Kumbe Rais ndiye huidhinisha malipo ya Serikali

koryo1952

JF-Expert Member
Mar 7, 2023
381
764
Jana katika kikao cha Bunge kulikuwa na mtifuano kuwa ni nani anyeidhinisha malipo ya Serikali.

Waziri wa Fedha akajibu jibu ambalo halikumridhisha Mhe. Sendeka na Mhe. Spika akaongezea ufafanuzi kwenye majibu ya Waziri wa Fedha.

Kama ni kweli Mhe. Rais ndo anaidhinisha malipo ya Serikali basi hakuna haja ya kutumia rasilmali fedha ya Serikali kutayarisha bajeti toka ngazi za chini mpaka Bunge. Kama hilo ni kweli hakuna haja ya kuwa na vikao vya Bunge takriban mwezi mmoja na nusu.

Mimi ninavyofahamu bajeti ikiishapitishwa na Bunge kila kifungu kilichopitishwa na Bunge lazima kipate fedha iliyoidhinishwa. Pili haitakiwi kufanya matumizi nje ya bajeti iliyopitishwa na Bunge na kama kuna jambo la dharura basi jambo hilo hupelekwa tena Bungeni.

Hili la Rais kupitisha malipo ya Serikali ni jambo geni kwangu.
 
Siasa Chafu Ipo Ccm Tu
Hapo Wanasoteana Mpaka Tusahau Yote
 
Ukiona mtu yeyote anaiunga mkono ccm huyo tambua ni chanzo cha matatizo ya nchi yetu
 
Wahuni wako kazini. Acha wapige pesa za watu wasiojitambua. Watanzania ni mazwazwa.
Unayo nafasi ya kufanya watanzania wenzako wajitambue kwa manufaa ya Tanzania na watanzania kwa ujumla, tusihishie tu kusema hawajitambui?
 
Jana katika kikao cha Bunge kulikuwa na mtifuano kuwa ni nani anyeidhinisha malipo ya Serikali.

Waziri wa Fedha akajibu jibu ambalo halikumridhisha Mhe. Sendeka na Mhe. Spika akaongezea ufafanuzi kwenye majibu ya Waziri wa Fedha.

Kama ni kweli Mhe. Rais ndo anaidhinisha malipo ya Serikali basi hakuna haja ya kutumia rasilmali fedha ya Serikali kutayarisha bajeti toka ngazi za chini mpaka Bunge. Kama hilo ni kweli hakuna haja ya kuwa na vikao vya Bunge takriban mwezi mmoja na nusu.

Mimi ninavyofahamu bajeti ikiishapitishwa na Bunge kila kifungu kilichopitishwa na Bunge lazima kipate fedha iliyoidhinishwa. Pili haitakiwi kufanya matumizi nje ya bajeti iliyopitishwa na Bunge na kama kuna jambo la dharura basi jambo hilo hupelekwa tena Bungeni.

Hili la Rais kupitisha malipo ya Serikali ni jambo geni kwangu.
Fedha na rasilimali nyingine zipo chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hiyo yeye ndiye mtia saini wa mwisho wa bajeti.

Na ikumbukwe kwamba bajeti kutoka Wizara zote hupelekwa bungeni baada ya kuwasilishwa kwa Rais kwanza kupitia Wizara ya Fedha na Mipango, na ndiyo maana bajeti ikikataliwa Rais aweza kulivunja Bunge.

Kuhusu suala la kwamba vifungu vyote lazima vipatiwe fedha kwenye bajeti siyo sahihi. Kwa uchumi wetu kila mwaka huwa tunatekeleza bajeti isiyo na fedha kamili (nakisi).
 
Back
Top Bottom