Kambi ya Fisi
JF-Expert Member
- Feb 3, 2018
- 13,525
- 22,019
Namaanisha kumpiga mkeo mangumi ama kipigo kama cha mbwa mwizi ama paka shume sio poa kabisa
Huwa ninasoma mabandko mengi hapa ambapo baadhi ya wanaume hujitapa jinsi walivyowatwanga wake zao na kuwatusi, na leo nina ujumbe kwa wote wenye tabia ya kupiga wake zao.
Ndugu yangu mpendwa, tumia mikono yako kumkumbatia, kumbembeleza na kumkanda mkeo.
Mungu alikupa misuli ya kuweza kumpelekea moto mkeo mkiwa faragha, kumwinua na kumlinda mkeo na hatari zote. Mkeo anapaswa kujisikia salama na salama zaidi mikononi mwako.
Rafiki yangu mpendwa, tumia ulimi wako kumbusu na kumbariki mkeo.
Ikiwa una matatizo huko kazini kwako Usimwagie hasira zako kwa mkeo, hata ukiwa na matatizo ya kifedha usipeleke hasira zako kwa mkeo.
Maneno ya kinywa chako yanapaswa kujaa sifa, pongezi na kutia moyo.
Ni woga ndio unaomfanya mtu kumpiga mkewe. Kwa kawaida waoga hujificha nyuma ya vurugu ili kuepuka uwajibikaji.
Jifanye kuwa bora kuliko kuwa muoga .
Kamata hii..... "mke mzuri ndiye anayekusaidia kukua na kuimarika kimwili (kiakili) na kiroho". Hivyo jionyeshe kuwa umekua na una akili kwa kutatua maswala yote kwa uangalifu.
Ubarikiwe
Huwa ninasoma mabandko mengi hapa ambapo baadhi ya wanaume hujitapa jinsi walivyowatwanga wake zao na kuwatusi, na leo nina ujumbe kwa wote wenye tabia ya kupiga wake zao.
Ndugu yangu mpendwa, tumia mikono yako kumkumbatia, kumbembeleza na kumkanda mkeo.
Mungu alikupa misuli ya kuweza kumpelekea moto mkeo mkiwa faragha, kumwinua na kumlinda mkeo na hatari zote. Mkeo anapaswa kujisikia salama na salama zaidi mikononi mwako.
Rafiki yangu mpendwa, tumia ulimi wako kumbusu na kumbariki mkeo.
Ikiwa una matatizo huko kazini kwako Usimwagie hasira zako kwa mkeo, hata ukiwa na matatizo ya kifedha usipeleke hasira zako kwa mkeo.
Maneno ya kinywa chako yanapaswa kujaa sifa, pongezi na kutia moyo.
Ni woga ndio unaomfanya mtu kumpiga mkewe. Kwa kawaida waoga hujificha nyuma ya vurugu ili kuepuka uwajibikaji.
Jifanye kuwa bora kuliko kuwa muoga .
Kamata hii..... "mke mzuri ndiye anayekusaidia kukua na kuimarika kimwili (kiakili) na kiroho". Hivyo jionyeshe kuwa umekua na una akili kwa kutatua maswala yote kwa uangalifu.
Ubarikiwe