Nimekuelewa sana mleta mada
Sawa we lala kutwa nzima utii amri za mungu usipo geuka amba rutty
Umetolea mfano wa kuku hapo juu..ukasema hawatumiaa akili basi wanakutegema wewe, ukaweka mfano wa watoto pia (ukiwa mzazi) ukasema nao hawatumii akili wanafata amri zako! Sasa mkuu mbona hujasema sisi (wafuga kuku/wazazi) tusitumie akili tumfate nani??
Na je,kuhusu hao wanaotutegemea na kufata akili zetu (kuku/watoto) huoni kuwa wanafanya hivyo kwa sababu sisi tuna akili zaidi labda kuliko wao? sasa unataka na sisi tuache kutumia akili zetu hao wanaoishi kwa kutegemea akili zetu wataishije tena?
Kwa hiyo tuwe mazwazwa??
Tatizo kachanganya imani na maisha
Amri kumi za mungu hazitoi ugali usipotumia akili ugali utapataje?
Kuishi bila kutumia akili labda uwe tegemezi wa kutupwa.
Maandiko hayohayo yanasema asiyefanya kazi na asile.
Kijana! Kama unamwamini Mungu wako, basi fanya kazi huku ukimwimbia Mungu moyoni mwako
Je, waweza kufanya kazi pasipo kutumia akili? Wewe mleta mada hela ya kuweka bando na kununulia simu ulihongwa?
Kwahiyo tukubali wewe ni tegemezi kwa ndugu zako, jamaa na marafiki sio?
Hebu tuambie mwenzetu wewe unaishije hapa mjini bila kipato [emoji23]
KWANZA UNA FAMILIA?
Unajua hizi dini zimewaharibu akili sana
Mi naamini mtoa mada ana ujumbe mzuri na sahihi kabisa,ila maneno aliyoyatumia yanawa mis-lead baadhi ya watu.
"Kuisikiliza sauti ya Mungu ni salama zaidi kuliko logic"