voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,553
- 11,885
Ni kitambo sasa tangu tumuone akiwa bega kwa bega na Rais Samia kwenye ziara za kimataifa, kama inavyopaswa kuwa.
Na Pia katika shughuli zingine za kidiplomasia, ndani ya nchi kama tulivyokwishazowea. kumuona.
Mara ya mwisho hadharani, kama sikosei ilikuwa ni kwenye ziara ya Rais Samia kwenda kuhutubia Baraza la umoja wa Mataifa nchini Marekani.
Huyu ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nchini Tanzania.
Kidiplomasia anawajibika kuwepo kwenye shughuli zote za Kiserikali, zinazohusiana na Diplomasia na mahusiano ya kimataifa. Pale anapokuwepo Rais kwenye ziara za nje ya nchi.
Hata huyo JK...kilichompatia uzoefu na hadi kuwaaminisha watanzania kwamba angeweza kuongoza nchi hii.
Alianzia huko huko kwenye ziara za Mzee Mkapa (R.I.P).
Liberata Mulamula alianza kwa kasi na kuwa na vyombo vya habari mara nyingi,akiitolea taarifa mbalimbali Serikali kupitia Wizara yake na matukio husika.
Lakini kuanzia kwenye Royal Tour, hatukumuona tena na badala yake tulimuona Bwana Hassan Abbas na wengineo akiwemo Zuhura Yunus.
Hali imeendelea hivyo na hata ziara zilizofuatia hivi karibuni.
ikiwemo ya Uganda na sasa huko Ghana.
Tunaomba mwenye kujua nini kilichomsibu waziri wetu.
Atuwekee hadharani, kwa sababu huyu ni kiongozi wa umma na anapaswa kuwepo kwenye eneo lake la kazi kwa mujibu wa sheria na katiba.
Na Pia katika shughuli zingine za kidiplomasia, ndani ya nchi kama tulivyokwishazowea. kumuona.
Mara ya mwisho hadharani, kama sikosei ilikuwa ni kwenye ziara ya Rais Samia kwenda kuhutubia Baraza la umoja wa Mataifa nchini Marekani.
Huyu ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nchini Tanzania.
Kidiplomasia anawajibika kuwepo kwenye shughuli zote za Kiserikali, zinazohusiana na Diplomasia na mahusiano ya kimataifa. Pale anapokuwepo Rais kwenye ziara za nje ya nchi.
Hata huyo JK...kilichompatia uzoefu na hadi kuwaaminisha watanzania kwamba angeweza kuongoza nchi hii.
Alianzia huko huko kwenye ziara za Mzee Mkapa (R.I.P).
Liberata Mulamula alianza kwa kasi na kuwa na vyombo vya habari mara nyingi,akiitolea taarifa mbalimbali Serikali kupitia Wizara yake na matukio husika.
Lakini kuanzia kwenye Royal Tour, hatukumuona tena na badala yake tulimuona Bwana Hassan Abbas na wengineo akiwemo Zuhura Yunus.
Hali imeendelea hivyo na hata ziara zilizofuatia hivi karibuni.
ikiwemo ya Uganda na sasa huko Ghana.
Tunaomba mwenye kujua nini kilichomsibu waziri wetu.
Atuwekee hadharani, kwa sababu huyu ni kiongozi wa umma na anapaswa kuwepo kwenye eneo lake la kazi kwa mujibu wa sheria na katiba.