Kuishi na mwanaume bila ndoa

Kuishi na mwanaume bila ndoa

Maisha hayana formula, kuna walioishi pamoja ndoa ikaja baadae, ila nakupa angalizo ukikubali kuishi naye jitahidi uzae. Tofauti na hapo utajikuta unapoteza muda wako bure.
 
Usidhani kua akidondoka huku akiwa kwenye ndoa ni tiketi yakuionja pepo,je ambao wako kwenye ndoa nabado wanasaliti ndoa,wao wakifa huenda peponi kisa wamefunga ndoa na waume zao ambao huwa tunawaona wanasalitiwa... ndoa siku hizi ni fasheni tu,tena wengine huwa mnafunga mkiwa wajawazito.
WANAWAKE WANAOMVUNJA MOYO HUYU DADA HAWAJAPATA HIZO NAFASI NDIO MAANA WANAMKATISHA TAMAA
 
Hiyo Ndoa unayoisema itawashirikisha Akina nani mfano akisema aje kwenu.. Kwa Mfano akasema aje huko Kwenu na Kuitikia Ombi Lako atakuja kukutana na Watu Gani kwako. Kwa hao siyo Ndugu Zako ambao ndiyo wanaohitaji Kushirikishwa. Unashindwa nini Kuwashikirikisha Hili ila upo Tayari Kuwashirikisha Ndoa?

Kwa hiyo Unatuhakikishia kuwa Wewe ni Yatima, Huna Mlezi, Huna Majirani, Huko Shuleni Huna hata Mshauri wa Mambo yako ya Kiroho?

Are you really Serious....
mimi Nina ndugu Lakin mtu wa karibu niliekua na mtrust katangulia mbele ya haki na si kila mtu anatakiwa kukupa ushauri

Sent from my SM-A800F using JamiiForums mobile app
 
Kama mama yako na baba yako waliishi kwenye ndoa na wewe ukazaliwa kwenye ndoa , na yeye wazazi wake kama walifunga ndoa iweje yeye akatae? Hivi wanaume wanaogopa nn ndoa?

Usikubali kusogezwa. Hujui ya kesho.

Mmh bila ndoa ? nimzuie mama yangu sacrament?? Hapana kabisa

Nyie viumbe kanisani mnaogopa nini?

Mungu nae ana mengi unakutana na mtu hata kanisani mwisho akumbuki alisali lini? Hawazi watoto watakuwa ktk maadali gani?

Hakuna kinachoshindikana kwa mungu saliii mungu ndo mwenye uwezo wa kumbadilisha mtu.
 
Ndugu zangu natumai hamjambo....hivi hili suala la mwanaume kumwambia mwanamke waishi bila ndoa then wafunge ndoa baadae mnalionaje.

Mimi mwenzenu niko njia panda baada ya boyfriend kusema tuishi bila ndoa.

Je faida na hasara zake hua ni zipi? kwa mliotangulia kuoa ama kuolewa naombeni msaada
Daah, usingesema boyfriend wako ungesema mzinzi mwenzio tu

Makandila
 
sahau kupata mpenzi serious

Sent from my HUAWEI P7-L10 using JamiiForums mobile app
 
Ndugu zangu natumai hamjambo....hivi hili suala la mwanaume kumwambia mwanamke waishi bila ndoa then wafunge ndoa baadae mnalionaje.

Mimi mwenzenu niko njia panda baada ya boyfriend kusema tuishi bila ndoa.

Je faida na hasara zake hua ni zipi? kwa mliotangulia kuoa ama kuolewa naombeni msaada
nia ni kuwachunguza zaidi ili pindi baada ya harusi kila mmoja awe amekubali mapungufu ya mwenzi wake.
 
Nivizur kushi kwanza kabla ya ndoa ili kusomana tabia then ndoa badae
 
mimi Nina ndugu Lakin mtu wa karibu niliekua na mtrust katangulia mbele ya haki na si kila mtu anatakiwa kukupa ushauri

Sent from my SM-A800F using JamiiForums mobile app

Sawa kama huko Nyumbani unakotaka Aje Kujitambulisha nako Upo Pekee yako Basi Sawa Ila kuna vitu Vingine kama Mke anayejua kuwa utakuja kuwa na Familia yako kuna Vitu unapashwa kuomba Ushauri na Kuna Vitu Hupashwi kuomba Ushauri.

Mfano Umemwambia kuwa aje Kwenu Amekataa, Bado Unaamini Kuna Mtu Humu Ndani atakupa Mbinu yakumbadirisha Juu ya Katazo Lake? Kama Hili Dogo tu Unashindwa Kulidadavua Mpaka unataka watu wakusaidie majibu na Uamzi Je siku Mtoto Akizaliwa si Ndiyo Utauliza hivi Mtoto Akiwa ananyoinya anavutaje Chuchu??

Tutumie Elimu Zetu Kutupanuwa na Kujua Majukumu Yetu baada ya kuacha Majukumu ya Usichana na Kuwa Mwanamke au Kuacha Uvulana na Kuwa Mwanamume.
 
Kuna Tofauti Kati ya Mvulana na Mwanaume
Kuna Tofauti kati ya Msichana na Mwanamke.

Wewe Bado ni Msichana bado Hujafika kuwa na akili za Mwanamke. Samahani
 
Inawezekana mleta mada ametoa taarifa nusunusu. Kwa imani na upeo wangu ninajua lazima kuna sababu kubwa ya kukuomba kuishi nawe ambayo moja wapo yawezekana kutokuwa vizuri kifedha na kimaisha kwa sasa kwa uwezo wa kufunga ndoa. Lakini kama kweli umeona nia yake kwa muda wote mliokuwa kwenye mahusiano yenu basi wewe nenda tu. By the way, mnamuda gani kwenye mahusiano yenu??
 
Ndugu zangu natumai hamjambo....hivi hili suala la mwanaume kumwambia mwanamke waishi bila ndoa then wafunge ndoa baadae mnalionaje.

Mimi mwenzenu niko njia panda baada ya boyfriend kusema tuishi bila ndoa.

Je faida na hasara zake hua ni zipi? kwa mliotangulia kuoa ama kuolewa naombeni msaada
We kaa hapo hapo njia panda, ukija kutahamaki wenzako wana watoto wako darasa la pili.

Hivi kwa nini mnapenda tuwaoe regardless ya ubutu wenu linapokuja suala la 'kuwa MKE'?
 
Inawezekana mleta mada ametoa taarifa nusunusu. Kwa imani na upeo wangu ninajua lazima kuna sababu kubwa ya kukuomba kuishi nawe ambayo moja wapo yawezekana kutokuwa vizuri kifedha na kimaisha kwa sasa kwa uwezo wa kufunga ndoa. Lakini kama kweli umeona nia yake kwa muda wote mliokuwa kwenye mahusiano yenu basi wewe nenda tu. By the way, mnamuda gani kwenye mahusiano yenu??
Another Immoral Advise
 
Ndoa kwanza ndiyo muishi pamoja. Usikubali kuishi pamoja kabla ya ndoa. Ukifanya hivyo ndoa ujue itaota mbawa.

Ndugu zangu natumai hamjambo....hivi hili suala la mwanaume kumwambia mwanamke waishi bila ndoa then wafunge ndoa baadae mnalionaje.

Mimi mwenzenu niko njia panda baada ya boyfriend kusema tuishi bila ndoa.

Je faida na hasara zake hua ni zipi? kwa mliotangulia kuoa ama kuolewa naombeni msaada
 
Inawezekana mleta mada ametoa taarifa nusunusu. Kwa imani na upeo wangu ninajua lazima kuna sababu kubwa ya kukuomba kuishi nawe ambayo moja wapo yawezekana kutokuwa vizuri kifedha na kimaisha kwa sasa kwa uwezo wa kufunga ndoa. Lakini kama kweli umeona nia yake kwa muda wote mliokuwa kwenye mahusiano yenu basi wewe nenda tu. By the way, mnamuda gani kwenye mahusiano yenu??
tuna 5 yrs na pesa sio tatizo mbona ni watu tunaojiweza

Sent from my SM-A800F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom