Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,800
- 59,267
Salamuni wandugu!
Swali la "kama ni sawa watu kuishi pamoja bila au kabla ya kuoana" lilishaulizwa hapa jamvini zaidi ya mara moja.Kama maswala mengine tunayojadili hapa wapo waliopinga vikali na wapo waliosapoti.
Iwe ni kwasababu wawili ndo wameamua kuishi maisha yao hivyo ama wanatumia nafasi hiyo kufahamiana zaidi wakiwa na malengo ya kuona mbeleni ikiwa wataeendelea kua kwenye ukurasa mmoja au kwa sababu nyingine yoyote ile wapingaji wengi hua wanaegemea zaidi kwenye dini.
Ohhh kwanini uishi na mtu bila ndoa???
Biblia inaelekeza watu kuona na sio kuishi kwa makubaliano.
Vipi kukiuka amri za Mungu na kuzini?
Binafsi nakubaliana na haya yote....ila kwenye maisha ya karne hii ambayo ndoa haziheshimiki wala kupewa maana na hadhi zistahilizo je ni maadili yapi hayo tunayofuata kuoana?
Ndoa nyingi za siku hizi zimejaa unafiki ....Unakuta baba ana nyumba ndogo....mara sijui katembea na dada wa kazi mpaka kumpa mimba...mama nae ana kakijana kake mtaa wa pili basi tunachoona na kutambua kama usahihi na unyoofu wa maisha kinageuka uozo.Sasa je tunapozipigia debe ndoa hizi hizi ambazo yanayofanyika ndani yake hayaelezeki na kusema au hata kufikia kuwahukumu wale wanaishi pamoja bila hizo ndoa tunakua tunamdanganya nani haswa???Sisi wenyewe na nafsi zetu au muumba wetu tunaejifanya tunafuata na kutimiza maandiko yake kwa kuoana????
Japo sisemi watu wasiendelee kuoana ila tukumbuke kwamba mtu anapooa au kuolewa hafanyi hivyo ili aonekane na ukoo...kanisa...msikiti..au majirani bali kwaajili yako mwenyewe....kwahiyo tusijidanganye kwa kuuridhisha umma huku nafsini tukijua kinachoonekana sicho. Watu wawili ambao hawajaoana mbele ya umati na kupigiwa vigelele ila wakawa wakweli na waaminifu ndani ya nafsi zao wenyewe ni bora kuliko ndoa zinazohalalishwa kwa matarumbeta zikisindikizwa na maneno ya vitabu vya dini wakati wanaoingia ndani yake si mioyo wala akili zao zilizopo kwenye hizo ndoa.
Usihukumu usije ukahukumiwa...haswa ukiwa unajua unayofanya wewe japo watu wengine wanaweza kua hawajui ni mabaya kuliko unayohukumu. Uaminifu na uzuri wa kweli ni ule unaouona wewe hata kama wengine hawaoni.....
Swali la "kama ni sawa watu kuishi pamoja bila au kabla ya kuoana" lilishaulizwa hapa jamvini zaidi ya mara moja.Kama maswala mengine tunayojadili hapa wapo waliopinga vikali na wapo waliosapoti.
Iwe ni kwasababu wawili ndo wameamua kuishi maisha yao hivyo ama wanatumia nafasi hiyo kufahamiana zaidi wakiwa na malengo ya kuona mbeleni ikiwa wataeendelea kua kwenye ukurasa mmoja au kwa sababu nyingine yoyote ile wapingaji wengi hua wanaegemea zaidi kwenye dini.
Ohhh kwanini uishi na mtu bila ndoa???
Biblia inaelekeza watu kuona na sio kuishi kwa makubaliano.
Vipi kukiuka amri za Mungu na kuzini?
Binafsi nakubaliana na haya yote....ila kwenye maisha ya karne hii ambayo ndoa haziheshimiki wala kupewa maana na hadhi zistahilizo je ni maadili yapi hayo tunayofuata kuoana?
Ndoa nyingi za siku hizi zimejaa unafiki ....Unakuta baba ana nyumba ndogo....mara sijui katembea na dada wa kazi mpaka kumpa mimba...mama nae ana kakijana kake mtaa wa pili basi tunachoona na kutambua kama usahihi na unyoofu wa maisha kinageuka uozo.Sasa je tunapozipigia debe ndoa hizi hizi ambazo yanayofanyika ndani yake hayaelezeki na kusema au hata kufikia kuwahukumu wale wanaishi pamoja bila hizo ndoa tunakua tunamdanganya nani haswa???Sisi wenyewe na nafsi zetu au muumba wetu tunaejifanya tunafuata na kutimiza maandiko yake kwa kuoana????
Japo sisemi watu wasiendelee kuoana ila tukumbuke kwamba mtu anapooa au kuolewa hafanyi hivyo ili aonekane na ukoo...kanisa...msikiti..au majirani bali kwaajili yako mwenyewe....kwahiyo tusijidanganye kwa kuuridhisha umma huku nafsini tukijua kinachoonekana sicho. Watu wawili ambao hawajaoana mbele ya umati na kupigiwa vigelele ila wakawa wakweli na waaminifu ndani ya nafsi zao wenyewe ni bora kuliko ndoa zinazohalalishwa kwa matarumbeta zikisindikizwa na maneno ya vitabu vya dini wakati wanaoingia ndani yake si mioyo wala akili zao zilizopo kwenye hizo ndoa.
Usihukumu usije ukahukumiwa...haswa ukiwa unajua unayofanya wewe japo watu wengine wanaweza kua hawajui ni mabaya kuliko unayohukumu. Uaminifu na uzuri wa kweli ni ule unaouona wewe hata kama wengine hawaoni.....