Naomba sana Jamii forums Uzi huu ikiwezekana ufikishwe Kwa ofisi ya waziri mkuu,
Tar 4 mwezi November 2022 waziri mkuu akizindua zoezi la ugawaji vishikwambi namnukuu, "kila mwalimu apate kishikwambi, idadi ya walimu tunaijua na idadi ya vishikwambi tunaijua!"
Kumbe bhana ni kama Ile kauli ya "yupo ofisini anachapa kazi zake, anawasalimia sana!"
Sasa Leo hii unaambiwa vishikwambi havitoshi na imebidi utolewe muongozo ufuatao;
1. MAELEKEZO WA MGAWANYO NGAZI YA SHULE
Vishikwambi ngazi ya Shule vigawanywe kulingana na mgawanyo wa Majukumu kwenye Taasisi husika. Aidha magawanyo huu haumaanishi wanaopewa ndio watakuwa wamiliki wa kishikwambi, kishikwambi chochote kitatumiwa na mwalimu yoyote kutekeleza majukumu ya Taasisi husika.
1.2.1 .Vipaumbele vya mgawanyo Elimu Msingi
Mwalimu Mkuu
Mwalimu Mkuu Msaidizi
Mwalimu wa Taaluma
Mwalimu wa Takwimu
Mwalimu wa Darasa la kwanza na la pili
Mhasibu wa shule(Mwalimu wa Fedha)
Aidha mwalimu mwenye majukumu yanayoingiliana atapewa kishikwambi kimoja kwa majukumu yote.
1.2.2 Vipaumbele vya Mgawanyo Elimu Sekondari
Vishikwambi Elimu Sekodari vigawanywe kwa kuzingatia mtiririko ufuatao:-
Mkuu wa shule
Makamu Mkuu wa shule
Mwalimu wa Taaluma
Mwalimu wa Malezi na Nidhamu
Mwalimu wa Takwimu
Mwalimu wa Somo la ICS(kama shule inafundisha masomo hayo)
Mhasibu
Mwalimu wa Miradi/ujenzi
Aidha mwalimu mwenye majukumu yanayoingiliana atapewa kishikwambi kimoja kwa majukumu yote!
Na hivyo ndivyo ilivyo sasa.
Naomba tena Waziri Mkuu ajitokeze kukanusha kauli yake ya kishikwambi Kwa kila mwalimu na aseme sasa ni kishikwambi Kwa kila shule!!
Vinginevyo msiwafanye walimu kama vitoto!!
Tar 4 mwezi November 2022 waziri mkuu akizindua zoezi la ugawaji vishikwambi namnukuu, "kila mwalimu apate kishikwambi, idadi ya walimu tunaijua na idadi ya vishikwambi tunaijua!"
Kumbe bhana ni kama Ile kauli ya "yupo ofisini anachapa kazi zake, anawasalimia sana!"
Sasa Leo hii unaambiwa vishikwambi havitoshi na imebidi utolewe muongozo ufuatao;
1. MAELEKEZO WA MGAWANYO NGAZI YA SHULE
Vishikwambi ngazi ya Shule vigawanywe kulingana na mgawanyo wa Majukumu kwenye Taasisi husika. Aidha magawanyo huu haumaanishi wanaopewa ndio watakuwa wamiliki wa kishikwambi, kishikwambi chochote kitatumiwa na mwalimu yoyote kutekeleza majukumu ya Taasisi husika.
1.2.1 .Vipaumbele vya mgawanyo Elimu Msingi
Mwalimu Mkuu
Mwalimu Mkuu Msaidizi
Mwalimu wa Taaluma
Mwalimu wa Takwimu
Mwalimu wa Darasa la kwanza na la pili
Mhasibu wa shule(Mwalimu wa Fedha)
Aidha mwalimu mwenye majukumu yanayoingiliana atapewa kishikwambi kimoja kwa majukumu yote.
1.2.2 Vipaumbele vya Mgawanyo Elimu Sekondari
Vishikwambi Elimu Sekodari vigawanywe kwa kuzingatia mtiririko ufuatao:-
Mkuu wa shule
Makamu Mkuu wa shule
Mwalimu wa Taaluma
Mwalimu wa Malezi na Nidhamu
Mwalimu wa Takwimu
Mwalimu wa Somo la ICS(kama shule inafundisha masomo hayo)
Mhasibu
Mwalimu wa Miradi/ujenzi
Aidha mwalimu mwenye majukumu yanayoingiliana atapewa kishikwambi kimoja kwa majukumu yote!
Na hivyo ndivyo ilivyo sasa.
Naomba tena Waziri Mkuu ajitokeze kukanusha kauli yake ya kishikwambi Kwa kila mwalimu na aseme sasa ni kishikwambi Kwa kila shule!!
Vinginevyo msiwafanye walimu kama vitoto!!