Kujitoa CWT na kujiunga CHAKAMWATA

Kujitoa CWT na kujiunga CHAKAMWATA

Weka namba yako,mi niko nachingwea,mwalimu na tutakuwa pamoja mkuu
 
Naamini CWT ni mafisadi tena sana,ila siungi mkono hoja yakuanzisha chama kipya,badala yake nashauri ya fuatayo:
1.Katiba ya CWT ipitiwe upya ili kubaini mapungufu na kuyarekebisha.
2.Mapato ya chama yawekwe bayana na matumizi yake.
3.Ifanyike Auditing KATIKA mali za CWT na repoti ipelekwe kwa wanachama ikajadiliwe
4.Makato ya mshahara yapungue na kuwa kiwango kimoja km vile 2,000/=kwa mwezi kuliko asilimia hiyo 3 au 2inayokatwa sasa hivi kwani:
i.Chama kina rasilimali nyingi kwa sasa tosha kuendeshea chama
ii.Chama kina ingiza wanachama wengi kwa mwaka kutokana na ajira za walimu takribani 25,000 kila mwaka walimu wapya huajiriwa,hivyo michango ya fedha ni nyingi.
iiii.Kiwango cha asilimia 2 au 3 inayokatwa sasa siyo lazima,kwani kiwango hicho kilipangwa wakati chama kikiwa kichanga na kinahitaji mapato mengi kujiendesha,kwa sasa kiwango hicho ni kikubwa.
5.Mfumo wa kuwatunza wanachama wastafu uangaliwe upya,kwani si haki mwanachama amekichangia chama kipindi chote cha utumishi halafu akistaafu aishie kupewa bati 20,atafanyia nini? bati 100 angalau na inawezekana,au apewe mkono wa kwa heri 1,500,00 0/=
6.Mikutano ya mara kwa mara na wanachama na viongozi wakuu iwe inapatiwa kipaumbele nk.
Haya ni mambo machache ya kushughulikia na wengine wanaweza kubainisha na mengine,changamoto hizi zikitatuliwa chama ni kizuri,
Kubomoa nyumba unayoishi na kujenga mpya kwa mara moja si jambo jepesi.
Pia ili kujitoa kutoka chama kilichopo na kujiunga na chama kipya bila kubainisha changamoto zilizopo katika chama cha awali ni kazibure.Utajuaje kama chama kipya hakitakuwa na matatizo?
Karibuni kwa maoni.
CWT ni tawi la CCM, hakuna jipya
 
Hilo nalo ni jipu kwa waalimu na linatakiwa kutumbuliwa. Hivi mnajua pesa zinazopatikana kwa mwezi zinafanya nini na zinakuwa edited kivipi? Nitarudi kesho kuchangia vizuri
 
Hilo nalo ni jipu kwa waalimu na linatakiwa kutumbuliwa. Hivi mnajua pesa zinazopatikana kwa mwezi zinafanya nini na zinakuwa edited kivipi? Nitarudi kesho kuchangia vizuri
 
Naomba nikusahihishe mahesabu hayawezi kuwa edited badala yake yanakuwa audited.CWT kama zilivyo taasisi nyingine zinakaguliwa na internal auditors lakini tuchukue katiba ya CWT tuisome tuweze kujua mgawanyo Wa madaraka na kazi za viongozi na kamati ni zipi.Wewe kwenye kituo cha kazi kuna Mwakilishi Wa CWT ambaye ni mjumbe Wa mkutano Mkuu Wa CWT Wilaya je, ulishamwomba mchanganuo hata Wa bajeti ya Wilaya kabla yakuikimbilia taarifa ya fedha ya taifa?CWT inahitaji marekebisho madogomadogo lakini ni mkombozi Wa walimu.Benji ya walimu inaanzishwa may na nafasi za kazi zimeshatangazwa ukute kuna walimu kwenye sifa za kibenki wamekaa kulalamika halafu mje mseme hamkupata taarifa.
 
Wewe unaye sema walimu ni mburura you should come back to your senses otherwise you know not what you are talking.
 
bora mjitoe tu maana hakunq namna nyingne
 
Hakuna MTU ambaye hapendi kula cha msingi kufanya uchunguzi na kutoa maamuzi yako ya kipekeee peer group nomaaa
 
Kumbuka kila siku mtawala anafurahia anapoona migogoro katika vyombo vya ushirikishwaji. Hili sio geni kwetu tunaliona katika vyama vya siasa! Wingi wao unamfanya mwenye madaraka aendelee kuitawala nchi. Kwa, hili mnalotaka kulifanya linaweza likawa sio suluhisho bali kuongeza suluba kwa mwalimu.
Hebu fikiri, mwalimu amehama CWT baada ya siku kadhaa huko alipohamia ukizuka mgogoro (Na mara nyingi pale furusi inapoongezeka) anakuwa katika kizungumkuti na hajui pa kwenda. Kwa yakini kabisa, je, mtakuwa mmemsaidia au mmempotosha mwalimu pindi mtakapoanza migogoro ya kiuongozi katika hicho chama kipya? Je, mmeshindwa kuwaondoa viongozi wa CWT waliopo madarakani?
Nia yangu sio kutaka kuwakwaza ila natoa angalizo kwa hili wazo mnalotaka kulifanya.
Mkuu njooni na huku Mara....tupo wengi tungependa kujiondoa kwa huyu kupe mnyonyaji...cwt...

Sapoti ipo ya kutosha ...ikiwezekana tuwasiliane tuone namna ya kushirikiana katika hili...

Moja ya mambo yanayoniumiza ni hili la cwt kukata mshahara wangu bila idhini yangu....na sioni msaada Wao kwangu...wamekuwa ni tawi la serikali hivo hawawezi kututetea tena....

AMKENI WALIMU WENZANGU...TUNANYONYWA NA HUYU KUPE
 
Kujitoa siyo rahisi! Tatizo lenu walimu mnapenda kutymika sana, mkishapewa kiposho cha 20,000/= huwa mnasahau shida zenu! Kwa ufupi ni sekta yenye mburula wengi sana pamoja na kujidai kwamba mnajua vitu lakini nyie ni mburula viongozi wa mburula wote!
 
Tupo wengi huku Mwanza tunahitaji sana tu kujitoa kwenye hili dubwasha la cwt
 
Back
Top Bottom