Kujishusha!!.....

Unalipiza kisasi cha Manu nini? naona masuali magumu kama interview ya Pentagon! heheh

Bek to suali lako: Unajua jambo lolote linalohusu mahusiano kwanza unapaswa umuelewe mwenza wako zaidi kuliko kujielewa mwenyewe, Kuna mwenza anaweza akaabyuzi udhaifu wako na kuna mwenza anaziba udhaifu wako kwa kujirekebisha.

Sasa kama una mwenza ambae anatafuta udhaifu wako autumie basi utahitajika kujishusha pale umefanya kosa tu na pia kwa tahadhari kwani anaweza akalitumia kosa lako kukuhukumu milele. Ila kama mwenza wako unapojishusha anaonesha kubadilika kutokana na kujishusha kwako basi ni vyema ukajishusha hata pasipobidi kujishusha na nakuhakikishia mwenza wa namna hii mwisho atajifunza kwako kujishusha na mwisho mtakuwa mnagombaniana kujishusha.

I might be wrong! Leo nina njaa ajabu pointi hazikuji.

Kloro umeniacha hoi..bado nina usongo na wewe, kichapo kiko akili yani kila saa magoli ya Barca yana-replay:))

Senkyu kwa mtazamo wako, hii idara umetulia kweli na unatoa ushauri wa nasaha ipasavyo haswa ukila vizuri..kweli hamna kitu kibaya kama kuchezea udhaifu wa mwenza wako, njia sahihi na kumuelewa mwenza na ku-deal nae kutokana na udhaifu wake mana ni ngumu kubadilika mara moja.

Kitu ambacho tunajisahau watu wengi ni kuweza ku-accomodate udhaifu wa wenza wetu..mana kwa njia moja ama nyingine kila mtu ana udhaifu wake ambao unaweza kuwa kikwazo kwa mwenzie, je unamsadiaje? au ndiyo mtu akishaujua anauchezea kwasababu anajua 'which button to press' ?!!!..

Ukale sasa kabla hujaanza kuota mchana kwa njaa!!



kukumbushia kosa kunakujaje? tatizo kuna mwenza mwingine yuko too vulnerable with the same kosa! sasa kama ur past kila siku ina-catch up na ww, namaanisha kila wakati unafanya kosa lile lile ila unabadili mtindo lazma utakumbushiwa tu. na hakuachi walau ukasahau,anakuchakachua tena!inakera kukumbushwa lakini ukirudie kosa, utakumbushwa tu somehow! na kuomba msamaha kila mara kwa kosa lile lile (tena kosa strategic,hahaha,with clear planning and repeatitive,lol!), inakuwa haileti maana ya msamaha kamwe!

Kabisaa, kosa lile lile lazima likumbushiwe mana lina historia inayofanana hata kama lilitokea mwaka mmoja nyuma..ila ikiwa ni kitu tofauti ni ngumu sana kukumbushia..maana ya msamaha ni kutorudia same kosa. siyo kujiwekea akilini kuwa nitaomba msamaha tena ya yataisha, no uzito at all!!


jamani mimi gf wangu ni mbish kupitiliza, na hata akikosea hawezi kujishusha au kusema sory hata cku, instead anakugeuzia kosa kwmba we ndio mkosaji, hapa 2lipo 2mefight nachukia sana anapokosea then anakugeuzia kosa. Hivi wanawake wote mko ivi? Je inakuaje kwny ndoa m2 anakaa na mtu 50yrs wanakaaje kama ndo mko ivi?

Pole Sailor..sasa weweu umetambua wazi udhaifu wa mwenza wako. kwani mkiwa mnabishana kitu wewe nawe unakuwa juu? mana inabii uje na technique tofauti sasahivi yani kama anapenda kubisha na wewe unaendelea kusisitiza, inabidi sasahivi akianza kubisha ukae kimya na kumwacha ajione mshindi..halafu mkiwa kwenye muda na maongezi mazuri umwelezee wazi kuwa 'dear ulikosea hiki na kile na jitahidi kukubali unapokoea' halafu uone reaction yake hapo...
Wanawake wote hatupo hivyo, hivi vitu ni baadhi ndugu yangu..
 

humble.png
"...aint too proud to beg for forgiveness!" Leo nimeikumbukia hii mada ya kujishusha. Kabla sijapandisha Uzi, nimekutana na hii ya BJ,..nikajionea si vibaya tukumbushane mawili matatu..
 
Wanawake wachache sana ambao ukijishusha
na kuomba msamaha hata kama kosa ni lake ,mambo yanakwisha na kuwa mazuri...

Wanawake walio wengi ukijishusha na kuomba msamaha.....

1.anakupanda kichwani na kuongeza ujeuri

2.anahifadhi hilo kosa,na kila siku utakumbushwa kuwa

alikusamehe kosa siku fulani.....

I prefer kuomba msamaha kwa vitendo....

Zawadi hivi,au out ya nguvu......

...Dahhh, Mw'Mungu anijaalie asiye na kibri hiko....

Ha ha BlackBerry, you're one in a million!!..nadhani linapokuja suala la kukumbushia, ni ngumu kwa binadamu kusahau kila kitu sema kuna wengine wamezidi kukumbushia yani badala ya kuishi maisha ya sasa kila siku mpo past tense.

...kuna wengine huandika kwenye Diary!...siku mkitibuana tu anatafuta 'Reference!'

mimi kama siko kwenye mood ya ugomvi
hata kama sina kosa naomba msamaha....

Tatizo wengine ukiomba msamaha unajipalia makaaa

Nimekusamehe lakini sitokusahau aliimba nani tena???

Unaomba msamaha hata kama kosa si lako ndo solution mambo yaishe na maisha yaendelee mbele

...hivi hii ndio ile 'basi yaishe!,' au inakwenda deep kabisa kiasi cha kutamka 'samahani, nimekosa, nisamehe?'
Ukimzoesha mwenza yeye tu kushinda kesi, siku ya siku hata haki ikiwa yako utadhulumiwa tu.
Ni aheri kuuma na kupuliza.
 
Hello wapendwa,

Kwa wapenzi/wanandoa linapotokea suala la mifarakano ya hapa na pale mpaka wengine kutaka kuachana, mnalichukuliaje suala la kujishusha? Hapa naongelea kuwa chini (kupunguza hasira/jazba) na kuweza kurudisha amani kwa kuanzisha maongezi au/na kuomba msamaha.

Pia, ukiwa na mtu asijependa kujishusha ilhali kakosea unakabiliana vipi na hali hii? Mana kuna mtu hakubali kosa yao wala kuomba msamaha hata kama amekosea.

Wimbo mahususi:- Ain't Too Proud To Beg - The Temptations

Siku njema katika kulijenga Taifa!...
sasa hapo ishu inakuja nani aanze, ukikuta wote mangangari ndo hakitaeweka kabsaaaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
sasa hapo ishu inakuja nani aanze, ukikuta wote mangangari ndo hakitaeweka kabsaaaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
<br />
<br />
Hii style mbaya sana, yaani kila mtu anakuwa anajiona kuwa ana haki kuliko mwenzake na hawatakaa wasolve tatizo kwa mtindo huu. Kujishusha ni jambo zuri sana kama mkitaka ugomvi wenu uishe salama. Kinachotakiwa mtu asiangalie eti akijishusha basi ndo atadharauliwa na mwenzake, hapana just do it for ur love then baadae mtaongea taratibu na kwa ustaarabu basi mambo yanaisha. Kwanza mnakuwa mmesave hata muda wa kujadili mambo mengine ya muhimu zaidi.
 
Hii Mada iko so sensitive kwangu mwe!!..................................BDA hiyo taktic ikizoeleka itakuumiza
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
sasa hapo ishu inakuja nani aanze, ukikuta wote mangangari ndo hakitaeweka kabsaaaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Halafu unakuta mmoja akiwa juu anaweza kuongea maneno ambayo yakampandisha hasira ambaye alidhamiria kujishusha..mnajikuta wote juu..
Inahitaji moyo sana na kujizuia kw ahali ya juu..!
 
1. Kuomba msamaha hata kama kosa si lako inawezakuwa njia nzuri ya kumaliza hacra zake kwa wakati huo. But hii inatakiwa iwe na follow-up plan yaani utafute siku mko vizuri uclear whatever mlichokuwa mnagombana (Hapa nitaambiwa una-bank makosa) Potelea mbali lakini ni vema mkawekana sawa kwani haichelewi kuwa kawaida - yaani akajua akifanya makosa utakiri wewe na kisha imetoka. Unamzoesha

Kama wengine ni one in a million wewe ni one in a billion(one in a million of those who r one in a million)
-Nothing to add have I
 
kWENYE MAHUSIANO AU NDOA KAMA msamiati WA KUJISHUSHA/ KUSAMEHE hautakuwepo au hautatumika , Hapo itakuwa shida kwa mahusiano hayo kudumu
 
Nani aseme samahani loo !!
Nimejitahidi sana "MAMA YAISHE BASI"

Kwahiyo na wewe ukikosewa na kuambiwa ''mpenzi yaishe basi'' unaonaje??
Maana kuna siku unakosea na kuna siku utakosewa..Zingatia hilo!!
 
Back
Top Bottom