Kuna kosa lisilosameheka

Kuna kosa lisilosameheka

Aurora

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2014
Posts
7,308
Reaction score
5,275
habarini wana mmu,
kuna habari nimeisoma mahali nikaona si vibaya nikiwashirikisha ambayo imenifanya nijiulize kweli KUNA KOSA LISILOSAMEHEKA? kuna mwimbaji maarufu wa bongo flava ambae ana pesa na hata amemnunulia mama yake gari la 38 M na pia anatumia mamilioni ya pesa kwenye starehe ili hali baba yake anaumwa mguu kwa muda mrefu bila msaada wowote ikiwa ni sh milioni 1 tu ndio inayoitajika kumtibu.

Kipindi cha nyuma kidogo mwimbaji huyu aliwai kusema kuwa baba yake alimkana,na mama yake ndie aliyeangaika nae toka mdogo kwa kila kitu.
Ingawa mwenye kuhuku ni Mungu lakini kwa hisia zako hivi alifanyalo huyu mwimbaji ni sahihi au si sahihi?

Ni hayo tu,nawatakia week-end njema.

NB: kwa ambao mmeshavurugwa na foleni,kazi,stress e.t.c msi comment
 
Sio wajibu wake, ila angemsaidia ingekuwa vyema. Sio lazima kama mzazi (huenda hata sio baba yake) lkn kama binadamu yoyote ahitajiye msaada.

Ni wajibu wa mzazi kumtunza mtoto aliyemzaa, lkn ni baraka kwa mtoto kumtunza mzazi wake awapo mzee na asiyejiweza. Sasa mbaba mwenye late forties sio mzee.
 
Sio wajibu wake, ila angemsaidia ingekuwa vyema. Sio lazima kama mzazi (huenda hata sio baba yake) lkn kama binadamu yoyote ahitajiye msaada.

Ni wajibu wa mzazi kumtunza mtoto aliyemzaa, lkn ni baraka kwa mtoto kumtunza mzazi wake awapo mzee na asiyejiweza. Sasa mbaba mwenye late forties sio mzee.

kwa mujibu wa huyo baba anasema ni mwanae kabisa,ingawa ndio hivyo tena huko nyuma alimtelekeza. Ni kweli kumsaidia mzazi ni baraka
 
Thanks for being so bold, and articulate in bringing what you consider essential for consideration before anymore steps are taken in that direction.
I hope you wont only deal with EA Federation agenda, but other similar incidents both within and outside TZ, i.e extension of contract for the Container Handling Company in the DAr Port, Presidential Jet saga, Kigamboni Ferry menace, Muhimbili National Hospital state, patient refferal system to India etc!

hahaaa JF where we dare to talk openly....

sorry hayo maandishi Muhimbil federal yanatokea wapi tena
 
Hakuna , Mungu ndiye muhukumu,anapaswa kumsaidia tu,ndo maana kwa wakristo katika sala ya Baba yetu kuna kipengele kinasema tusamehe makosa yetu kama na sisi tunavyowasamehe waliotukosea, kuna nguvu kubwa sana ya kusamehe.
 
Sijui hata tunachotakiwa kukifanya hapa ni kipi na kipi sahihi

Nimeshidwa kuunganisha dots kabisa

Ngoja niwe mpole kwanza!
 
Sio wajibu wake, ila angemsaidia ingekuwa vyema. Sio lazima kama mzazi (huenda hata sio baba yake) lkn kama binadamu yoyote ahitajiye msaada.

Ni wajibu wa mzazi kumtunza mtoto aliyemzaa, lkn ni baraka kwa mtoto kumtunza mzazi wake awapo mzee na asiyejiweza. Sasa mbaba mwenye late forties sio mzee.

Kuna watu wana hasira sana .........

 
Last edited by a moderator:
Dogo anajitafutia laana,hiyo mamake hana akili ya kumshauri mwanae.
 
Hakuna , Mungu ndiye muhukumu,anapaswa kumsaidia tu,ndo maana kwa wakristo katika sala ya Baba yetu kuna kipengele kinasema tusamehe makosa yetu kama na sisi tunavyowasamehe waliotukosea, kuna nguvu kubwa sana ya kusamehe.

nakubaliana na wewe,kusamehe ni kuzuri kuliko kubeba mzigo moyoni
 
Dogo anajitafutia laana,hiyo mamake hana akili ya kumshauri mwanae.

inaelekea hata mama ni kitu kimoja na mwanae coz asingeshindwa kumsaidia yeye kama yeye
 
si ungesema tu Diamond.....

amsaidie tu sidhani ka kuna jambo atapungukiwa zaidi naona tu kuna baraka atapata.

mdomo unaponza! Lakn sio vbaya ulivyomtaja cos mm nilikuwa simjui.
Kumbe jamaa anaroho mbaya kiasi hicho!
 
Sijui hata tunachotakiwa kukifanya hapa ni kipi na kipi sahihi

Nimeshidwa kuunganisha dots kabisa

Ngoja niwe mpole kwanza!

nimetaka kujua mitazamo ya wengine pia coz mimi kama mimi naona angemsamehe na kumuachia yote mungu amsaidie baba yake wakati huu anaotafuta matibabu bila msaada wowote
 
Back
Top Bottom