Mkuu be serious. Hapa Tanzania, hakuna kiongozi mwenye utashi, nia wala jeuri ya kuvunja uhusiano na taasisi hizo. Kinachoendelea ni politiki uchwara kuwafunga kamba “wanyonge” - period.
Hata Nyerere alijua hana jeuri hiyo. Angalau alisimamia mwiko wake binafsi wa yeye kutokuwa na mkono katika makubaliano ya kushinikizwa na “mabeberu” hao; akampasia mzee ruksa urais na zigo lake la kumwaga wino kwenye makubaliano na IMF.
Tusimame na kutembea kwa miguu yetu wenyewe? Won’t happen kwenye jamii iliyojaa watu wanaoshindana kuwa wajanja, kula bata kwa sana kwa utajiri wa harakaharaka wa kufisidi dola, kuchezesha kamari, kuchuuza upako, miujiza, ulozi n.k.
Tumeachwa mbali kabisa na nchi za Asia ya mbali (China, Japan, Malaysia, Singapore, n.k.) zenye utamaduni wa kufanya kazi kwa juhudi kubwa na maarifa ambazo, pamoja na yote, hazina mpango wa kilevi wa kukorofishana na Marekani, WB, IMF.