ukijichanganya anakugaragaza kwa hoja ila jamaa ni mwepesi tu ukimsoma saikolojia yake ukawa mbele ya kile anachotaka kukuuliza au kukujibu. Ana misamiati mingi ila ni wa kawaida Sana kwenye hoja ihusuyo Mungu,sijui kwa nini Kuna ambao wanamgwaya Sana.
Nishamtia za uso uko hadi kani-ignore,

Post in thread 'Maisha ya Hussein Jumbe ni ushuhuda tosha kwamba jamii zetu zina wachawi, watu wenye roho mbaya sana na makatili. Tuwe na Imani kwa Mungu' Maisha ya Hussein Jumbe ni ushuhuda tosha kwamba jamii zetu zina wachawi, watu wenye roho mbaya sana na makatili. Tuwe na Imani kwa Mungu
 
HIcho hapo
Asante sana mkuu.Japo kina page nyingi sana,na inaonekana ni kigumu sana,ni km kitabu kimoja kinaitwa Summa Theologica,kiliandikwa na Mt.Thoma wa Akwino,nacho ni kikubwa sana na ni kigumu balaa.
 
kuna pembetatu ambayo hapohapo ni duara, wakati unajua pembetatu na duara ni vitu tofauti, na haiwezekani kuwapo pembetatu ambayo hapohapo ni duara.
Wewe utawashinda wajinga wajinga tu kwa hizi hoja zako uchwara
Screenshot_20230415-043723.png
 
Urantia Book nimeisoma mara tano ,au mara kumi,au mara kumi na tano,au zaidi.
Kuhusu hiki kitabu nadhani No Comment is the best comment.
There is nothing special about the book. There are some inaccuracies.
Jambo moja ni significant. Wanasema ata the Center of creation,there an Island ,a Physical Island called "Paradise" ambako Mungu anaishi. Hili jambo linapata support kwenye Maandiko mengine .
Nilikuwa New Mexico( Marekani),nimealikwa katika nyumba ya mtu,kwenye shelf niliona pale kitabu,"How the Urantia Book was written". Hiki kitabu nakitafuta kwenye internet,sikionj,jambo ambalo linanifanya nifikirie labda Urantia Book imeandikwa na watu wahuni.
Haya mambo labda ni somewhat important lakini kama unataka spirituality labda usome Tsongkapa,The Great Ecposition of Secret Mantra au Six Yogas of Naropa.
I notice Ile posting iliyokuwepo hapa sasa hivi ya yule mtu anatrack safari za ndege ya Rais Samia imeondolewa JF. Nilikuwa nimedown ile app ya Live Flighf Tracking,nilikuwa sasa naitafuta namba ya ndege ya rais wetu mpendwa( mpendwa na Dunia yote).
Kuna hiki kingine. Kinaonesha fix zilizomo katika hicho kitabu cha Urantia.

Bahati mbaya the PDF is too large to upload here

Urantia: The Great Cult Mystery.

Author(s): Martin Gardner

Publisher: Prometheus, Year: 2008

ISBN: 1591026229,9781591026228



Description:
Well-known skeptic and acclaimed popular science writer Martin Gardner presents a complete history of the Urantia movement, from its beginnings in the early 20th century to the present day. In addition to providing an outline of the Urantia cult's worldview, Gardner presents strong evidence to establish the identity of the man whose trancelike orations formed the basis of the book. Gardner also analyzes the flaws in Urantian science and points out many instances of plagiarism in various sections of the book.In a new postscript to this paperback edition, Gardner details recent developments in the Urantia movement, corrects some errors in the original edition, and responds to critical reactions from Urantia believers to his skeptical perspective on the book and the movement.Although there are other histories of The Urantia Book, this is the only one written by a skeptic. Anyone interested in the New Age, cults, or the development of new religions will find much fascinating material in Gardner's thorough overview.
 
Nimekwambia naanza na Mungu anayesemwa na waamini Mungu, kwa mfano, wa kwenye Biblia na Quran.Huyu ana sifa za kujua yote, kuweza yote na kuwa na upendo wote.

So, kwa huyo, hayupo, kwa sababu clearly anakuwa contradicted na simple logic ya Epicurean Paradox.

Kama una Mungu mwingine, thibitisha na yeye yupo, si wa hadithi za watu tu.
Mkuu wewe mbona kichwa chako nikigumu kuelewa Nimekuuliza tunatumia logic ipi kupata maana sahihi ya Neno Mungu ?

We unasema wa biblia na Qur'an Mimi sijauliza Mungu gani nataka maana ya Mungu
Mboka akili yako Ni nzito sana!!

Ukishindwa waombe msaada kina scar wakusaidie.
 
Mkuu wewe mbona kichwa chako nikigumu kuelewa Nimekuuliza tunatumia logic ipi kupata maana sahihi ya Neno Mungu ?

We unasema wa biblia na Qur'an Mimi sijauliza Mungu gani nataka maana ya Mungu
Mboka akili yako Ni nzito sana!!

Ukishindwa waombe msaada kina scar wakusaidie.
Nimekwambia Mungu ni hadithi tu, hayupo, kila utamaduni unatunga hadithi yao ya Mungu, sasa unataka maana gani?

Yani unataka nikwambie Mungu yupo anakaa mbinguni wakati hayupo?

Nimekwambia kama unabisha thibitisha Mungu yupo.

Umeshindwa.

Kwa sababu hayupo.
 
Nimekwambia Mungu ni hadithi tu, hayupo, kila utamaduni unatunga hadithi yao ya Mungu, sasa unataka maana gani?

Yani unataka nikwambie Mungu yupo anakaa mbinguni wakati hayupo?

Nimekwambia kama unabisha thibitisha Mungu yupo.

Umeshindwa.

Kwa sababu hayupo.
Haya thibitisha kuwa maana ua neno Mungu Ni hadithi bila kuacha shaka yoyote?

Kumbe Erick shigongo huwa anatunga Mungu nzuri sana za kusisimua sivyo
 
Asante sana mkuu.Japo kina page nyingi sana,na inaonekana ni kigumu sana,ni km kitabu kimoja kinaitwa Summa Theologica,kiliandikwa na Mt.Thoma wa Akwino,nacho ni kikubwa sana na ni kigumu balaa.
vitabu vikubwa ndio vina madini ,pg,8000 soma pg 80 daily siku 100 kimeisha
 
Kuna kosa la msingi huwa unalifanya.

Kitendo Cha kuthibitisha au kutothibitisha uwepo wa Mungu haifanyi hiko kitu kuwepo au kutokuwepo.

Mfano;

Mimi nimeua Kisha nikapelekwa mahakamani kusomewa mashtka, kabla ya hukumu nikapewa nafasi ya kujitetea "nithibitishe" kwamba sijaua. Hapo mahakamani nikatoa maelezo yangu ya utetezi Kisha wakati wa hukumu Sheria ikaona Sina kosa na hivyo kuikwepa hukumu ya kifungo au kunyongwa kwa kosa la mauaji. Nimekuwa huru kwa mujibu wa Sheria.

Kwa lugha nyepesi ni kwamba, Sheria imeshindwa kuthibitisha kwamba Mimi ni muuaji(nimeua).

Ila ukweli ulio wazi ni kwamba niliua/nimeua. Ila Sheria imeshindwa kuthibitisha hivyo ikashindwa kunihukumu.

Nahitimisha kwa kusema kuwa MUNGU ANASIMAMA KAMA KWELI.MUNGU NI KWELI. Kweli inasimama Kama moja. Kweli haithibitishiki. Either unishinde kwa hoja au nikushinde,hiyo haifanyi kutokuwepo kwa Mungu.

Ni Kama uchawi tu, either uuthibitishe au usiuthibitishe haifanyi uchawi usiwepo. Uchawi upo na kupitia nguvuna matokeo ambayo binafsi nimezishuhudia kwa macho Kama mtu aliyekufa kisha kuwekwa msukule kisha kumuona akiwa mzima miaka mingi baadae ikiwa imeenda. Kama tusivyoweza kuona uchawi ila tunauona kupitia matokeo ndivyo ambavyo hatuwezi kumwona Mungu na kumthibitisha katika namna ambayo wasioamini wanataka tuthibitishe ila tunaona nguvu zake zinavyooperate.

Mungu yupo.

NB: Hili la uchawi nimechomekea tu,tusifanye kuwa mjadala.
Mungu yupo...
 
Back
Top Bottom