BelindaJacob
Platinum Member
- Nov 24, 2008
- 6,474
- 4,022
- Thread starter
- #81
Unalipiza kisasi cha Manu nini? naona masuali magumu kama interview ya Pentagon! heheh
Bek to suali lako: Unajua jambo lolote linalohusu mahusiano kwanza unapaswa umuelewe mwenza wako zaidi kuliko kujielewa mwenyewe, Kuna mwenza anaweza akaabyuzi udhaifu wako na kuna mwenza anaziba udhaifu wako kwa kujirekebisha.
Sasa kama una mwenza ambae anatafuta udhaifu wako autumie basi utahitajika kujishusha pale umefanya kosa tu na pia kwa tahadhari kwani anaweza akalitumia kosa lako kukuhukumu milele. Ila kama mwenza wako unapojishusha anaonesha kubadilika kutokana na kujishusha kwako basi ni vyema ukajishusha hata pasipobidi kujishusha na nakuhakikishia mwenza wa namna hii mwisho atajifunza kwako kujishusha na mwisho mtakuwa mnagombaniana kujishusha.
I might be wrong! Leo nina njaa ajabu pointi hazikuji.
Kloro umeniacha hoi..bado nina usongo na wewe, kichapo kiko akili yani kila saa magoli ya Barca yana-replay)
Senkyu kwa mtazamo wako, hii idara umetulia kweli na unatoa ushauri wa nasaha ipasavyo haswa ukila vizuri..kweli hamna kitu kibaya kama kuchezea udhaifu wa mwenza wako, njia sahihi na kumuelewa mwenza na ku-deal nae kutokana na udhaifu wake mana ni ngumu kubadilika mara moja.
Kitu ambacho tunajisahau watu wengi ni kuweza ku-accomodate udhaifu wa wenza wetu..mana kwa njia moja ama nyingine kila mtu ana udhaifu wake ambao unaweza kuwa kikwazo kwa mwenzie, je unamsadiaje? au ndiyo mtu akishaujua anauchezea kwasababu anajua 'which button to press' ?!!!..
Ukale sasa kabla hujaanza kuota mchana kwa njaa!!
kukumbushia kosa kunakujaje? tatizo kuna mwenza mwingine yuko too vulnerable with the same kosa! sasa kama ur past kila siku ina-catch up na ww, namaanisha kila wakati unafanya kosa lile lile ila unabadili mtindo lazma utakumbushiwa tu. na hakuachi walau ukasahau,anakuchakachua tena!inakera kukumbushwa lakini ukirudie kosa, utakumbushwa tu somehow! na kuomba msamaha kila mara kwa kosa lile lile (tena kosa strategic,hahaha,with clear planning and repeatitive,lol!), inakuwa haileti maana ya msamaha kamwe!
Kabisaa, kosa lile lile lazima likumbushiwe mana lina historia inayofanana hata kama lilitokea mwaka mmoja nyuma..ila ikiwa ni kitu tofauti ni ngumu sana kukumbushia..maana ya msamaha ni kutorudia same kosa. siyo kujiwekea akilini kuwa nitaomba msamaha tena ya yataisha, no uzito at all!!
jamani mimi gf wangu ni mbish kupitiliza, na hata akikosea hawezi kujishusha au kusema sory hata cku, instead anakugeuzia kosa kwmba we ndio mkosaji, hapa 2lipo 2mefight nachukia sana anapokosea then anakugeuzia kosa. Hivi wanawake wote mko ivi? Je inakuaje kwny ndoa m2 anakaa na mtu 50yrs wanakaaje kama ndo mko ivi?
Pole Sailor..sasa weweu umetambua wazi udhaifu wa mwenza wako. kwani mkiwa mnabishana kitu wewe nawe unakuwa juu? mana inabii uje na technique tofauti sasahivi yani kama anapenda kubisha na wewe unaendelea kusisitiza, inabidi sasahivi akianza kubisha ukae kimya na kumwacha ajione mshindi..halafu mkiwa kwenye muda na maongezi mazuri umwelezee wazi kuwa 'dear ulikosea hiki na kile na jitahidi kukubali unapokoea' halafu uone reaction yake hapo...
Wanawake wote hatupo hivyo, hivi vitu ni baadhi ndugu yangu..