Na mwandishi wetu wa kugandia(embedded journalist)
Kaka wa fedha taslimu wa JF Ville au (CMB) alinukuliwa "Serikali kushindana na JF"
Kwa kile ambacho kimewashangaza vijana na watoto wengi JF Ville ni pale bubu mmoja kuongea ! Bubu huyo alisikika akisema "Hawatakuwa na mafanikio makubwa" na ndipo shilingi iliporushwa kuona upande mwingine wa serikali na ndio ilipobainika kuwa DNF(Daily New-Forum) Danganyika!
Mda mchache baada ya vuguvugu hilo kuanza mwandishi wetu alinukuu "nani mjinga atakwenda kupost kwenye site ya serikali na issue serious?" Aliuliza mwanahudhuria mmoja wa JF Ville. Naye mwanhudhuria mashuuri (m-the great) alidai DNF ni propaganda "Dunia ya hoja yenye msingi na ukweli siku zote hujitenga na Propaganda"
Mda mwingine haukupita kwani kombora aina ya ‘rpg' ilipigwa DNF na kusema haita acha hata chembe moja ya huko! Mlio huo wa kombora hilo uliwaamsha wanavijiji wa JF Ville na kuona ni rahisi zaidi kupigana makombora hayo kwa kujiunga nao-" naenda kujiunga nao nione" alisikika mwanakijiji mmoja huko... Wakati huo huo ngurumo za kombora hiyo ilimtoa nyoka gamba shimoni mwake na kusema "halafu nimecheki list yao" mwandishi wetu alibaini.
Wasanii JF Ville hawakuwa mbali kwani michango yao ya sayansi kwenye midahalo huitajika…wasanii waligundua kwa kufanya uchunguzi wa taipureta kuwa wana DNF(Danganyika[sic] News Forum) kuwa sio asili "niliwaambia…sio mwenzetu ana asili…angalieni typings..." Ulibainisha uchunguzi huo wa kisanii. Hii iliwafanya watanzania waishio huko JF Ville kuanguka kicheko "kwi kwi kwii"
Tahadhari: "Tangu nijiunge JF nimekuwa kiakili na sasa nategemea kuoa karibuni" Haija julikana kama ni ndoa ya Mwana JF na Mwana DNF au ya JF na DNF.
Nayo nyota moja huko JF Ville ilingara pale ilipoonyesha wazi jiko la DNF na kuonekana vyakula havipakuliwi na vimejaa nyongo! "Natumaini watakuwa…bila kinyongo" alinukuliwa. Naye mwanahudhuri wa kujisafisha alisema DNF ina wasaliti ambao aliwataja kwa ‘ID zao kede kede'([sic])
Umahiri wa kike wa kiafrika haukupitwa, kwani alifanya utafiti kwa kutumia supa(office)kompyuta kuona nguvu ya DNF na kubainika "Wana system kali sana" hata hivyo alisitisha zoezi hilo kwa kile alichoamini kuwa JF Ville kuna "Protection ya ID's za membaz wake." Bila ya kueleweka tahadhari nyingine ilitolewa kwenye mdahalo huo "JF, hiyo kuweni macho," kilieleweka.! Wanakijiji nao, waliogopa, pale walipogundua "wana system kali sana" na kujihoji.
Tahadhari hizo ziliendelea kutapakaa JF Ville na kufikia JF Ville forest reserve, Nyani huko aliuliza kama watu wanajua majina yao…alijiuliza na kujijibu "labda uwe unaishi kwenye kisiwa…" alijijibu na kuona! Lakini kwa kile kilichomshangaza mwandishi huyu ni kule Nyani huyo kula babaiku kila wikiendi. Hii ilimwacha hoi mwandishi huyu alipobainisha hayo na kujiuliza, ‘Nyani hula babaiku'? Kwi
Mwandishi wetu pia alibainisha kuwa maarifa ya JF ni kuwa tayari na madongo "niko huko tayari…NITWAPA madongo…" alibainisha. Maarifa hayo yalipigwa ki-mkumbo!
Mjadala huo uliendelea mpaka pale mainjinia wa DNF walipoomba dua na ushauri "sisi tukiwa kama IT-technicians ‘Danganyika News Forum' tufanyeje?" Dua lake lilijibiwa na kuonyeshwa picha ya jinsi gani wafanye!
Wakati mwandishi huyu akirudi mtamboni wanahudhuria na wanaharakati DNF walidai
Insurbordination imefanywa , mwandishi wetu amepelekwa huko kutuletea kisa mkasa.
Kwa habari zaidi bofya hapa……
Na hapa....