sijui nina damu ya kunguni!,yaan kla safar lazma nikae na kizee au kiajuza,duu ni noma 2pu!
kwasababu gani hupendi kukaa kwenye basi na mwanamke mwenzako?
hahahaha umenikumbusha nilipanda na mama wa kisukuma. Ye anafkiri wote tunajua kisukuma basi mwanzo mwisho ni "hii bhabha umekujamooh-jashilaga! telakawiza getegete"
Jaman mamdenyi tupe experience huu si ndo ukumbi wenye we tufungukie
Mimi SINA BAHATI kabisa yaani ukitangulia kwenye seat utaashangaa kitakacho kuja! Akiingia binti mzuri unasema labda ndio hyu anapita huyooooooooooooooooooo! Halafu inakuja ndume moja au maza fulani kapakata kuku wakinenyeji ana watoto kama wa 3 hivi. Patamu
HaHAHAHAAHAHAAAAAAA!!!Umenichekesha sana, halafu ana watoto wote hao anachukua siti moja, pia anakuomba msaada wa kumsaidia kubeba mmoja, mkifika kati kati ya safari anakukojolea, halafu yule mama anachukua khanga yake chafuuuu anakufuta nayo huku anakuomba msamaa, sijui utafanyaje?
wanawake hawapendani, huo ndiyo ukweli jumapili iliyopita nilikuwa safarini gari likawa limejaza sana kuna dada mmoja akaanguka nadhani anamatatizo ya moyo basi tulijikuta wanaume kama wanne tuna mhangaikia kama kumkalisha tulipokuwa tumekaa sisi huku tukimpepea wangine wakimumwesha maji wengine wakifungua madirisha maana pamoja na gari kujaza watu walikuwa wamefunga madirisha mpaka anapata fahamu yule dada hakuna mwanamke aliesogeza pua...kwa uzoefu wangu nikosafiri halafu nilie kaanae awe chadema basi safari yangu huwa njema sana kwanza tunatungumzia maisha, siasa, biashara...nikikuta -------- yaani ccm nitaomba kuhamishwa maana kama natoka Arusha naenda mbeya ama Mwanza njiani naweza mtandika makofi hasa nikijionea watu wanavyoteseka mikoani...
Booking officers huwa nawaambia kabisa wanipe siti atayokaa mrembo, kwa style hii nishawapata wawili na mmoja nategemea kumuoa
MKUU huyo lyassa inawezekana ndo huyohuyo wiseboy so usimind sana.Kwenye gazeti la leo la Mwanaspoti kuna makala ya mwandishi (Lyassa) ambayo amenakili maelezo ya wiseboy na wachangiaji wengine kana kwamba ni utafiti wake.