Kumbe Rwanda Bureeeeee!


Mkuu kijakazi ubishi hauna maana ebu tuelimishe vema tupe statistics nzuri kwa kuutambua uchumi wa inchi kwa kutumia matumizi ya umeme wa nchi husika compare to population, mfano kenya wako kiasi gani na matumizi yao ni ni MW ngapi na pia Tanzania, malasya, South Africa n.k.
 
Huyu mtu hajasoma uchumi, mwache! Kama RwF 630 = 1USD, na Tsh 1660= 1USD halafu mtu anasema ni bureeeee!! Hamna kitu hapo usitoke povu utajichosha bure tu!! Ukizungumzia GDP ndio unamvuruga kabisaaa!!


Mkuu siku nyingine usitumie kigezo cha exchange rate utaaibika!Kwani Pound ya Uingereza na Dollar ya Marekani ipi ipo juu? Vipi kuhusu uchumi wa nci hizo mbili upi upo juu zaidi ya mwenzake?
 
Wao c mabwege sisi ndo mabwege,wameuana wakitaka changes na kwelih wamepata na maendeleo yameonekana,fuatilia historia mataifa yote makubwa dunian apa yashawah kupigana civil war,so shingai kwa Rwanda...we kataa kubali wale wametuzidi period.
 
Huyu mtu hajasoma uchumi, mwache! Kama RwF 630 = 1USD, na Tsh 1660= 1USD halafu mtu anasema ni bureeeee!! Hamna kitu hapo usitoke povu utajichosha bure tu!! Ukizungumzia GDP ndio unamvuruga kabisaaa!!

Thamani ya pesa sio kipimo cha maendeleo ya nchi.je wafahamu yuan ngapi (china) ndo equivalent to US dollar?au Yen (Japani) ngap ni sawa na dola?halafu Kwacha ngapi (Malawi) ni sawa na dola?
Ukipata majibu haya nafikiri mkuu utakuwa umelielewa vizuri somo la Thamani ya pesa.
 
Wao c mabwege sisi ndo mabwege,wameuana wakitaka changes na kwelih wamepata na maendeleo yameonekana,fuatilia historia mataifa yote makubwa dunian apa yashawah kupigana civil war,so shingai kwa Rwanda...we kataa kubali wale wametuzidi period.


Changes zipi za kweli zimepatikana Rwanda mkuu acha kutudanganya? Nchi kuongozwa na watutsi (minority) tena kidikteta ndiyo changes za kweli hizo? Hivi unajua Muhutu anavyonyanyasika ndani ya nchi yake lakini au unaongea tu? Sasa hivi kazi maofisini na opportunities mbalimbali kama scholarships zote wanatoa kwa ukabila kama siyo mtutsi imekula kwako je hayo ndiyo mabadiliko ya kweli kwako? Unasema nchi yao inaendelea sawa sikatai lakini maendeleo yapi bora kati yetu na ya kwao ya kuua raia na kupora rasilimali za Congo D.R.C na sisi ambao kila thumni yetu tunaipata kihalali?

It's a shame Mtanzania kujishusha hivyo mpaka kujilinganisha na Rwanda (Magaidi wakuu ukanda wa maziwa makuu). Hawajatuzidi na hawatatuzidi kwa lolote kama unabisha leta data tuone wametuzidi kwa lipi.
 

Mkuu punguza Jazba,binafsi sijaona umuhimu wa huu Uzi humu jamvini bt tuendelee kupeana challenge kwa lugha nzuri.
 
Watu hawajui maendeleo ya Rwanda yako Kigari , nasisitiza jiji la Kagari tu, Tanzania tuna majiji mangapi; Kingine utajiri wa Rwanda unatokana na maliasili ya Congo wizi mtupu. Tatizo la watanzania samahani watanganyika tunapenda kusifia wezi. Mnamsifia Kagame kwa lipi wizi aghrrrraaaaa???????
 

Wakiiba wazungu ndio tunafurahi tunawapa na Ulinzi wa kutosha.
 
Tatizo natumia kilongalonga hukuna button ya like, nimelike post hii ile mbaya. Mod weke like kwenye post hii juu kwa niamba yangu
 
Tanzania ya leo utaisifia kwa lipi ndugu,km kwel wanaiba congo na wana-transform uchumi na social welfare za nchi yao,basi those guys are smart,vp sisi ambao tunaibiwa kwenye makaratasi tunasaini mikataba ya kijinga,jiulize kwa style hii tunayoendana nayo wajukuu wako watakuwa na nn,30-40 years time frm now?
 

Kwa Uchumi wa kisasa Umeme ndio kila kitu, yaani upatikanaji wa Umeme wa kutosha ndio moja ya kipimo kikubwa cha maendeleo ya nchi kwani bila Umeme hakuna kitu utafanya, hakuna uwekezaji wowote ule usiohitaji umeme, hata kufuga kuku kisasa unahitaki Umeme, umeme unabadilisha Maisha ya watu, unawakomboa watu Kiuchumi, subiri uone huu Mradi wa sasa hivi wa kupeleka Umeme vijijini (kama ni kweli) ukamilike maisha vijijini yatabadilika kabisa kutakuwa na vijana watakao jiajili kwa kuchomelea welding, wauza vinywaji baridi, wanafunzi kujisome usiku, hospitali kuhifadhi dawa, gereji, stationery n.k Umeme ndio kila kitu!

Kenya uwezo wao wa kutumia Umeme sasa hivi ni kama MW 1 000 wametuzidi kidogo tu hata sisi tunacheza hapo hapo, Afrika kusini ndio usiongelee kabisa, Afrika nzima tunazalisha MW 40 000 za Umeme ambazo ni sawa tu na Umeme unaotumiwa na nchi moja tu ya Uhispania bara la Ulaya na kati ya hizo zaidi ya asilimia 50% zinatoka AK hivyo utaona jinsi A.Kusini walivyo juu!

Hivyo Umeme ndio mambo yote, hizo nyingine zoote ni blah blah tu, ukisikia nchi fulani ina uchumi mkubwa moja kati ya vielelezo vyake angalia sehemu ya nishati wanayozalisha na ndio maana sasa hivi kuna mgogoro kati ya Ethiopia na Kenya kupitia Wazungu ambao Ethiopia wanajenga Bwawa la kuzalisha MW 10 000 wazungu hawataki wanatumia propaganda za kuharibu mazingira kwa maana wanajua Ethiopia wakiwa na huo Umeme ndio kila kitu, umaskini bai bai!

 
Development refers to an increase in national income and production of goods and services to satisfy the people needs in social services like infrastructures, health, education and financial services to the maximum national population, so it does not matter the number of people in a country as long as they acquire good social services the nation is taken as developed its the same to compare the nations like Tanzania and China in population, if Tanzania has been developed you cant say its not true by compare it with China basing on the population sense between the two countries.
 
KUNA WATU 10,000,000 KATIKA NCHI YA RWANDA NA WAKATI HUO HUO WATU 6,000,000 WAMEANGAMIA KWA MAUAJI YA HALAIKI NA KUZIKWA KATIKA ARDHI HIYO BILA SHAKA HAKA KAMA KUNGEKUWA NA MAENDELEO BADO MUNGU ATAIHUKUMU ARDHI YA RWANDA NA WATU WOTE WALIOHUSIKA !!!

mAENDELEO YOTE AMBAYO YANAKUJA BAADA YA KUUA NI HATARI NA DAMU ALIYOMWAGA KAGAME INAMULILIA MUNGU!!!
 
Ukitaka kumtafuta nyoka mulika kuanzia miguuni mwako.
 

Nakuunga mkono. Hilo jamaa linafikiria kwa (.....). Kagame na kakaye M7 they hold all the hallmarks of dictators.
 
Hivi we Kijakazi umewahi kufika Rwanda?Au umedadisi kuhusu nchi hii ndogo na ukapata linalohusu umeme ukaona umemaliza kuhusu Maendeleo ya Rwanda?
 
What's so special with Rwanda guys? Hakuna utawala wa sheria kule. Kagame is everything....aliingia kwa mtutu, hataki demokrasia, anafunga na kuua wapinzani, anachukia makabila mengine wasio watutsi, anang'ang'ania madaraka n.k. Rwanda inaongozwa na dikteta. Si mfano wa kuigwa kwa lolote.
 
Kagame ni jambazi na anajulikana kila kona ya Maziwa makuu.Juzi tu wanafunzi 16 waliomaliza kidato cha Sita Rwanda wametorokea Uganda wakihofia kuuawa na idara za usalama za Rwanda.Hii imetokea baada ya matokeo ya kidato cha Sita kutoka na vijana hao kutopata matokeo yao.Walipoamua kufuatilia wakakutana na vitisho vya kuuawa la sivyo waende kuisaidia M23 na watakuwa salama na matokeo watapata.
 
Huyu mtu hajasoma uchumi, mwache! Kama RwF 630 = 1USD, na Tsh 1660= 1USD halafu mtu anasema ni bureeeee!! Hamna kitu hapo usitoke povu utajichosha bure tu!! Ukizungumzia GDP ndio unamvuruga kabisaaa!!

GDP inachangia kujua thamani ya uchumi wa nchi sikatai,ila inapatikana kwa kugawanya pato la taifa kwa idadi ya watu,,sasa linganisha millioni kumi na millioni arobaini na tano,,mwanza pekee inatumia 43mw per day,,,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…