Kuna athari zozote kama tukivunja uhusiano na WB,IMF au Marekani?

40% .... 60% iliyobakia na wahisani...


Cc: mahondaw
Kumbe kama ni kwa 40% basi tuachane nao tu. Maana bila ya kuachana nao nchi yetu itaendelea kugawanyika kati ya Vibaraka wa mabeberu na wazalendo. Nadhani tukiachana nao Tanzania itabaki na wazalendo tu wanaopambana kwa manufaa ya nchi yao!!
 
Kuvunja inawezekana lakini je tunaweza kutoboa?
Huko nyuma Mwl.Nyerere Nyerere aliwahi kuvunja uhusiano na Marekani sababu ya Rhodesia enzi za Mlowezi Ian Smith lakini haikuleta mabadiriko yoyote kwa USA haikubadirisha sera yake juu Rhodesia. Akarudisha baada ya muda mfupi.
Ila nakumbuka huyo Raisi Dr.Mwl.Julius Nyerere aliingia mgogoro na IMF, na Word Bank lakini hakuvunja.
Sababu wao ndio guarantee au ni reference ya sisi kukopa hata mabenki ya nchi nyingine.
Mara nyingi wamebadirisha madeni yetu kuwa misaada au wamefuta madeni yetu kabisa.
Kumbe ni watu wazuri. Tuendelee nao.
 
Sio kujiondoa.. Waweke vikwazo tu.. Muulize Mugabe
Kwanza lazima ujue nchi yako ipi kundi gani? In short ni nchi masikini
IMF, Ukiishiwa fedha za kigeni utanunua nini nje ya nchi kwa Tshillings?
WB inakupa tafu Sana mikopo mingi... Ingawa inakudai pesa kibao.
marekani ina piga tafu miradi mingi ikiwemo ukimwi etc.. Pia inaushawishi kwa mataifa mengi.. Ni rahisi mataifa mengine kukutaaa..
Bado hujafika kiwango cha kujitegemea... Hata hao Iran, North Korea etc wanalia Marekani iwaondolee vikwazo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi kuna jambo lolote baya litatokea kama Tanzania tukiamua kuvunja uhusiano na Shirika la fedha Ulimwenguni (IMF), Benki ya Dunia (WB), au nchi ya Marekani? Badala ya mjadala wa kuendelea ama kutokuendelea kuwa na uhusiano na taasisi hizo ama nchi ya Marekani kwa nini kama taifa tusiamue uhusiano ufe?

Maana ni kama kila wakati inakuwa ni mjadala wa nani kibaraka ama mzalendo kuelekea taasisi hizo na nchi ya Marekani. Hivi kuna ulazima wa kuwa na Mahusiano nao?

Ni wakati wa kusimama na kutembea kwa miguu yetu wenyewe!!
Kabla ya kujiuliza hilo SWALI, weka kwanza list ya mikopo na misaada tunayopewa na inakotoka. usisahau huu wa juzi wa kupambana na COVID-19... THEN BAADA YA HAPO CHECK HIYO LIST NS KAMA HAO ULIOWATAJA WAPO, BADI JUA MADHARA YAKE NI MAKUBWA.. utakosa yote yaliyosababisha tupewe mikopo na misaada
 
Hivi kuna jambo lolote baya litatokea kama Tanzania tukiamua kuvunja uhusiano na Shirika la fedha Ulimwenguni (IMF), Benki ya Dunia (WB), au nchi ya Marekani? Badala ya mjadala wa kuendelea ama kutokuendelea kuwa na uhusiano na taasisi hizo ama nchi ya Marekani kwa nini kama taifa tusiamue uhusiano ufe?

Maana ni kama kila wakati inakuwa ni mjadala wa nani kibaraka ama mzalendo kuelekea taasisi hizo na nchi ya Marekani. Hivi kuna ulazima wa kuwa na Mahusiano nao?

Ni wakati wa kusimama na kutembea kwa miguu yetu wenyewe!!
Hakuna.

As long as we have our own 'Moses' as described by Prof. wa Jalalani, Kalamaganda Kibudu.

However, as soon as we are without him, in one way or the other; ni lazima kuwarudia hao jamaa haraka. Hakuna tunachopoteza kwa kuwa nao, mradi tunajua tunachofanya.
Hawatulazimishi kufanya lolote bila ya matakwa yetu wenyewe, na kujua hali yetu ipoje, inaruhusu kukataa/kukubali masharti?
 
Huko nyuma Mwl.Nyerere Nyerere aliwahi kuvunja uhusiano na Marekani sababu ya Rhodesia enzi za Mlowezi Ian Smith lakini haikuleta mabadiriko yoyote kwa USA haikubadirisha sera yake juu Rhodesia. Akarudisha baada ya muda mfupi.
Kipimo cha "kuleta mabadiliko" kukoje mkuu sblandes'?
Unajuaje kuwa hakukuleta mabadiliko, au ulitaka siku hiyo hiyo ya "kuvunja uhusiano na Marekani" Uhuru wa Zimbabwe upatikane?
 
Baniani mbaya kiatu chake dawa..
Bosi hanuniwi..
Hata mpalestina anashindwa kuvunja uhusiano na muisraeli..
Palestinians cross border kwenda vibaruani Israel..
Tumbo tumbo lazima tulihudumie...

Everyday is Saturday.........................:cool:
 
China tu kila siku anaomba marekani amuondolee vikwazo kwenye makampuni yake na kwenye jeshi lake aweze kununua vifaa na technolojia ya kijeshi nchi za nje.

Sisi ndio tuvunje mikataba na mahusiano? Kikwazo kimoja tu njaa inatuua.
 
Back
Top Bottom