Kimbunga
Platinum Member
- Oct 4, 2007
- 14,941
- 9,947
WanaJF naomba kufahamishwa kidogo kama kuna mtu anafahamu; hivi Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga aliyeteuliwa hivi karibuni anaitwa nani?
Wakuu, habari zimeenea huko shinyanga kuwa mkuu wa mkoa mteule wa mkoa wa Shy bw. L. Mwananzila amehamishwa leo kwenda mkoa wa Lindi na mkuu mpya wa mkoa ameripoti leo mchana. Habari za kuamika kutoka kwa mtu aliyepo Shinyanga katika viwanja vya Shycom ambako maadhimisho ya miaka 50 yanafanyika kimkoa amesema ameona makundi ya watu wakiwa wanajadili juu ya uhamisho huo wa ghafla.
Wengi wakihusisha uhamisho huo na kauli yake aliyoitoa akiwa bungeni ya kuwatimua wasukuma kutoka jimboni mwake huko Rukwa.
Nawasilisha
Wakuu,
Kuna jamaa yangu mmoja anaishi Mjini Shinyanga amenipa taarifa muda si mrefu kuwa yule Mkuu mpya wa Mkoa wa Shinyanga aliyeteuliwa hivi karibuni Mhe. Mwananzila amehamishwa na kupelekwa mkoa wa Lindi.
Nasikia wanabadilishana na mkuu mpya wa Mkoa wa Lindi.
Mabadaliko haya yanatokea hata mwezi haujaisha tangu hawa jamaa wafike kwenye ofisi zao mpya.
Kulikoniiiii!!!!?????