Kumbe Kibonde nae ana Point

Kibonde akiongea point ni bahati mbaya sana.

Kwa kawaida yeye ni full Pumba, tunamjua. Hata kama anazengea U-DC, ikitokea mkuu amejichanganya na kumpa basi hiyo wilaya atakayopelekwa wahesabu hawana DC ila wana MC tu.
 
Ibange, za jioni.
Nimemsikia Kibonde kwenye kipindi cha Jahazi mimi nilimsikia akiongea pumba. Kamsifia sana Makatta kwamba alisoma na mama yake! PPF zote eti ni kazi yake.
Ili ATC ifufuke katoa pendekezo ipeleke mchanganuo wa biashara TIB ili wapewe mkopo wa kununua ndege - hapo ndo niligundua ni aina gani ya akili aliyonayo Kibonde.
Kwa pamoja mle studio nilisikia wakihoji kama Mramba aliweza kulazimisha ndege ya rais inunuliwe hata kama wananchi watakula majani itakuwaje serilkali isiidhamini ATC kupata mkopo kununua ndege?

Hayo mambo ya fulani kasoma na mama yangu sio ya kuzungumzia hadharani. kwani huwezi jua pengine huyo unayemzungumzia alikua buzi la maza.
 
Nilikuwa nimeipuuza sana clouds na kibonde wake. leo nikiwa foleni namsikia kibonde anamwaga point kuhusu kufa mashirika ya umma hasa atc na bima. Wale wanaopenda kutetea magamba, hivi inakuwaje mtu binafsi anaendesha precision kwa ufanisi mkubwa atc wanashindwa? kwanini shirika kubwa kama bima linakufa wakati lilikuwa na ukiritimba. rushwa jamani magamba mmeua nchi tumechoka


Holly craaap
 
Hayo mambo ya fulani kasoma na mama yangu sio ya kuzungumzia hadharani. kwani huwezi jua pengine huyo unayemzungumzia alikua buzi la maza.

MKuu jana na Mimi nilimfuatilia sana, Alisafisha Taka Zoooote za Mataka, Na nafikiri matakataka ya mataka yameisha. Alidai kwamba Mataka akiwa NIC alikuwa anafanya kazi na mama yake na yeye ndio mahali alipomfahamia , kila alipoenda kazini kwa mama yake alikuwa akimuona. Na kwamba jamaa ni mchapa kazi sana, alikuwa NIC Katika Kitengo ambacho baadaye kilizaa PPF na Mataka akawa ndio Boss wa Kwanza Pale, Alihaidi kuwa watamuita ili wamuhoji, kwa kuwa alifanya kazi nzuri sana ya kuiota ATCL toka SAA. Lakini baadaye Mataka akaombwa tena aende akaitengeneze Bima, Kwa kazi nzuri aliyofanya ATCL.
My Take: Alitumia Nafasi ile kujitafututia ujiko kwa Mataka, Lakini pia alikuwa anamsafisha kiaina. Kwani Nani asiyemjua Mataka hapa mjini?
 
Mataka ni takataka hasafishiki ingawa anajifanya Mkapa alimuonea... Mkapa was right kumtimua cheki bobu PPF. Kumbuka enzi zake alivyokuwa anaishi maisha ya anasa ni wakati huo ufisadi ulikuwa haujakomaa alionekana mapema ufisadi wake na akashughulikiwa ipasavyo na ndicho alistahiri.
 
Nilikuwa nimeipuuza sana clouds na kibonde wake. leo nikiwa foleni namsikia kibonde anamwaga point kuhusu kufa mashirika ya umma hasa atc na bima. Wale wanaopenda kutetea magamba, hivi inakuwaje mtu binafsi anaendesha precision kwa ufanisi mkubwa atc wanashindwa? kwanini shirika kubwa kama bima linakufa wakati lilikuwa na ukiritimba. rushwa jamani magamba mmeua nchi tumechoka


Kibonde ni gamba tu, amekufurahisha nini?, mnafiki tu.
 
Kibonde anazengea u-DC baada ya kukosa ubunge wa viti maalumu ndiyo maana huwa siku zote anamsifia JK. Anakera sana huyu mbwiga.

Hiyo Wilaya itakayopewa Mkuu wa aina hiyo itakuwa imeliwa!! Any way ****** hajali anaweza kumzawadia kwa kweli!!
 
PPF kabla ya kuwa shirika kamili ilikuwa ni kitengo cha Idara ya pensheni ndani ya shirika la Bima la Taifa (NIC) enzi za Mkurugunzi Mkuu ndugu Gibbons Mwaikambo ambaye pia alama yake kuu ni ujenzi wa jengo la kitega uchumi, bima makao makuu na asilimia 90 ya majengo yote ya bima nchini yalijengwa chini ya uongozi wa Mwaikambo.

Ndugu Mwaikambo ndiye aliyemsomesha mataka na kumpandisha cheo kuwa meneja wa kitengo cha PPF ndani ya shirika la Bima. Inaelezwa kwamba Mwaikambo ndiye alipendekeza kujitenga kwa kitengo hicho baada ya kuridhika kwamba majukumu ya pensheni yanaongezeka na ndipo akakipa mtaji mkubwa na viwanja vya kujenga nyumba ya PPF house na PPF towers vilivyokuwa mali ya shirika la Bima hapo kabla.

Kwa mantiki hii ni kwamba Mataka anaonekana amefanya vizuri PPF kuliko ATC kwa sababu PPF alipewa kila kitu kutoka Bima ikiwemo wafanyakazi wa bima waliohamia PPF. Kiongozi mwenye mafanikio ni yule anayelikuta shirika linayumba na analisimamia vema hadi linaingia kwenye ushindani wa kibiashara. Kwa mfano, pale TRA aliyeleta mabadiliko makubwa ni SANARE haina ubishi na ndiyo TRA tunayoiona leo labda washindwe wengine waliokuja baada yake, NBC kuna Amon Nsekela

Mataka kusema Nyerere alimsaidia ni uongo je bila Mwaikambo kumteua pale bima kuwa mkuu wa kitengo Nyerere angemjulia wapi na leo anajitokeza kumshutumu Mkapa. Mataka asikwepe kwamba hajaacha kumbukumbu ya kutosha ATC na kama aliona kuna vikwazo kwa nini hakujiuzuru mapema amesubiri hadi anasitaafu ndipo anarusha madongo kwa mkapa na wengine.

Kibonde ana zaidi ya kuilezea jamii kuhusu mataka.
 
Nilikuwa nimeipuuza sana clouds na kibonde wake. leo nikiwa foleni namsikia kibonde anamwaga point kuhusu kufa mashirika ya umma hasa atc na bima. Wale wanaopenda kutetea magamba, hivi inakuwaje mtu binafsi anaendesha precision kwa ufanisi mkubwa atc wanashindwa? kwanini shirika kubwa kama bima linakufa wakati lilikuwa na ukiritimba. rushwa jamani magamba mmeua nchi tumechoka

hata mm nashindwa kuelewa kabisa.. that is bullshit! haiwezekani taasisi zetu zife kipumbavupumbavu tu kiasi hicho..! watanzania tusimame jamani tuikombee nchi yetu.
 
Maskini Kibonde! alikuwa anasafisha uchafu asioujua! mimi binafsi nilisikiliza kipindi hicho nilishangaa sana maana Mattaka hana cha kujivunia sana. Mattaka alipokuwa PPF juhudi zote na mafanikio yake foundation iliwekwa na Marehemu Mwaikambo, tena bora Mzee Mkapa alifanya kumstaafisha maana vinginevyo angefungwa! Ameiba sana na hali ilikuwa mbaya the only way out kumsaidia kwa vile ni mwenzetu i kumstaafisha. Cha kusikitisha washauri wa JK nadhani walikuwa likizo ndio maana akateuliwa ku-restructure NIC ambako amekwenda kuharibu kuliko lilivyokuwa. Ameshirikiana na mafisadi kaka akina mama Bukuku kuajiri ndugu zao wasio na uwezo wala experience ya NIC na kuwaacha wakongwe, wachapakazi na wanaojua mali za NIC zikoje ili wapate kula vizuri. Leo hii NIC ipo ICU, wamegawana nyumba na kupeana kama zawadi. Vitega uchumi vyote vya NIC vipo vipo tu. Poor Tanzania!
 
kama mataka ni mbunifu basi wakati wa ku-restructure NIC tungemuona mafanikio yake. wengi walijidanganya kwa kuwa kabla ya PPF alitokea ndani ya shirika la Bima kwa hiyo wakaamini atalifufua bila kukumbuka kwamba baada ya Mwaikambo hakuna mtanzania mwingine aliyeweza kuendesha shirika hilo kwa mafanikio makubwa. Mwaikambo ndiye alikuwa mtanzania wa kwanza kuwa mkurugenzi mkuu wa bima Tanzania. Baada ya Mwaikambo wakaja mwengine kama Magani, Lubambe, Temu hawakupata mafanikio. Jambo la msingi tukumbuke kwamba Mwaikambo aliondoka Bima ikiwa matawi ya juu sana nchini. Bima ilikuwa katika viwango vya juu ikishindani na NBC wakati huo kwa viwango vya ubora wa kwanza na pili nchini. Leo hii Mataka anarusha vijembe kwa Mkapa wapi na wapi?
 
Mimi naona mataka amevuna alichopanda, kwa wale wanaomfahamu mataka enzi zake alikuwa yuko peponi, akishinda disco bila kujali wadhifa wake, akiimbwa kwenye nyimbo kwa kipaji chake cha kufadhili bendi za muziki wakati huo huo ni mwajiliwa wa serikali. hata kama alikuwa analipwa vizuri basi inaonekana malipo hayo yalimzidi kimo akaanza kukufuru.

Mataka akiwa Mkurugenzi wa PPF mwenye magari ya kazi ya kisasa ambayo pia yalikuwa ya anasa yalitoa huduma nyumbani na kazini ingawa kwa wadhifa alikuwa anastahiri kupewa magari hayo lakini bado unanunua wa magari binafsi wa benzi la anasa, Nissan Patrol ya anasa na gari lingine nimesahau jina lake xxxx la anasa sio rahisi kupona na tuhuma kipindi cha mkapa.... naona Mkapa alikuwa sahihi.
 
daah! kibonde kama anasoma hii thread basi inabidi ajirekebishe manake comments almost zote mpaka saa hii, ni negative kwake. this is not a good image kabisa.

he has to change.
 
Shida ya kibonde mungu kamjalia kusema hatoi fursa kwa wengine kwenye kipindi cha jahazi wakasema anatawala jukwaa lakini pia ajifunze kuwa msikilizaji kwa wenzake anaweza kupata kujifunza mengi toka kwa wengine. Lakini aache mtindo wa kusema namjua fulani na fulani na yule ni rafiki yangu na huyu kafanya kazi na mama hiyo inatupa sisi kumpika vizuri comments zake kama zinatoka moyoni au ni za kujigonga.

Unafahamu mtu kufanya kazi na mama yako usije dhani unamfahamu vyema wapo ambao wanaweza kuwa wanamfahamu mtu huyo zaidi yako kibonde.... kusimama leo kumtetea mataka unaonyesha jinsi usivyomfahamu vizuri
 
Sa... Kibonde ambaye ni dada ya Eflahim kibonde yuko PPF na aliajiriwa na mataka enzi hizo mnategemea atamsema vibaya Mataka? Huyo ni dada yake wa damu kwa mama na baba mmoja. ndio maana ana jeuri ya kumwita mataka jahazi kusema upupu wakati amesitaafu ajisafishe.
 
Back
Top Bottom