Kumbe Kikwete Alianguka Pia 1997 Ubelgiji?

Akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, JK aliwahi kuzidiwa ghafla uwanja wa ndege wa Brussels nchini Ubelgiji akiwa njiani kuelekea nchini Cuba, hali iliyosababisha alazwe kwa saa kadhaa kabla ya kuruhusiwa kuendelea na safari.

Source: Tanzania Daima: 25th August 2010.

My take:

Kama habari hii ni ya kweli, Ni vema wanaoangalia afya ya Rais wakatafuta ufumbuzi wa kudumu wa tatizo hili, la sivyo litazidi kujirudia.

Kuna habari pia JK ana maumivu kidogo ya shingoni ambayo huenda aliyapata akiwa kijana kutokana na tukio kwenye Michezo au Mafunzo ya Kijeshi (Mwanahalisi; 25-31 August 2010). Ni vema wahusika waweke bayana pia ili wananchi wake wajue.

Kwa hiyo ana kifafa cha msimu au ni nini? Pole presidaaaa!!

 
afya yake hiko imara, yuko fit kuelekea magogoni


We malaria sugu vipi??? haiwezekani awe anaanguka hovyohovyo halafu useme yuko fiti. Nadhani huyu ndo rais wa kwanza kuanguka mara nyingi hadharani tangu dunia iumbwe. Na inawezekana ndo akawa wa mwisho pia. Watanzania nawashauri tumsaidie huyu mzee - apumzike (kwa kumnyima kura). Tumpe kura mtu mwenye afya imara.
 
Kamanda;

Maneno yako yanaonyesha hisia kali sana. Tumwombee pia ni Kiongozi wetu sote. Ama?

Hatuna haja ya kupoteza muda kwa Kiongozi asiyejali afya yake na badala yake anaonekana kujali kujionyesha yuko imara. Huenda ni kwa faida ya CCM tu. Hili ni Taifa na kama ni maombi yabidi tuwape Wa-Tz wanaopoteza maisha kwa kukosa madaktari Muhimbili.

Sasa hivi taarifa tulizonayo zinaonyesha madaktari wengi wako safarini kuzunguka na wanasiasa wa CCM mikoani. Hospitali imeachwa tupu.

Wangapi wanakufa kwa uzembe wa aina hii?
 
Kwa hiyo ana kifafa cha msimu au ni nini? Pole presidaaaa!!


Kifafa siyo tatizo. Ni magonjwa sawa na mengine tena yapo ya hatari zaidi. Tatizo la huyu ni kujifanya safi. Kila wakati kusema ni tatizo dogo. Mwaka 2005 kambi ya Sumaye ilitueleza tunakaribisha msiba wa Ki-taifa, hawakueleza undani wake labda ndo matokeo yake sasa pamoja na uwezo mdogo wa kufikiri unaoonekana.

Haya mambo ya kuficha kwa faida ya CCM na uchaguzi, tunaelekea kupata hata Rais zezeta huku tukiambiwa yuko fiti!
 
Back
Top Bottom