Wakuu, habari zimeenea huko shinyanga kuwa mkuu wa mkoa mteule wa mkoa wa Shy bw. L. Mwananzila amehamishwa leo kwenda mkoa wa Lindi na mkuu mpya wa mkoa ameripoti leo mchana. Habari za kuamika kutoka kwa mtu aliyepo Shinyanga katika viwanja vya Shycom ambako maadhimisho ya miaka 50 yanafanyika kimkoa amesema ameona makundi ya watu wakiwa wanajadili juu ya uhamisho huo wa ghafla.
Wengi wakihusisha uhamisho huo na kauli yake aliyoitoa akiwa bungeni ya kuwatimua wasukuma kutoka jimboni mwake huko Rukwa.
Nawasilisha
Wakuu,
Kuna jamaa yangu mmoja anaishi Mjini Shinyanga amenipa taarifa muda si mrefu kuwa yule Mkuu mpya wa Mkoa wa Shinyanga aliyeteuliwa hivi karibuni Mhe. Mwananzila amehamishwa na kupelekwa mkoa wa Lindi.
Nasikia wanabadilishana na mkuu mpya wa Mkoa wa Lindi.
Mabadaliko haya yanatokea hata mwezi haujaisha tangu hawa jamaa wafike kwenye ofisi zao mpya.
Kulikoniiiii!!!!?????
WanaJF naomba kufahamishwa kidogo kama kuna mtu anafahamu; hivi Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga aliyeteuliwa hivi karibuni anaitwa nani?
Kweli kabisaLudovick Mwananzila.NEXT TIME Ugoogle tu.huna haja ya kuuliza JF,swali kama hili
Ludovick Mwananzila.NEXT TIME Ugoogle tu.huna haja ya kuuliza JF,swali kama hili
Anaitwa Ludovick Mwananzila. Alikuwa Mbunge wa Kalambo (Mkoa wa Rukwa) kabla ya kuangushwa kwenye kura za maoni uchaguzi uliopita. Aliwahi pia kuwa naibu waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi kwenye baraza la kwanza la Mkwer'e.
Swali jingine?!!
Mungu wangu wote mmekosa jawabu sahihi!!!! Mnatakiwa muwe mna google kila baada ya dakika kumi!! Mambo katika nchi hii hayatabiriki!!
du. Wewe uko nchi gani. Mwananzila ni mkuu wa mkoa wa lindi
kumbe ni kitendawili?
ngoja nipite kwanza.
Na aliyeteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Lindi amefika tu hata kabla hajakabidhiwa ofisi akahamishwa kwenda Shinyanga!!
Afadhali Polisi!! Watu hawako nchini wanajibu maswali ya mitego bila kufikiri kwanza!! Sina hakika kama Mwananzila amewahi kuikanyaga Shinyanga kama Mkuu wa Mkoa!! Na aliyeteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Lindi amefika tu hata kabla hajakabidhiwa ofisi akahamishwa kwenda Shinyanga!! Sijui hata kama vyombo vya habari vinalijua hili!
Unaambiwa siku nyingine uwe una google!! Watu wanaamini kila kitu kinapatikana kwenye google!! Hii ni Tanzania, leo unasimamishwa kazi kesho unarudishwa kwa mamlaka aliyopewa anayekuridisha lakini kabla hujakaa sawasawa inakuja mamlaka nyingine inakurudisha likizo!!
Ally Nassoro