Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 2,786
- 7,567
Wakuu,
Mwaka 1974, Rais Idi Amin kupitia Tangazo la Kisheria Na. 2 la mwaka 1974 alianzisha Tume ya Uchunguzi kuhusu Watu Waliopotea nchini Uganda, ikiwa ni jitihada ya kuchunguza matukio ya watu kutoweka yaliyoripotiwa tangu alipochukua madaraka kupitia mapinduzi ya kijeshi mwaka 1971. Tume hiyo ilipewa jukumu la kuchunguza matukio hayo, kubaini waliohusika, na kutoa mapendekezo ya namna ya kukomesha ukiukwaji huo wa haki za binadamu, ambapo tume hiyo lifanya kazi licha ya Wauganda wengi kuikataa na kuhoji uhalali wake.
Tume ilifanya kazi kati ya mwaka 1974 na 1975, ikiendesha vikao vya hadhara, kusikiliza ushahidi wa mamia ya waathirika na mashahidi, na kurekodi kesi mbalimbali za watu waliodaiwa kutekwa au kupotea. Katika uchunguzi wake, tume ilihitimisha kwa kulaumu vyombo vya usalama (kama jeshi), kwa vitendo vya utekaji na ukiukwaji wa haki za binadamu, bila kumhusisha moja kwa moja Idi Amin katika matukio hayo.
Ripoti ya mwisho ya tume hiyo haikuwahi kutangazwa hadharani. Badala yake, iliwasilishwa kwa Idi Amin pekee na kuwekwa kuwa siri. Hatua hiyo ilifuta uwezekano wa uwajibikaji wa wazi, kuzuia utekelezaji wa mapendekezo yoyote ya mageuzi ya vyombo vya usalama, na kudhoofisha haki kwa waathirika na familia zao.
Kwa mujibu wa taasisi za kimataifa; International Center for Transitional Justice (ICTJ) na African Transitional Justice Hub, tume hiyo ilibaki kuwa jaribio lililoshindikana la kuleta uwajibikani kwenye matukio hayo ya watu kutekwa na kutoweka.
Baada ya kumalizika kwa kazi ya tume hiyo, makamishna walitishiwa na kulengwa na dola kama hatua ya kulipiza kisasi, kwa sababu ya kuashiria uwezekano wa Amin kuhusika na kutoweka kwa watu kwa nguvu (USIP, 2009). Mwenyekiti wa tume alipoteza wadhifa wake serikalini, Kamishna mwingine alidaiwa kufunguliwa mashtaka ya uongo ya mauaji na kuhukumiwa kunyongwa, huku kamishna wa tatu akikimbia nchi ili kuepuka kukamatwa (Hayner, 1994). Inadaiwa kuwa makamishna watatu kati ya wanne walipotea. Kutokana na hali hiyo, tume hiyo haikuwa na athari yoyote au ilikuwa na athari ndogo sana kwa nchi wala kwa namna Amin alivyoendesha utawala wake hadi alipoondolewa madarakani mwaka 1979.
Licha ya Tume hiyo kutokuwa na athari yoyote chanya kwenye vitendo vya utekaji, watu kupotea na ukandamizaji mwingine wa haki za binadamu, Amin aliweza kuitumia kujionesha kama kiongozi mwenye kujali, jambo lililomsaidia kujijengea mtaji wa kisiasa. Hili linathibitishwa na kuchaguliwa kwake kuwa mwenyekiti wa Umoja wa Nchi za Afrika (OAU) mwaka 1975, mara tu baada ya kumalizika kwa kazi ya tume hiyo. Aidha, Uganda ilichaguliwa kuwa mjumbe wa Tume ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu mwezi Mei 1976 (Decker, 2013).
Source African Transitional Justice Hub
Mwaka 1974, Rais Idi Amin kupitia Tangazo la Kisheria Na. 2 la mwaka 1974 alianzisha Tume ya Uchunguzi kuhusu Watu Waliopotea nchini Uganda, ikiwa ni jitihada ya kuchunguza matukio ya watu kutoweka yaliyoripotiwa tangu alipochukua madaraka kupitia mapinduzi ya kijeshi mwaka 1971. Tume hiyo ilipewa jukumu la kuchunguza matukio hayo, kubaini waliohusika, na kutoa mapendekezo ya namna ya kukomesha ukiukwaji huo wa haki za binadamu, ambapo tume hiyo lifanya kazi licha ya Wauganda wengi kuikataa na kuhoji uhalali wake.
Tume ilifanya kazi kati ya mwaka 1974 na 1975, ikiendesha vikao vya hadhara, kusikiliza ushahidi wa mamia ya waathirika na mashahidi, na kurekodi kesi mbalimbali za watu waliodaiwa kutekwa au kupotea. Katika uchunguzi wake, tume ilihitimisha kwa kulaumu vyombo vya usalama (kama jeshi), kwa vitendo vya utekaji na ukiukwaji wa haki za binadamu, bila kumhusisha moja kwa moja Idi Amin katika matukio hayo.
Ripoti ya mwisho ya tume hiyo haikuwahi kutangazwa hadharani. Badala yake, iliwasilishwa kwa Idi Amin pekee na kuwekwa kuwa siri. Hatua hiyo ilifuta uwezekano wa uwajibikaji wa wazi, kuzuia utekelezaji wa mapendekezo yoyote ya mageuzi ya vyombo vya usalama, na kudhoofisha haki kwa waathirika na familia zao.
Kwa mujibu wa taasisi za kimataifa; International Center for Transitional Justice (ICTJ) na African Transitional Justice Hub, tume hiyo ilibaki kuwa jaribio lililoshindikana la kuleta uwajibikani kwenye matukio hayo ya watu kutekwa na kutoweka.
Baada ya kumalizika kwa kazi ya tume hiyo, makamishna walitishiwa na kulengwa na dola kama hatua ya kulipiza kisasi, kwa sababu ya kuashiria uwezekano wa Amin kuhusika na kutoweka kwa watu kwa nguvu (USIP, 2009). Mwenyekiti wa tume alipoteza wadhifa wake serikalini, Kamishna mwingine alidaiwa kufunguliwa mashtaka ya uongo ya mauaji na kuhukumiwa kunyongwa, huku kamishna wa tatu akikimbia nchi ili kuepuka kukamatwa (Hayner, 1994). Inadaiwa kuwa makamishna watatu kati ya wanne walipotea. Kutokana na hali hiyo, tume hiyo haikuwa na athari yoyote au ilikuwa na athari ndogo sana kwa nchi wala kwa namna Amin alivyoendesha utawala wake hadi alipoondolewa madarakani mwaka 1979.
Licha ya Tume hiyo kutokuwa na athari yoyote chanya kwenye vitendo vya utekaji, watu kupotea na ukandamizaji mwingine wa haki za binadamu, Amin aliweza kuitumia kujionesha kama kiongozi mwenye kujali, jambo lililomsaidia kujijengea mtaji wa kisiasa. Hili linathibitishwa na kuchaguliwa kwake kuwa mwenyekiti wa Umoja wa Nchi za Afrika (OAU) mwaka 1975, mara tu baada ya kumalizika kwa kazi ya tume hiyo. Aidha, Uganda ilichaguliwa kuwa mjumbe wa Tume ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu mwezi Mei 1976 (Decker, 2013).
Source African Transitional Justice Hub