Kumbe ulishazaa na mavirusi huenda unayo….!

Kumbe ulishazaa na mavirusi huenda unayo….!

Mtambuzi

Platinum Member
Joined
Oct 29, 2008
Posts
8,809
Reaction score
15,442
man-upset-3.jpg


Kwako mpenzi wangu wa zamani, ambaye ulinifikisha uliponifikisha kupitia utapeli wa kimapenzi ambao ulinifanyia. Kwako niliamini kabisa kwamba, nimepata mpenzi wa kweli na wa kuaminika, kumbe nilikuwa nimevaa mkenge, kama wanavyosema watoto wa mjini.

Tulipokutana kwa mara ya kwanza, Machi 16, 2002, nilikwambia ukweli wangu wote, kuhusu maisha yangu ya nyuma ya kimapenzi na hata familia yangu. Sikudanganya hata kidogo. Nawe kwa upande wako ulijifanya ati unaniambia ukweli kuhusu maisha yako, wakati ukijua kwamba, kila neno ulilotamka lilikuwa ni uongo mkubwa ajabu. Kila neno lilikuwa ni sumu ya nyoka moma.

Kwanza uliniambia kwamba, hukuwahi kuwa na rafiki wa kiume kwa sababu ya chuki yako dhidi ya wanaume. Uliniambia ati mwaka 1995, wakati ukiwa na miaka 18 ulibakwa na kijana mmoja mlipokwenda kwenye pikiniki na tangu hapo ukawa huwapendi kabisa wanaume. Nilikuhurumia na kukupa pole kutoka moyoni mwangu.

Niliona kuwa ni vizuri nikakuchukulia polepole ili unizoee na kujenga imani yako iliyopotea dhidi ya wanaume. Kwa hiyo tangu hiyo Machi 2002, sikukutajia mambo ya tendo la ndoa. Bila shaka unakumbuka kwamba, tulianza kushiriki tendo la ndoa Juni, 2002.

Siku hiyo ya kwanza ilinionesha kwamba, hukuwa mgeni wa jambo hilo, kwani ulishiriki kitaalamu sana. Nilijiambia kwamba, labda ulifundishwa unyagoni mambo hayo na uliyaweka ili uje uyatumie kwa umpendaye. Kama vile ulikuwa ukijua kilichokuwa kinaendelea kwenye kichwa changu, uliniambia kwamba, bibi yako mzaa mama alikuwa akikufundisha mambo hayo ili uje umridhishe mumeo.

Mwaka 2003, nilianza kupata taarifa zako. Nilipata taarifa kwamba, umewahi kuishi na mwanaume mwaka 1997 na mkazaa mtoto wa kiume. Niliambiwa kwamba, huyo jamaa alifariki mwaka 1999, kwa maradhi ya kifua kikuu na mwaka huo huo mtoto wenu wa mwaka mmoja alifariki pia.

Nilipata taarifa zaidi kwamba, mwaka 1999 hadi 2001, uliishi na wanaume wawili tofauti, mmoja akiwa ni Mnyarwanda. Niliambiwa mmoja kati ya hao alikuwa ni mgonjwa sana, wakati napewa taarifa hizo, na mmoja mliachana baada ya mkewe kutaka kukuuwa, kufuatia fumanizi.

Sikutaka kukurupuka baada ya taarifa hio, bali niliendesha uchunguzi wangu na kubaini kwamba yote niliyoambiwa yalikuwa ni kweli. Ndugu na jamaa zako wengi waliamua kuficha siri zako nyingi ili kukulinda uolewe, kwani ulikuwa unawaaibisha kwa tabia zako.

Nilipokuja kukupa taarifa ulilia sana, ukisema kwamba, hayo ni majungu na kuwalaani hao walionipa taarifa hizo. Baada ya kukubana sana ulikubali kwamba, taarifa zile zilikuwa ni za kweli. Bila shaka unakumbuka nilivyokuwa nimechanganyikiwa. Kwanza kwa kudanganywa, na pili kwa kuhofia kwamba, huenda ulikuwa na virusi vya ukimwi.

Ni wazi unakumbuka kwamba, nilikutimua kwa uchungu siku ile ile. Niliamua baadaye kwenda kupima afya yangu ili kujua kama nilikuwa nimeukwaa. Kwa bahati nzuri nilikwenda kupima mara mbili na kuonekana sijaathirika.

Kupitia kwako nimejifunza jambo moja kubwa, sipaswi kuamini kauli za mpenzi bila kuchunguza kuhusu anachoniambia. Pia nimejua kwamba, siyo vyote vinavyong'aa ni dhahabu.

Lakini kwa upande wako, ni kwa nini usiwe mkweli kwa nafsi yako? Kwa nini uwe na moyo mgumu kiasi hicho kwa kujipenda kupindukia? Mimi nilikuhurumia kwa kukufukuza, kuna siku mwanaume mwingine atakata shingo yako, kutokana na utapeli wako wa kimapenzi…!

Copy to: Nivea, Lisa, Mrembo by Nature, King'asti, charminglady, Elizabeth Dominic, Asnam, Paloma, amu, MadameX, Madame B, gfsonwin, BADILI TABIA, vivian, Jeska, Mamndenyi, sweetlady, FirstLady, FirstLady1, Remmy, Mayasa, mwaJ, Swts, Smile
 
mshukuru mungu wewe hilo limekwenda lilia pengine yalaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Hivi siku hizi hatupimi kabla ya kuanza mahusiano????
Unazungumzia mwaka gani Kaunga..?
Kumbuka ni miaka ya 2003, kuwa na ngoma ilikuwa ni noma maana hata ARV zilikuwa zinapatikana nchini South Africa tena kwa gharama kubwa
 
Pumzika kwa Amani rafiki zangu wapenzi na classmates, Shamila, Asha na Zaujia, pamoja na Salama walikua ni mabinti wazuri na warembo mno, kila mtu atakufa but si kwa muda waliokufa rafiki zangu hawa; walikufa wangali wanacheka, ni kama maua yalichumwa kabla ya wakati wake, na wote ilikua ni ishu ya AIDS, kati ya hao wote ni Zaujia peke yake aliekuwa amefikisha umri wa miaka 25 wakati mauti haya katili ikimkukuta.....jamani tujitunzeni.... Mtambuzi umenitonesha kidonda maana Asha na Salama vifo vyao kwa kweli kwa salimia kubwa ilikua ni tunda la ndoa za utotoni. Ntakuja kusimilia siku moja ilikuaje.....be blessed
 
Last edited by a moderator:
Ni wachache sana wanaofanya hvyo. Na wengi wao huwa hawapimi kwa sababu ya kushndwa kuwa na subira ya kusubiri kupima tena baada ya miezi mitatu.
wakati naoa nilitakiwa niende kupima HIV mmmmmhh jamani ni kazi kubwa sana usikie tu hio kitu
 
Wadanganyifu ni wengi! Ubinafsi umetujaa, tunaangalia leo tu,bila kufikiri huyu mwenzangu akijua itakuaje? Tunasahau dunia ni ndogo sana siri nyingi sio siri tena. Hofu ya Mungu imetutoka. Kwa uongo tunaua wengi. Mbaya sana.
 



Kupitia kwako nimejifunza jambo moja kubwa, sipaswi kuamini kauli za mpenzi bila kuchunguza kuhusu anachoniambia. Pia nimejua kwamba, siyo vyote vinavyong’aa ni dhahabu.

Asante Mtambuzi kwa waraka huu wenye mafunzo. Ni vyema kuwa makini kwenye mahusiano. Wakweli waliobaki ni wachache sana, lakini wengi ni wabinafsi wasio na huruma. Wanakwenda kwa marafiki zao ma-GFs/BFs na kuwadanganya kuwa wanawapenda, kumbe mwilini wamejibebea magonjwa tayari kuwatafuna wasio na hatia. Mbaya sana!
 
wakati naoa nilitakiwa niende kupima HIV mmmmmhh jamani ni kazi kubwa sana usikie tu hio kitu
Mie wazazi wa mama Ngina waliniambia waziwazi kwamba, bila kupima hakuna ndoa, tena nipime mara mbili ndio nipate ridhaa, sema tu nilishapima na kujua joto lake, haikunisumbua sana maana zile ngalambe zangu za ujanani nilishastaafu......
 
Mie wazazi wa mama Ngina waliniambia waziwazi kwamba, bila kupima hakuna ndoa, tena nipime mara mbili ndio nipate ridhaa, sema tu nilishapima na kujua joto lake, haikunisumbua sana maana zile ngalambe zangu za ujanani nilishastaafu......
hahahahaaaaa mie hata sikuwaonyesha nilienda kwa Pastor moja kwa moja maana Pastor alitaka eti atupeleke twende nae, siku hio asubuhi wakati naenda job nikapitia hospital fulani hivi nikapima fasta huku nimelowa jasho...sio kuwa labda nilikau mkorofi na mtundu No NO but yale maswali tu ya imagination yale ya ...what if.....
 
Mie wazazi wa mama Ngina waliniambia waziwazi kwamba, bila kupima hakuna ndoa, tena nipime mara mbili ndio nipate ridhaa, sema tu nilishapima na kujua joto lake, haikunisumbua sana maana zile ngalambe zangu za ujanani nilishastaafu......

Ulikuwa mjanja eeh; maana mjanja anaenda pima kwanza halafu ndio anaenda ukweni kujieleza. Kuna watu walishahama mji aisee. Wazazi wa binti mmoja wakitoa masharti kama ya wakwe zako, kilichotokea binti yao ndio akakutwa na maambukizi. Jamaa aliwashukuru sana wazazi kusisitiza kupima. Binti kahamia mwanza kwa kina Nicas Mtei ambao hawaijui hiyo story.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom