Michelle
JF-Expert Member
- Nov 16, 2010
- 7,621
- 3,514
Kila mtu aishi maisha yake na afanye maamuzi kutokana na kile anachoona sahihi kwenye maisha yake....kwangu mimi sidhani kama ni kujidanganya mtu kuona watu wanaoishi pamoja kabla ya ndoa kama wanakosea....katika kila kitu binadamu tunaongozwa na misingi fulani kama dini,elimu,tamaduni...na si lazima tuwe perfect kwenye hiyo misingi ndo uunge/kutounga mkono hoja fulani fulani....
Hakuna ndoa iliyo perfect,wala haitakaa iwepo....haijalishi mliishi pamoja mkajuana sana kabla ya ndoa au hamkuishi,changamoto ziko pale pale...vishawishi na vikwazo viko tu na vinashamiri kila siku....kusema ndoa za siku hizi zimejaa unafiki,sijui ni za siku zipi ambazo hazikuwa na unafiki......manake kukiuka viapo vya ndoa ni kitu kimekuwepo tangu enzi hizo...mapungufu ya kwenye ndoa si unafiki,ni matokeo ya kuishi binadamu wawili ambao wote wamepungukiwa utukufu wa Mungu na wana tamaa...
Sijidanganyi wala simdanganyi muumba wangu anayeona sirini kwa kupinga kuishi pamoja kabla ya ndoa....kutokuishi pamoja kabla ya ndoa hakunifanyi mimi/wala yeyote mkamilifu ila nina sina budi kujitahidi kadri ya uwezo wangu kutii na kufuata taratibu za dini ninayoiabudu....na tamaduni nilizolelewa....
Hakuna ndoa iliyo perfect,wala haitakaa iwepo....haijalishi mliishi pamoja mkajuana sana kabla ya ndoa au hamkuishi,changamoto ziko pale pale...vishawishi na vikwazo viko tu na vinashamiri kila siku....kusema ndoa za siku hizi zimejaa unafiki,sijui ni za siku zipi ambazo hazikuwa na unafiki......manake kukiuka viapo vya ndoa ni kitu kimekuwepo tangu enzi hizo...mapungufu ya kwenye ndoa si unafiki,ni matokeo ya kuishi binadamu wawili ambao wote wamepungukiwa utukufu wa Mungu na wana tamaa...
Sijidanganyi wala simdanganyi muumba wangu anayeona sirini kwa kupinga kuishi pamoja kabla ya ndoa....kutokuishi pamoja kabla ya ndoa hakunifanyi mimi/wala yeyote mkamilifu ila nina sina budi kujitahidi kadri ya uwezo wangu kutii na kufuata taratibu za dini ninayoiabudu....na tamaduni nilizolelewa....