Kukiri

Kukiri

makenze

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2014
Posts
356
Reaction score
217
Nimeona nitumie ukurasa huu kukiri kwamba kuna kaka kazini nimetokea kumpenda sana mpaka yeye mwenyewe amejua na yeye kaanza kunipenda

Ni mdogo kwangu kiumri na mimi ndo nilimpokea kazini.

Mwanzoni sikuwahi hata kumuweka akilini mwangu hata kidogo yaani wala kumuwaza,ila hivi karibuni baada ya yeye kuwekwa kwenye idara yangu aisee natamani kila saa nimuone

Na yeye nahisi ananijali kuliko kawaida kwani amekua akinisaidia kazi nyingi sanaaa tena bila kumuomba.ananijali sana
Ki ukweli hali ya yeye kunisaidia kazi nyingi ndo imepelekea nikamuelewa sana.

Sasa sijui kama yeye ananipenda au mimi ni mawazo yangu na kijana hana hata hayo mawazo.

Kuna siku tunapiga stor nikamuuliza kama ana mpango wa kuoa akasema hana kabisa.

Mpaka naandika hii stor ni kwamba leo wakati ananielekeza jambo flani alinishika mkono bila sababu na nilijihisi tofauti sana.

Niliona kabisa jamaa ananipenda na sio uongo.

UBAYA NI KWAMBA NIMEOLEWA na ubaya mwingine ni kwamba mume wangu ndo boss wetu.

Naogopa moyoni na nahisi kumsaliti mume wangu kihisia

Sihitaji hata kukutana nae tena japo haiwezekani maana tunaonana mara kwa mara.
Nafanyaje wandugu
 
Nimeona nitumie ukurasa huu kukiri kwamba kuna kaka kazini nimetokea kumpenda sana mpaka yeye mwenyewe amejua na yeye kaanza kunipenda
Ni mdogo kwangu kiumri na mimi ndo nilimpokea kazini.
Mwanzoni sikuwahi hata kumuweka akilini mwangu hata kidogo yaani wala kumuwaza,ila hivi karibuni baada ya yeye kuwekwa kwenye idara yangu aisee natamani kila saa nimuone
Na yeye nahisi ananijali kuliko kawaida kwani amekua akinisaidia kazi nyingi sanaaa tena bila kumuomba.ananijali sana
Ki ukweli hali ya yeye kunisaidia kazi nyingi ndo imepelekea nikamuelewa sana.
Sasa sijui kama yeye ananipenda au mimi ni mawazo yangu na kijana hana hata hayo mawazo.
Kuna siku tunapiga stor nikamuuliza kama ana mpango wa kuoa akasema hana kabisa.
Mpaka naandika hii stor ni kwamba leo wakati ananielekeza jambo flani alinishika mkono bila sababu na nilijihisi tofauti sana.
Niliona kabisa jamaa ananipenda na sio uongo.
UBAYA NI KWAMBA NIMEOLEWA na ubaya mwingine ni kwamba mume wangu ndo boss wetu.
Naogopa moyoni na nahisi kumsaliti mume wangu kihisia
Sihitaji hata kukutana nae tena japo haiwezekani maana tunaonana mara kwa mara.
Nafanyaje wandugu
Pole sana.
Naona kijana akiharibu kazi muda si mrefu.
 
Na ubaya ni kwamba utakuwa sababu ya kijana kupoteza kibarua chake maskini! Kama mumeo ni mtu anakupenda na anakujali sioni sababu za wewe kupata hisia za kimapenzi kwa mwanaume mwingine shouger tulia na ndoa yako km inakupa heshima na thamani sjui hujaona kule MLIMA WA MOTO mabinti wanavohangaika kutafuta ndoa BILA DALILI??
 
Na ubaya ni kwamba utakuwa sababu ya kijana kupoteza kibarua chake maskini! Kama mumeo ni mtu anakupenda na anakujali sioni sababu za wewe kupata hisia za kimapenzi kwa mwanaume mwingine shouger tulia na ndoa yako km inakupa heshima na thamani sjui hujaona kule MLIMA WA MOTO mabinti wanavohangaika kutafuta ndoa BILA DALILI??
Thanx dear.namjali mume wangu sijawahi kumsaliti.hizi hisia tu zinaniuzunisha kwani nahisi kumsaliti tayari.
Naona kama namkosea Mume wangu na Mungu.
Natamani niziondoe kabisa
 
Jambo Dogo Sana, Mitala Ruksa Hata Kwa Wanawake Jitahidi Sana Uwe Nao Wote, Mumeo Na Huyo Best Looser
 
Hao ndio wanawake ukiona mtu haoi wala hana mpango huo hata usimuulize kwanini.
 
Back
Top Bottom