Jamani naomba kujua,
Hivi Dokta mwaka yeye anatibu akina dada zetu na wanawake tu? Nauliza hivi kwa kuwa kila nimsikiapo either Redioni or katika Runinga (TV) yeye huzungumzia tu magonjwa yanayowasibu dada, wake na mama zetu.....Mara Utamsikia sijui fibroid, mara matiti kuuma, hujakaa sawa utasikia sijui kukoma kwa hedhi, hujapumua vizuri utasikia miscarriages, hujapumzika vizuri mara unasikia sijui uvimbe sehemu ya kizazi na ukisema ukae utafakari anakuja tena sijui na mirija ya uzazi na kadhalika.
Swali langu hivi huyu Dokta Mwaka yeye hospitali yake Foreplan Herbal Clinic inatibu tu jinsia ya kike? Ina maana sisi wa kiumeni hatuna matatizo? Sisi yetu nadhani anaweza kuona ni machache ila nadhani wanaume wengi ndiyo tuna matatizo ya kufa mtu!
Naomba kuwasilisha, Jumapili njema.