Kuna mdada nafanya naye kazi ofisi moja, nampenda lakini naogopa kumwambia — nifanye nini?

Kuna mdada nafanya naye kazi ofisi moja, nampenda lakini naogopa kumwambia — nifanye nini?

ChekoFagia

Senior Member
Joined
Sep 20, 2025
Posts
115
Reaction score
339
Mimi ni mfanyakazi katika moja ya ofisi hapa mkoa wa Arusha. Tunafanya kazi ambayo siyo ngumu sana, mara nyingi ni kutumia kompyuta na kushughulikia majukumu ya kila siku ya ofisi. Ndani ya mazingira haya ya kazi, kuna mdada mmoja ambaye tumekuwa tukifanya kazi pamoja kwa muda sasa.

Kwa mwanzo, mahusiano yetu yalikuwa ya kikazi tu salamu za asubuhi, kuulizana hali, na mazungumzo ya kawaida kuhusu kazi. Lakini kadri siku zilivyoendelea, nilijikuta nikianza kumfikiria zaidi ya mwenzangu wa kazi. Kila tunapokutana, napata furaha ya kipekee, na muda mwingine hata nasahau kabisa msongo wa kazi.

Changamoto yangu kubwa ni hofu. Naogopa kumwambia hisia zangu kwa sababu tunaendelea kufanya kazi ofisi moja. Najiuliza, vipi kama atanielewa vibaya? Je, hali ya kikazi itabaki kuwa ya kawaida au itabadilika? Sitaki kuvuruga mazingira ya kazi wala kumuweka katika hali ya kutokuwa na uhuru.

Je, nifanye nini katika hali kama hii? Niendelee kuficha hisia zangu na kulinda kazi yangu, au nichukue ujasiri nimwambie kwa heshima na utulivu, nikikubali matokeo yatakavyo
 
Mapenz hayana Formula.
Unaweza kudate na mtu ofisi moja na mambo yakaenda.

Swali kwanini unaogopa kumuambia?.

Alaf sikuhizi kuna kutongoza?.

Ww anza kuchat nae vizur. Mualike Lunch au Dinner siku mbil tatu (ulipie ww) . Mnunulie zawad tatu nne . Mtoe out weekend.
Ukiona ana respond vizur kwenye Haya.

Bas unaanza kumuita majina mazur mazur na akijibu kwa kukuita na ww majina hayo basi kitu imetick 😁😁😁😁😁 .

Onyo: Usitongoze kwa sms wala kwa kumpigia simu.
Date hizi za siku ya kwanza usitoe hela kumpa au kumuhonga. Atahisi una mnunua.
Ila akiwa na shida ya hela akakuomba msaada inabid umpe.

NB:
Najua ww ni kijana mdogo na ndio unakua. CODE nying hujui.
 
Kuwa na mpenzi ofisi moja ni hatari,bora umfute kichwani na kibaya zaidi akikukataa halafu wewe ulishamweka moyoni utapata tabu sana.

Fanya kazi iliyokupeleka hapo, watumie wazazi hela nyumbani, saidia ndugu, weka mipango ya kuinua uchumi wako.
 
Kwanini hauna demu mwingine nje ya ofsi unapofanyia kazi?Acha tamaa mshahara wako wote ataumaliza yeye wakati huo zake zimekaa na muda si mrefu kuna mmoja atafukuzwa kazi
😂😂😂😂
 
Kuna kitu unatafuta, na kitakupataaa.
😂😂😂😂😂
 
Mimi ni mfanyakazi katika moja ya ofisi hapa mkoa wa Arusha. Tunafanya kazi ambayo siyo ngumu sana, mara nyingi ni kutumia kompyuta na kushughulikia majukumu ya kila siku ya ofisi. Ndani ya mazingira haya ya kazi, kuna mdada mmoja ambaye tumekuwa tukifanya kazi pamoja kwa muda sasa.

Kwa mwanzo, mahusiano yetu yalikuwa ya kikazi tu salamu za asubuhi, kuulizana hali, na mazungumzo ya kawaida kuhusu kazi. Lakini kadri siku zilivyoendelea, nilijikuta nikianza kumfikiria zaidi ya mwenzangu wa kazi. Kila tunapokutana, napata furaha ya kipekee, na muda mwingine hata nasahau kabisa msongo wa kazi.

Changamoto yangu kubwa ni hofu. Naogopa kumwambia hisia zangu kwa sababu tunaendelea kufanya kazi ofisi moja. Najiuliza, vipi kama atanielewa vibaya? Je, hali ya kikazi itabaki kuwa ya kawaida au itabadilika? Sitaki kuvuruga mazingira ya kazi wala kumuweka katika hali ya kutokuwa na uhuru.

Je, nifanye nini katika hali kama hii? Niendelee kuficha hisia zangu na kulinda kazi yangu, au nichukue ujasiri nimwambie kwa heshima na utulivu, nikikubali matokeo yatakavyo
Jiue ufe KABISA, pumbavu takataka mavi
 
Back
Top Bottom