Ndugu wanaJF, nilikuwa Algeria kwa wiki moja hivi na huko nimeonana na baadhi ya Watanzania, ambao wameamua kufanya kazi huko kuliko kurudi Tanzania kwa kile walichodai "viongozi wetu ndio wanaorudisha maendeleo nyuma".
Nilipokuwa naongea nao, walinithibitishia kuwa huko Algeria elimu ni bure hadi chuo kikuu, kinachotakiwa ni juhudi za mwanafunzi tu. Hata allowance ya wanafunzi ni hela nzuri tu. Pili, walisema hata huduma za afya zinapatikana vizuri zaidi kuliko Tanzania ila wana utaratibu kwamba wanalipia 20% ya gharama, kwa namna ambayo inawafanya wapate huduma hiyo bila shida na bila ubaguzi wala ruhwa.
Walisema kila wakikutana na viongozi wa Tanzania huwa wanawauliza kwa nini wasijifunze baadhi ya mambo yanayoenda vizuri Algeria na kuyafanya Tanzania - mfano uchimbaji wa madini unaoinufaisha nchi yetu.
Nimeona niliseme hili kwani wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu baadhi ya viongozi wa CCM walidai hakuna nchi duniani inayotoa elimu bure (badala ya kusema hawajui kama kuna nchi duniani inayotoa elimu bure).
Nilipokuwa naongea nao, walinithibitishia kuwa huko Algeria elimu ni bure hadi chuo kikuu, kinachotakiwa ni juhudi za mwanafunzi tu. Hata allowance ya wanafunzi ni hela nzuri tu. Pili, walisema hata huduma za afya zinapatikana vizuri zaidi kuliko Tanzania ila wana utaratibu kwamba wanalipia 20% ya gharama, kwa namna ambayo inawafanya wapate huduma hiyo bila shida na bila ubaguzi wala ruhwa.
Walisema kila wakikutana na viongozi wa Tanzania huwa wanawauliza kwa nini wasijifunze baadhi ya mambo yanayoenda vizuri Algeria na kuyafanya Tanzania - mfano uchimbaji wa madini unaoinufaisha nchi yetu.
Nimeona niliseme hili kwani wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu baadhi ya viongozi wa CCM walidai hakuna nchi duniani inayotoa elimu bure (badala ya kusema hawajui kama kuna nchi duniani inayotoa elimu bure).