Kuhusu Morogoro a.k.a mji kasoro bahari

Kuhusu Morogoro a.k.a mji kasoro bahari

Mapondo Mapoka

JF-Expert Member
Joined
Feb 10, 2015
Posts
274
Reaction score
135
Wadau,

Nimekuwepo hapa Moro town kwa zaidi ya miaka 4 lakini hapo awali nimekua nikiishi nakusoma hadi high school huko mikoani. Nikiwa huko mikoani nidhahiri watu wamekua wakiisifu moro kua ni mahali pazuri sana, pana karibia kuwepo na kila aina ya starehe,majengo mazuri na vingine vingi.

Nikweli Moro mfano kwa wasafiri wakifika round about ya msamvu panamandhari nzuri nayakuvutia kwani inadaiwa msamvu ndio round about nzuri na kubwa kwa hapa Tz, pia Moro kwa tafiti ndogo nilizozifanya watu wa mikoa mingine hupaona Morogoro mahali fulani pako vizuri sana.

Kwa mimi nilichokiona moro nipakawaida tu nisawa tu au hata kuzidiwa na manispaa zingine, miundo mbinu na sehemu za vitega uchumi kiukweli bado sana yaani nitofauti sana Moro inavyotafsiriwa na watu ambao huwa wanapita tu bila Msamvu.

Tulitegemea Moro pengine kwa kua iko karibu na Dar mkoa wenye makao makuu ya shughuli nyingi zenye tija pia ianunganisha barabara kubwa za kuelekea kusini,kaskazini na Magharibi basi pangekua na vitega uchumi vikubwa na vyenye tija lakini bado mambo yanayofanyika ya kawaida sana.

Sijui wewe mdau unauzungumziaje mkoa huu mji kasoro bahari?

Nawasilisha.
 
Magojwa ni mengi sana katika huu mji na pia kuna uchakachuzi mwingi sana hasa katika vitu vinavyotumiwa kimwili na mwanadamu,Moro ingeweza kuwa nzuri endapo miondombinu has a ya maji ingeboreshwa,lakini pia udhibiti wa bidhaa feki ni nyingi sana hapa na ndio zinapelekea magonjwa mengi.
 
uzuri wa moro ni kwenye wilaya zake siyo hapo mjini, nenda huko turiani sijui kilombero, kilosa and the like ndo utajua uzuri wa moro, hapo mjini hamna kitu
 
uzuri wa moro ni kwenye wilaya zake siyo hapo mjini, nenda huko turiani sijui kilombero, kilosa and the like ndo utajua uzuri wa moro, hapo mjini hamna kitu

Nadhani huko wilayani patakua pazuri zaidi ya Moro town japo panahadhi ya halmashauri ya mji
 
Huu mji maji nni shida sana halafu wahusika wako kimya huu mwaka hautaisha nnahama maana ddaah tabu tupu
 
yaani mji huu wa moro ukifika maeneo yanayozunguka stand kuu ya Msamvu ambayo nikiungo muhimu sana maeneo kama ya pale itigi kwa wadada poa wajiuzapo pia ndipo pana parking ya magari makubwa yaani utachoka,pamejaa vibanda visivyopangika na zaidi panavumbi la kutisha na nyakati za mvua ndio kabisa hovyoo.
 
maji yatiririka milimani ohoo. Morogoro ohoo kweli yapendeza kuna milima na mabonde. Sisi tunaokaa kihonda tunaishukia sana manispaa yetu maji ni sheeda kwa kweli
 
huku nanenane tumeshaona nikawaida yaani maji hutoka kila baada ya siku 12, nashindwa kujua nikwalipi moro imefanya vizuri na inastahili pongezi kwani kila kitu naona kawaida sana.
 
Wadau,nimekuwepo hapa Moro town kwa zaidi ya miaka 4 lakini hapo awali nimekua nikiishi nakusoma hadi high school huko mikoani. Nikiwa huko mikoani nidhahiri watu wamekua wakiisifu moro kua ni mahali pazuri sana, pana karibia kuwepo na kila aina ya starehe,majengo mazuri na vingine vingi.....

Nikweli Moro mfano kwa wasafiri wakifika round about ya msamvu panamandhari nzuri nayakuvutia kwani inadaiwa msamvu ndio round about nzuri na kubwa kwa hapa Tz, pia Moro kwa tafiti ndogo nilizozifanya watu wa mikoa mingine hupaona Morogoro mahali fulani pako vizuri sana.
Kwa mimi nilichokiona moro nipakawaida tu nisawa tu au hata kuzidiwa na manispaa zingine, miundo mbinu na sehemu za vitega uchumi kiukweli bado sana yaani nitofauti sana Moro inavyotafsiriwa na watu ambao huwa wanapita tu bila Msamvu.
Tulitegemea Moro pengine kwa kua iko karibu na
Dar mkoa wenye makao makuu ya shughuli nyingi zenye tija pia ianunganisha barabara kubwa za kuelekea kusini,kaskazini na Magharibi basi pangekua na vitega uchumi vikubwa na vyenye tija lakini bado mambo yanayofanyika ya kawaida sana.

Sijui wewe mdau unauzungumziaje mkoa huu mji kasoro bahari?
Nawasilisha.

Kwa hiyo hii ndo news alert!😀
 
Nimekaa hapa mwaka wa kumi na mbili sasa maendeleo ni madogo sana,mzunguko wa hela ni mdogo sana
 
Hapana mkuu hiyo sio news alert Jaribu kugoogle mkuu utapata uelewa zaidi wa news alert ni nini mkuu,Mara nyingi haiwi ndeefu kihivo na inatoa instant and brief information

Nashukuru mkuu kwa kunielimisha zaidi.
 
Kifupi Manispaa ya Morogoro, mkurugenzi au wakurugenzi wote waliowahi kupita walitakiwa kuchapwa viboko. Mfano mdogo ni soko kuu. Lipo hovyo ajabu, uchafu na nliwahi kuipita wakati wa mvua matope tupu utadhani shamba lililotifuliwa. Watendaji wangefanya wajibu wao pangependeza. Ni mji unaoweza kuumodernize
 
Magojwa ni mengi sana katika huu mji na pia kuna uchakachuzi mwingi sana hasa katika vitu vinavyotumiwa kimwili na mwanadamu,Moro ingeweza kuwa nzuri endapo miondombinu has a ya maji ingeboreshwa,lakini pia udhibiti wa bidhaa feki ni nyingi sana hapa na ndio zinapelekea magonjwa mengi.

Nimeuziwa power bank feki juzi makuti! ishirini yangu ina umaa
 
Ajabu mnalalamika kuhusu shida ya maji wakati ndio mkoa wenye vyanzo vya mito miwili mikubwa Kilombero na Ruvu achilia mbali vijito vya wastani.
 
maji yatiririka milimani ohoo. Morogoro ohoo kweli yapendeza kuna milima na mabonde. Sisi tunaokaa kihonda tunaishukia sana manispaa yetu maji ni sheeda kwa kweli
mkuu kihonda ggani hiyo mi nipo veta huku halafhalafu umeongea kweli kabisa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom