Sote tunafahamu kuwa Makonda alikuja Arusha baada ya kuteuliwa kuwa mkuu wa Mkoa.
Kabla ya hapo, hakuwahi ishi zaidi ya mwaka mmoja.
Hana makazi ya kudumu.
Hajui matatizo ya watu wa Arusha na kuyasemea kwa undani kama mzawa.
Uwepo wake ni baada ya uteuzi tu, kama asingeteuliwa asingegombea Arusha kama alivyofanya Kigamboni alipokuwa Dar.
Kumruhusu Makonda kugombea Arusha baada ya kuwa mkuu wa mkoa, kutatengeneza alama mbaya ambayo mkuu wa mkoa yeyote atahakikisha kuwa anampiga vita Mbunge mzawa ili achukue jimbo, hii itatengeneza migogoro na kuchelewa kwa maendeleo katika mikoa husika.
Makonda anatakiwa aishie hapa, akiendelea zaidi ya hapa madhara yatakuwa makubwa sana kuliko akipita.