Hakuna mgao wa umeme Mteja, umeme upo mwingi wa uhakika na wa kutosha na hadi sasa uwezo wa kuzalisha umeme katika gridi ya Taifa umefikia Megawati 1,565.72 na matumizi ya juu ambayo yamefikiwa (peak demand) ni megawati 1,177.20, utaona kabisa kutoka hapo umeme upo wa kutosha na ziada.
SABABU ZINAZOWEZA KUSABABISHA KUKATIKA KWA UMEME
1. TANESCO itakata umeme
BILA kuwataarifu wateja endapo kuna sababu zifuatazo:-
a) Kuna mali inaungua (Mf. nyumba, kiwanda au mtambo)
b) Kuna mtu kanaswa na umeme.
c) Dharura
emergencies (imeelezwa hapo chini namba 4)
2. TANESCO itakata umeme baada ya kuwataarifu wateja -
Planned Interruptions endapo:-
a) Kuna matengenezo Kinga yaliyopangwa kufanyika ili kuimarisha miundombinu
Planned Preventive Maintanance (Mf. Kubadili nguzo zilizooza, kubadili waya chakavu, kubadili transfoma ili kuongeza uwezo wa umeme nk)
b) Matengenezo ya kila mara
Routine Maintanance (Mf. Kukata miti inayogusa line za umeme, kukagua vikombe na vifaa vingine kwenye line)
c) Kumuunga mteja mkubwa kwenye line ya msongo mkubwa wa umeme 11kV au 33kV
3. SABABU zinazoweza kusababisha umeme kukatika kwa dharura
Emergency cases nyingi ni Unplanned Interruptions
a) Za kiasilia
Natural Calamities (Mf. Radi kupiga transfoma, mvua au upepo mkali kuangusha nguzo, kukata waya, miti au minazi au matawi ya miti kuangukia line, mafuriko, wanyama kama komba, nyani, nyoka, kunguru kunasa kwenye mifumo ya umeme nk.
b) Hujuma za kibinadamu
Sarbotage
(Mf. Transfoma kuibiwa mafuta, kuibwa nyaya za umeme, nguzo kuchomwa moto na kuanguka, nguzo kubwa kuibiwa vyuma na kuanguka, magari kugonga nguzo za umeme na kuanguka, malori marefu kwenda juu kukata waya za umeme, wateja kukata miti ikaangukia kwenye line nk.
C) Uchomaji wa miundombinu ya umeme kama nguzo.
Hizi ni baadhi tu ya sababu za msingi zinazoweza kusababisha umeme Kukatika. Hivyo ieleweke kuwa sio kila KUKATIKA KWA UMEME -TANESCO wamekata ni suala pana linalohitaji kujua sababu. Wakati mwingine kwa maelezo hayo hapo juu, umeme unakatika hata TANESCO inabidi kufuatilia mifumo ili kujua sababu za kukatika.
Tunaomba umma uelewe sababu hizi na kuwa TANESCO tunaamini hakuna Mfanyakazi wa TANESCO anaweza kulihujumu Shirika kwa kukata umeme bila sababu au kukata umeme bila kufuata maagizo na utaratibu wa kukata line uliowekwa. Sio kila mfanyakazi au fundi anaweza kukata umeme. Upo utaratibu na wakati mwingine wa kimaandishi unaompa fundi ruhusa, kabla ya kukata umeme.
Tafadhali usiguse wala kukanyaga waya uliokatika au ulioanguka chini, toa taarifa Ofisi za TANESCO zilizo karibu.
Wasiliana nasi kupitia namba za simu zifuatazo: - Kitengo cha Miito ya Simu 0222194400 na 0768 985100
Tovuti:
www.tanesco.co.tz
Mitandao ya kijamii:umenijibu kisanii sana TANESCO KIBAMBA UMEZIDI HUYU MANAGER WENU HAFAI .KILA SIKU KILA SAA
Twitter,
www.twitter.com/tanescoyetu,
Facebook
https://www.facebook.com/tanescoyetultd