Galacha Maestro
JF-Expert Member
- Sep 29, 2011
- 1,353
- 2,231
KUKAA NA KINYONGO NI KUENDELEA KUJITESA TU
Ni kwamba unakosa nafasi ya kufuatilia mambo mengine muhimu kwako.Unaweza kujiaminisha kwamba kinyongo ulichomwekea mtu unastahili kabisa.
Alininyanyasa sana nilipokuwa mdogo, alinitesa sana katika mapenzi/ndoa, alinisababishia hasara kubwa kwenye biashara yangu, alisababisha kifo cha mtu muhimu sana kwangu na sababu nyingine nyingi unazojipa kwamba kuweka kinyongo kwa mtu ni haki yako kabisa.
Lakini hebu niambie, kwa kuwa na kinyongo hiko kumekusaidia nini mpaka sasa? Je alichokufanyia mtu huyo kipindi hiko kimebadilika?
Kukaa na kinyongo ni kuendelea kujitesa, kujinyima nafasi ya kufanya mambo ya msingi kwako na yatakayokupeleka kwenye mafanikio na kinyongo hiko hakikusaidii wewe wala yule ambaye umemwekea.
Ni kwamba unakosa nafasi ya kufuatilia mambo mengine muhimu kwako.Unaweza kujiaminisha kwamba kinyongo ulichomwekea mtu unastahili kabisa.
Alininyanyasa sana nilipokuwa mdogo, alinitesa sana katika mapenzi/ndoa, alinisababishia hasara kubwa kwenye biashara yangu, alisababisha kifo cha mtu muhimu sana kwangu na sababu nyingine nyingi unazojipa kwamba kuweka kinyongo kwa mtu ni haki yako kabisa.
Lakini hebu niambie, kwa kuwa na kinyongo hiko kumekusaidia nini mpaka sasa? Je alichokufanyia mtu huyo kipindi hiko kimebadilika?
Kukaa na kinyongo ni kuendelea kujitesa, kujinyima nafasi ya kufanya mambo ya msingi kwako na yatakayokupeleka kwenye mafanikio na kinyongo hiko hakikusaidii wewe wala yule ambaye umemwekea.