Kumbukumbu za Majumba ya Sinema Jijini Dar es Salaam

Ng'wanamalundi

JF-Expert Member
Feb 4, 2008
1,165
1,361
Nimeona uzi hapa JF ukisifia Jumba la Senema la Empire la siku hizo, nikaona nikumbushie (na kuwajuza uzao wa dot.com) majumba ya senema yaliyokuwepo Dar enzi hizo.

Miaka ya 70 kulikuwepo na majumba sita ya senema jijini Dar. Bila kufuatilia mpangilio wa umaarufu au kigezo kingine cho chote, nayataja majumba hayo kama ifuatavyo:-

1. Empire: Hili lilikuwa mtaa wa Azikiwe mkabala na Posta Mpya.

2. Empress: Hili lilikuwa Mtaa wa Samora maeneo ya Askari Monument, likiangaliana na tawi la benki la Bank House.

3. Avalon: Hili lilikuwa Mtaa wa Zanaki, jirani na Halmashauri ya Jiji. Jumba hili lilidumu muda mrefu kushinda yote, hadi mwaka 2000.

4. New Chox: Hili lilikuwa Mtaa wa Nkrumah likitazamana na viwanja vya Mnazi Mmoja, jirani na Chinese Restaurant ambayo ilikuwa ikijulikana sana kwa 'fried rice'.

5. Cameo: Hili lilikuwa Kisutu, Mtaa wa Jamhuri, karibu na Tawi la Posta La Kisutu. Hili lilijikita katika kuonyesha senema za Kihindi. Pamoja na hayo, Waswahili walikuwa wakifurika kuangalia senema hizo.

6. Drive-In: Hili lilikuwa palipo Ubalozi wa Marekani hivi sasa. Halikuwa jumba bali uwanja wa wazi, unaingia na gari lako na unaangalia senema ukiwa kwenye gari.

Majumba hayo yalikuwa yakionyesha senema tofauti mara mbili kwa siku. Senema ya "The Ten Commandments" mwaka 1975 (or was it 1976?) ndiyo ilikuwa ya kwanza na ya mwisho kwa majumba yote sita (pamoja na Cameo) kuonyesha senema hiyo hiyo mara zote mbili kwa wiki nzima na bado watu walikuwa 'wakipigana' kuingia. Huo ni ushahidi tosha wa jinsi senema hiyo ilivyopendwa.
 
Nimeona uzi hapa JF ukisifia Jumba la Senema la Empire la siku hizo, nikaona nikumbushie (na kuwajuza uzao wa dot.com) majumba ya senema yaliyokuwepo Dar enzi hizo.
Miaka ya 70 kulikuwepo na majumba sita ya senema jijini Dar. Bila kufuatilia mpangilio wa umaarufu au kigezo kingine cho chote, nayataja majumba hayo kama ifuatavyo:-
1. Empire: Hili lilikuwa mtaa wa Azikiwe mkabala na Posta Mpya.
2. Empress: Hili lilikuwa Mtaa wa Samora maeneo ya Askari Monument, likiangaliana na tawi la benki la Bank House.
3. Avalon: Hili lilikuwa Mtaa wa Zanaki, jirani na Halmashauri ya Jiji. Jumba hili lilidumu muda mrefu kushinda yote, hadi mwaka 2000.
4. New Chox: Hili lilikuwa Mtaa wa Nkrumah likitazamana na viwanja vya Mnazi Mmoja, jirani na Chinese Restaurant ambayo ilikuwa ikijulikana sana kwa 'fried rice'.
5. Cameo: Hili lilikuwa Kisutu, Mtaa wa Jamhuri, karibu na Tawi la Posta La Kisutu. Hili lilijikita katika kuonyesha senema za Kihindi. Pamoja na hayo, Waswahili walikuwa wakifurika kuangalia senema hizo.
6. Drive-In: Hili lilikuwa palipo Ubalozi wa Marekani hivi sasa. Halikuwa jumba bali uwanja wa wazi, unaingia na gari lako na unaangalia senema ukiwa kwenye gari.

Majumba hayo yalikuwa yakionyesha senema tofauti mara mbili kwa siku. Senema ya "The Ten Commandments" mwaka 1975 (or was it 1976?) ndiyo ilikuwa ya kwanza na ya mwisho kwa majumba yote sita (pamoja na Cameo) kuonyesha senema hiyo hiyo mara zote mbili kwa wiki nzima na bado watu walikuwa 'wakipigana' kuingia. Huo ni ushahidi tosha wa jinsi senema hiyo ilivyopendwa.


Tulienjoy sana enzi hizo
Drive in tushaenda kuangalia sana
Sinema babu,kama hauna kitu unaishia nje

Watanzania waliondolewa starehe moja matata sana ingekiwepo mpaka leo hata watoto wa sahv wange enjoy

Ova
Jamaa kanikumbusha mbali sana! Kule Mbeya, kulikuwa na ENTERPRISE CINEMA. Mmiliki mwarabu, ambaye alikuja kuwekeza Dar, na kufanya namba isomeke 7 badala ya 6. Akiliita hilo jumba, STARLIGHT!
 
Drive-In ilikuwepo hadi miaka ya 90...

Pale ilipo Zantel sasa palikuwa na kisoko mjinga kama gulio hivi kila wikiendi, ni mwendo wa mchiriku wa kimakonde toka Msasani, huku wanamazingaombwe nao hawakubaki nyuma...

Mkimalizana na mchiriku, mnazunguka nyuma kule Magunia kucheck kandanda safi, halafu usiku mnarudi hapo Ilipo Zantel na ule uwanja wa mpira pembeni na Tanesco, mnashuhudia sinema za bure kwenye jiukuta lile...
 
Jamaa kanikumbusha mbali sana! Kule Mbeya, kulikuwa na ENTERPRISE CINEMA. Mmiliki mwarabu, ambaye alikuja kuwekeza Dar, na kufanya namba isomeke 7 badala ya 6. Akiliita hilo jumba, STARLIGHT!
Mkuu huyu mzee bado yupo hai?maana pamoja ya kuwa shule hakua nayo ila alikua tajiri mno,i have a story to tell kuhusu mzee huyu ila sina hakika kama angali hai,kama ametangulia kwenye haki..no siwezi kuongea maana hatakua na uwezo wa kujibia.
 
Nakumbuka Driven-In tulikua tunaenda Tiketi Mbu, kule nyuma nje mnacheki movie bila sauti huku mkipiga tangawizi na chapati au miogo.

drive in.jpg


Noma sana
 
Ilipotoka movie la cyborg nakumbuka watu tulienda kubanana kuicheki
Sema pale drive in kwa nje cinema bubu shuguli
Ilikuwa syo ndogo,kila mtu anajuaa,wakalimani wapo wa kutoshaaa

Ova

Pale Drive In walikuwa wanaongoza kuweka movie za Kihindi khaaaa...
 
Back
Top Bottom