Kumbukumbu na shukrani kwa ushirikiano

Kumbukumbu na shukrani kwa ushirikiano

Dkt. Gwajima D

Minister
Joined
Nov 28, 2015
Posts
1,706
Reaction score
8,657
Wasaalam.

Tarehe 14 Julai, 2025 nimekuwa sehemu ya Kikao cha mwisho cha Baraza la Mawaziri la Serikali ya Awamu ya Sita tangu iingie madarakani, kilichofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 14 Julai, 2025.

Picha ya 1 ni ya kumbukumbu ya Wajumbe wa Baraza tukiwa pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko na Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi Dkt. Moses Kusiluka.

Picha ya 2 nikitembea kwenye viwanja vya Ikulu ya Chamwino kuwahi Kikao husika.

Hakika, Mungu ni mwema kutuwezesha kuiona siku hii ya kihistoria⚘️🇹🇿.

Ahsanteni sana Wananchi wote na Wadau wote kwa ushirikiano wenu.

Tuendelee kushirikiana daima kuelekea Uchaguzi Mkuu hapo Oktoba 2025✍️🇹🇿.
downloadfile-1.jpg

downloadfile-2.jpg
 
binafsi navutiwa na ww kwa sababu uko karibu na jamii yako. Mungu akubariki. na ahsante kwa udhubutu.

Maana mtumishi wa Umma tena mwenye Hadhi yako Kuwepo kwenye Jukwaa la JF tena bila kificho sio jambo dogo.

Nina amini Mawaziri wenzako wako na wamejificha kwa ID fake.

Mitano ijayo unastahili.
 
Mangi, hebu tusichafue uzi wa Mh. Waziri.
Mimi huyu mama nampenda buana!
Mama ni role model kwa wanawake wengi.
Kuanzia kwenye ngazi ya familia.
Kiuongozi kama Mbunge.
na kiuongozi kama Waziri.

ningekuwa jimbon kwake ningeenda kutick. japo sina Chama. ila nakubali harakat na moyo dhabiti alionao kwenye kutumikia jamii.
 
Back
Top Bottom