evangelical
JF-Expert Member
- Nov 21, 2011
- 5,970
- 9,901
Aisee kama unafikiria ndoa ni cheti umepotea sana.mila ipi sasa? mie nataka harus na yeye hataki pia naona kama nitapoteza muda kukaa na mtu Bila cheti hata cha ndoa
Sent from my SM-A800F using JamiiForums mobile app
Kwa mtazamo wangu mimi ndoa ni makubaliano ya hiari ya watu wa jinsia mbili tofauti kuishi kama mke na mume hadi kifo,au itapobidi kuachana kabla ya kifo.
Masuala ya msingi kwenye ndoa ni Upendo, Uvumilivu, kuheshimihana, kusaidiana na kufanya kazi halali ya kuingiza kipato.
Sheria ya ndoa ya Tanzania inatambua ndoa iliyofungwa kidini, kiserikali na kimila aidha sheria hiyo inatambua kwamba watu wakiishi kama mume na mke zaidi ya miaka 2 na kuendelea hapo ni ndoa imefungwa.
Halafu tambua kwamba ndoa ni suala la makubaliano ya watu 2 tu hakuna cha ndugu wala nini labda uwe chini ya miaka 18 ndipo inahitaji ridhaa ya wazazi au walezi kufunga ndoa .
Cheti, harusi sijui sherehe kwenye ndoa ni mbwembe tu, kama kuachwa unaachwa tu na cheti chako hata ikiwa ndoa ya kikatoliki. Wengi wameachwa na mavyeti vyao.
Mwisho nakushauri nenda kaishi na huyo jamaa cha msingi muwe manapendana, mnaheshimiana, mnavumilana,mnaingiza kipato halali inshala nakuombea mema uishi maisha marefu na ya amani kwenye hayo mahusiano na baadae ndoa yenu.
Hilo ni dhari wanaume wengi sikuhizi hatuhusudu sana kuoa wengi tunatafuta watoto tunawalea kisingle parent maisha yanaendela,
Mimi mwenyewe sijaoa lakini ikitokea nitake kuoa pamoja ni mkatoliki niliyesoma seminari kidogo niwe padri, ndoa hiyo kama kuna ulazima nitaenda kuifungia kwa DC na sio ndoa ya kanisa katoliki

usibishane nae huyo